Na Mahmoud Ahmad Arusha
Serikali imetakiwa
kushirikiana kwa karibu na jumuiya ya waajiri katika kuleta maelewano katt ya
waajiri na wafanyakazi ambapo suala hilo litaleta tija na kukuza uchumi pia
kuondoa migogoro,
Kauli hiyo imetolewa na Raisi
wa chama cha waajiri Afrika na pia mwenyekiti wa waajiri hapa nchini Almas
Maige wakati akizindua kitabu cha muongozo wa shirikisho la waajiri Afrika Mashariki
jijini Arusha
Maige ambaye pia ni Mbunge wa
Tabora Kaskazini alisema kuwa maelewano kati ya waajiri ikiwemo mipango na mazingira
rafiki ya ufanyaji kazi kati yao utasaidia kuondoa matatizo na kuweka mazingira
mazuri katika kuendeleza na kukuza soko la ajira hapa nchini na wanajumuiya ya
Afrika mashariki.
Akitolea mfano tozo walizokuwa
wakitozwa waajiri na kusema kuwa punguzo la tozo hiyo kutoka dola 1000 hadi
dola 500 litasaidia katika kuboresha mazingira ya waajiri na kujiona ni sehemu
ya wawekezaji hapa nchini na kuwa Tanzania imekuwa nchi ya kwanza kuonyesha
mfano katika tozo hiyo
“Kumeokuwa na malalamiko mbali
mbali ambayo serikali imeweka mikakati ya mazingira mazuri katika kuboresha
maeneo m,bali mbali ya uwekezaji hapa nchini na muongozo huu niliozindua leo
utasaidia nchi za Afrika mashariki kuwa na uwiano mzuri kwa waajiri na
waajiriwa”alisema Maige
Nae Mkurugenzi wa Jumuiya wa
waajri Zanzibar(ZANEMA) Salahi Salimu)alisema kuwa mazingira yakiboreshwa kati
ya waajiri na waajiriwa na kuwa na maelewano kutaepusha migogoro ambayo
ingeweza kutokea na kusababisha kutoweza kukua kiuchumi kwa wahusika na Taifa
kwa ujumla.
Alisema kuwa maelwano kati ya
serikali yanaenda vizuri ila ifike mahali upanuliwe wigo mpana katika kuboresha
shughuli mbali mbali za sekta hizo mbili katika kupata mafanikio ya kiuchumi katika
waajiri na serikali zao.
“Uwepo wa maelewano kati ya
waajiri na wafanyakazi kutajenga mazingira mazuri yatakayosaidia kukua kwa maendeleo
na kuleta tija amba[po itaondoa migogoro ambayo haikuwa na lazima na hivyo
kusaidia ukuaji wa kiuchumi”alisema Salahi
Mwishooooooooooooo
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni