TRA YAKUSANYA ZAIDI YA TRILIONI 7.87 KWA KIPINDI CHA NUSU MWAKA 2017/2018



index

DK KIGWANGALA : WIZARA YA MALIASILI, ARDHI NA TAMISEMI KUAMUA HATMA YA MGOGORO WA PORI LA AKIBA MKUNGUNERO



Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akimsikiliza Mwenyekiti wa Kijiji cha Ikengwa, Mohammed Tabahi aliyekuwa akimunesha mpaka wa kijiji hicho na Pori la Akiba Mkungunero wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji.

Na Mahmoud Ahmad - Kondoa, Dodoma
.....................................................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla jana tarehe 7 februari, 2018 ametembelea Pori la Akiba Mkungunero katika Wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma na kuwataka wananchi wanaozunguka pori hilo kusubiri uamuzi wa Serikali utakaoshirikisha Wizara yake, Wizara ya Ardhi na Tamisemi katika kujibu maombi yao ya kutaka kupewa sehemu ya ardhi katika pori hilo kwa ajili ya kuendesha shughuli za kibinadamu.

Dk. Kigwangalla ambaye aliongozana na Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo, alitembelea vijiji vinne vya Ikengwa, Keikei Tangini, Keikei na Kisondoko na kufanya mikutano ya hadhara kwa ajili ya kujiridhisha na kujifunza juu ya mgogoro uliopo baina ya vijiji hivyo na Pori la Akiba Mkungunero.

"Nimefika hapa leo kujifunza juu ya mgogoro huu, nimejionea hali halisi lakini pia nina maelezo ya wataalamu ambayo yapo kwenye maandishi naomba niende nikayasome, niyatafakari ili niweze kushauriana na wenzangu na mwisho wa siku tuweze kuja na suluhu ya namna ya kuondokana na changamoto ambazo zimekuwepo.

"Niwaombe sana wakati Serikali inaendelea kutafuta suluhu ya mgogoro huu ni vema tukafuata sheria zilizopo, tuzingatie mipaka iliyowekwa ili tusiingie kwenye migogoro, lakini kwa sasa siwezi kwa namna yeyote ile kutamka neno la kujibu maombi ya mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji na wananchi yaliyotolewa hapa leo.

"Kama Serikali tutakaa, Wizara yangu, Wizara ya Ardhi na Tamisemi ili tujue kiini cha mgogoro huu tufanye uamuzi kuwa ni maeneo gani yaongezwe katika hifadhi kwa ajili ya wananchi au ni vitongoji vipi vifutwe, tutaleta majibu, na jambo hili tutalifanya kwa uadilifu mkubwa bila kumuonea mtu ili kumaliza mgogoro huu," alisisitiza Dk. Kigwangalla.

Awali akimkaribisha Waziri huyo kuzungumza na wananchi wa kijiji cha Ikengwa, Mbunge wa jimbo hilo, Dk. Ashatu Kijaji alisema kutokana na ukweli kuwa Serikali ya awamu ya tano inasikiliza kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi, ni vema Waziri huyo akatumia hekima na kuangalia uwezekano wa kuwapa wananchi hao Kilomita 12 za mraba kutoka kwenye hifadhi hiyo kwa ajili ya kuendesha shughuli zao za kibinadamu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Ikengwa, Mohammed Tabahi alisema mgogoro baina ya vijiji hivyo na Pori la Akiba Mkungunero ulinza mwaka 2006 kufuatia zoezi la kuanzishwa kwake pamoja na lile na uwekagi wa vigingi vya mpaka na vijiji jirani kutoshirikisha wananchi na viongozi wa halmashauri za vijiji hoja ambayo ilipigwa na Meneja wa Pori hilo, Emannuel Bilaso. 

Aidha alisema wananchi wa vijiji hivyo wanakabiliwa na uhaba wa maeneo ya kilimo na ufugaji, hivyo akamuomba Waziri huyo pamoja na Serikali kwa ujumla kutumia busara kuwamegea wananchi wa vijiji hivyo eneo la Kilomita 12 za mraba kwa ajili ya shughuli za kilimo na ufugaji.

Naye Meneja wa Pori hilo, Emannuel Bilaso alisema Pori la Akiba Mkungunero lilianzishwa kwa tangazo la Serikali Na. 307 la mwaka 1996 baada ya kupandishwa hadhi kutoka Pori Tengefu. Alisema mchakato wa kupandisha hadhi pori hilo ulishirikisha wananchi na viongozi wa vijiji na wilaya ambapo mihutasari mbalimbali ilisainiwa.

Alisema pori hilo linakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazochochea mgororo huo ikiwemo kijiji kimoja cha Kisondoko kusajiliwa kimakosa ndani ya hifadhi hiyo pamoja na malalamiko mbalimbali ya wananchi kuwa hawakushirikishwa kwenye uanzishwaji wa pori pamoja na madai mengine kuwa pori hilo limeingilia mipaka ya vijiji hivyo.

Pori la Akiba Mkungunero ambalo lina ukubwa wa Kilimita za Mraba 557.9 lina umuhimu mkubwa kiuchumi na kiikolojia kwa kuwa ni chanzo muhimu cha mto Tarangire ambao ni uhai wa hifadhi ya Taifa ya Tarangire na ikolojia nzima ya ziwa Manyara. Pori hilo pia ni sehemu ya mapito na mazalia ya wanyamapori pamoja na makazi ya wanyamapori adimu duniani.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akisalimiana na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kondoa muda mfupi baada ya kuwasili wilayana humo jana.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akioneshwa ramani ya Pori la Akiba Mkungunero na Mrasimu Ramani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa, Peter Nyange (kulia) wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akioneshwa mipaka ya Pori la Akiba Mkungunero na Mrasimu Ramani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa, Peter Nyange (kulia) wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa tatu kulia) akiteja jambo na Meneja wa Pori la Akiba Mkungunero, Emannuel Bilaso wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa pili kulia) akiteta jambo na Mwenyekiti wa Kijiji cha Ikengwa, Mohammed Tabahi wakati wa ziara yake ya kikazi jana katika Pori la Akiba Mkungunero Wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akipokea mabango ya malalamiko kutoka kwa wananchi wa kijiji cha Kisondoko kuhusu Pori la Akiba Mkungunero na vijiji jirani wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kisondoko wilayani Kondoa jana.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akioneshwa mipaka ya Pori la Akiba Mkungunero na mmoja wa wahifadhi wa Pori hilo wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji.



MGODI BUZWAGI WAZINDUA MAKTABA SHULE YA SEKONDARI BUGISHA KAHAMA


Mgodi wa dhahabu wa Acacia Buzwagi umezindua maktaba iliyogharimu shilingi milioni 22.4 kwenye shule ya sekondari Bugisha iliyopo katika kata ya Mondo wilayani Kahama mkoani Shinyanga kwa lengo la kusaidia wanafunzi na walimu kuchangia katika kuboresha ubora wa elimu inayotolewa.

Maktaba hiyo imezinduliwa leo Alhamis Februari 8,2018 na Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba na kuhudhuriwa pia na Meneja Mkuu wa Migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu,Benedict Busunzu.

Hii ni maktaba ya pili katika wilaya ya Kahama kuzinduliwa na mgodi huo ambapo mwaka 2017 mgodi wa Buzwagi ulianzisha maktaba ya jamii katika kata ya Kagongwa ili kutoa rasilimali za elimu ya aina mbalimbali kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla.

Akizungumza wakati uzinduzi huo, Meneja Mkuu wa Migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu,Benedict Busunzu maktaba hiyo itasaidia kuboresha upatikanaji wa elimu kwa wanafunzi kutoka jamii inayouzunguka mgodi wa Buzwagi.
Alisema kupitia mpango wa Acacia wa maendeleo ya jamii wameamua kushirikiana na shirika la kimataifa la Read International kuboresha jengo moja la shule hiyo na kuliwekea samani kwa ajili ya matumizi ya maktaba.

“Read International ni wadau wetu wakubwa hasa katika masuala ya elimu na wamekuwa chachu ya kuleta maendeleo,kwa kutambua umuhimu wao tuliamua kukaa chini na kuamua kukarabati jengo moja na kulifanya maktaba ili vijana wetu wapate mahali pa kupatia maarifa zaidi”,alieleza.

Busunzu alisema Acacia itaendelea kuunga mkono sekta ya elimu nchini kwa njia ya kujenga miundombinu ya shule kama vile vyumba vya madarasa,nyumba za walimu,vyoo na maabara na kutoa misaada kwa wanafunzi kupitia vifaa vya elimu mfano vitabu,sare na ada kupitia programu ya CanEducate.

“Misaada inayotolewa na Acacia katika sekta ya elimu ni sehemu ya sera ya wajibikaji kwa jamii ya kampuni inayojikita katika kuhakikisha jamii inakuwa endelevu kupitia sekta ya elimu na sera hiyo inachangia moja kwa moja maono ya taifa hadi kufikia mwaka 2025 na malengo ya nchi ya kuleta maendeleo endelevu kwa kuhakikisha jamii inapata elimu iliyo bora”,alieleza.

Naye Mwakilishi wa shirika la Read International linalojihusisha na masuala ya elimu,Esther Kalwinzi mgodi wa Buzwagi ndiyo uliotoa shilingi milioni 22.4 kwa ajili kukarabati darasa kuwa maktaba.“Jumla ya vitabu 1,278 vimehifadhiwa katika maktaba hii ambayo itahudumia wanafunzi wapatao 290 na walimu 23 na jumla ya gharama za marekebisho ya jengo hili,vitabu na samani za maktaba ni shilingi 22,442,953”,alifafanua Kalwinzi.

Kwa upande wake,mgeni rasmi katika hafla hiyo,Mkurugenzi wa Mji wa Kahama,Underson Msumba aliushukuru mgodi huo kwa kuendelea kuwa karibu na jamii inayowazunguka na kushirikiana katika shughuli za maendeleo.

“Wakati mwingine huwa nafikiria bila mgodi Kahama ingekuwaje,kwa kweli mgodi umefanya juhudi nyingi katika kuboresha sekta ya elimu katika wilaya yetu,ninaamini uwepo wa maktaba hii utawafanya wanafunzi kufanya vizuri zaidi katika masomo yao”,alisema Msumba.

Aidha aliwataka wanafunzi kuzingatia masomo yao huku akisisitiza kuwa elimu ndiyo urithi pekee wa kudumu na wenye kubadilisha maisha yao.
Muonekano wa jengo la maktaba katika shule ya sekondari Bugisha lililoboreshwa na mgodi wa Buzwagi kwa kushirikiana na Read International - Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kahama Mji Underson Msumba,meneja mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu ,viongozi mbalimbali wa kata ya Mondo,walimu na wanafunzi wakiwa nje ya jengo hilo la maktaba kabla ya kuzinduliwa rasmi
Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba akikata utepe kuzindua rasmi jengo la maktaba katika shule ya sekondari Bugisha. Katikati ni Meneja mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu.Wa kwanza kushoto ni Mwakilishi wa shirika la Read International ,Esther Kalwinzi akifuatiwa na diwani wa kata ya Mondo Kija Peja
Mwakilishi wa shirika la Read International ,Esther Kalwinzi akionesha sehemu ya kuangalia orodha/aina ya vitabu vilivyopo katika maktaba hiyo
Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba akiangalia vitabu katika maktaba ya shule ya sekondari Bugisha
Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba na Meneja mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu wakisoma vitabu ndani ya maktaba ya shule ya sekondari Bugisha
Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba akiangalia mandhari ya maktaba hiyo
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kahama Mji Underson Msumba,meneja mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu ,viongozi mbalimbali wa kata ya Mondo,walimu na wanafunzi wakiwa nje ya jengo la maktaba baada ya uzinduzi
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kahama Mji Underson Msumba akiwasisitiza wanafunzi kuzingatia masomo yao
Meneja mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu akielezea namna walivyoshirikiana na shirika la Read International katika kufanikisha ukarabati wa jengo hilo la maktaba
Mwakilishi wa shirika la Read International ,Esther Kalwinzi akizungumza wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa jengo la maktaba katika shule ya sekondari Bugisha
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kahama Mji Underson Msumba
Mkuu wa shule ya sekondari Bugisha Limbuzizi Magumba akiushuru mgodi wa Buzwagi kwa kutoa shilingi milioni 22.4 kwa ajili ya ukarabati wa maktaba katika shule yake
Wanafunzi wa shule ya sekondari Bugisha wakiimba shairi wakati wa hafla ya kuzindua maktaba katika shule hiyo
Mwanafunzi Tedy Martine akisoma risala akisoma risala kwa mgeni rasmi.Alizitaja miongoni mwa changamoto zilizopo katika shule hiyo kuwa ni upungu wa viti na meza hali inayowafanya wakae wawili wawili lakini pia upungufu wa walimu wa masomo ya sayansi.
Diwani wa kata ya Mondo Kija Peja akiushukuru mgodi wa Buzwagi kwa kuendelea kusaidia jamii na kuomba ushirikiano uendelee kuwepo.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Wawindaji wa Panya Rukwa Kukomeshwa


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akipanda mti katika shule ya msingi Mpwapwa, kata ya Mpwapwa Wilayani Sumbawanga ikiwa ni kampeni ya kufikisha miti Milioni 6 kwa Mkoa kwa mwaka 2017/2018.
Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dk. Khalfan Haule akisaidiana na mwanafunzi wa darasa la kwanza Shule ya Msingi Mpwapwa Joanita Mwanandenje kupanda mti ili kuwahamasisha wanafunzi kuwa na utamaduni wa kupanda miti na kufikisha miti milioni 3 kwa Wilaya ya Sumbawanga.
Mjumbe wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa ACP George Kyando akijiandaa kuapanda mti katika Shule ya Msingi Mpwapwa ikiwa ni kampeni ya Mkoa kufikisha miti milioni 6 na kuhifadhi mazingira ya Mkoa.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akikabidhi miche kwa Didas Kosam M/kiti wa kitongoji cha Katupa, Kijiji cha Mpwapwa chenye vitongoji vinne. Ambapo kila kitongoji kilipewa miche 200.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo
Mjumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Rukwa, Afisa Uhamiaji Mkoa Carlos Haule akipanda mti nje ya Zahanati ya Mpwapwa ikiwa ni kuendeleza kuhamasisha kampeni ya upandaji miti Rukwa. 

……………

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Sumbwanga Dk. Khalfan Haule kuhakikisha anatafuta dawa ya kuulia panya wakiwa mashambani ili kuokoa miti kutokana na uchomaji wa misitu kwasababu ya uwindaji wa panya.

Amesema kuwa ameisikia changamoto hiyo ya uchomaji wa misitu kwasababu ya uwindaji wa panya kutoka kwa vijana mbalimbali wanaojishughulisha na mashamba ya upandaji miti pamoja na taarifa iliyosomwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga juu ya changamoto za kuendeleza misitu.

“DC tafuta dawa ya panya, wauliwe huko mashambani, ili panya wasiwepo na miti iokoke, mbona hamshangilii? Hawa panya tutawaua kwa sumu huko mashambani wasiwe chanzo cha mioto ambayo mnachoma huko kuwatafuta hawa panya ili wafie huko huko mashimoni msiwapate,” Alisisitiza.

Agizo hilo amelitoa katika muendelezo wa kampeni ya upandaji miti mijini na vijijini katika Kijiji cha Mpwapwa, kata ya Mpwapwa, Wilayani Sumbwanga baada ya kuwauliza wananchi wa Kijiji hicho juu ya changamoto aliyoisikia ya uchomaji wa moto misitu kutokana na kuwinda panya, japo wananchi walikataa.

Pia katika kuongezea hilo alimuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kuhakikisha anasimamia sheria ya hifadhi ya mazingira na kuwawajibisha wote wanaohusika na uharibifu wa mazingira.

Nae akisoma taarifa Mkurugenzi wa H/W ya Sumbawanga Nyangi Msemakweli alibainisha kuwa miongoni mwa changamoto ni muitikio mdogo wa uhifadhi wa mazingira pamoja na mila na tamaduni za wananchi za uwindaji wa panya hali inayosababisha uchomaji wa misitu wakati wa kiangazi.

“Changamoto nyingine ni baadhi ya viongozi wa serikali ya Kijiji kujihusisha na uuzajia wa maeneo yaliyotengwa kwaajili ya hifadhi ya Kijiji na usimamizi mdogo wa sheria ndogo za vijiji katika utunzaji wa misitu,” Alimalizia.

Mmoja wa vijana wanaojishughulisha na upandaji kiti wa kibiashara Julius Magaga alimweleza Mh. Wangabo kuwa chnagmoto inayowakatisha tamaa vijana wengi ni kutokana na uwindaji wa panya uliokithiri na kusababisha hasara katika misitu.

Kwa msimu wa 2017/2018 hadi 30/1/2018 Halmashauri ya Wilaya ya Sumbwanga imepanda miti 830,527 ambayo ni sawa na 55.4% na ina misitu 92 yenye ukubwa wa jumla ya Hekta 49,179.6. Huku Mh. Wangabo akigawa miche 850 kwa kaya 850 za Kijiji cha Mpwapwa, Wilayani Sumbawanga.

MKUU WA WILAYA YA KIBAHA ASSUMPTER MSHAMA ATOA SIKU TISINI KWA MWEKEZAJI KURUDISHA HEKARI 5000 KWA WANANCHI WA KIJIJI CHA LUKENGE


Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Assumpter Mshama akizungumza na umati wa wananchi wa kijiji cha Lukenge kata Magindu hawapo pichani katika mkutano wa adhara ambao aliuandaa kwa ajili ya kuweza kutatua mgogoro wa aradhi kati ya wananachi hao na mwekezaji ambao umedumu kwa kipindi kirefu
Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Assumpter Mshama akiwa anatoka kwenye mkutano na wananchi wa kijiji cha lukenge alipokwenda kwa ajili ya kumaliza sakata la mgogoro baina ya wananachi hao pamoja na mwekezaji.
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha lukenge wakiwa wanamsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Assumpter Mshama wakati wa mkutano wa adhara ambao uliandaliwa kwa ajili ya kusikiliza mgogoro uliopo katia ya wananchi na mwekezaji.
Wananchi wa kijiji cha lukenge wakiwa wameshika mabango yaliyokuwa yameandikwa ujumbe wa kumkataa mwekezaji huyo, ambapo walipita mbele kwa ajili ya kuweza kumuonyesha Mkuu wa Wilaaya ya Kibaha.
PICHA ZOTE NA VICTOR MASANGU



NA VICTOR MASANGU, KIBAHA PWANI

SERIKALI wilayani Kibaha,Mkoa wa Pwani imemtaka mwekezaji ambaye alichukua eneo lenye ukubwa wa hekari zipatazo 5000 za ardhi bila ya kuzingatia sheria na taratibu kuzirudisha kwa kipindi cha siku tisini kutokana na kushindwa kuliendeleza kwa kipindi cha zaidi ya miaka nane kama walivyokubaliana katiba mkataba na wananchi wa kijiji cha lukenge kata ya Magindu.


Sakata la mgogoro wa ardhi baina ya wananchi hao na mwekeaji limechukua sura mpya kufuatai Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Assumpter Mshama baada ya kupokea malalamiko mengi kutoka kwa wananchi hivyo kumtaka mwekezaji huyo kuzirudisha hekari hizo 5000 kwa wananchi ambazo alikuwa amepewa na serikali ya kijiji kwa ajili ya uwekezaji wa ufugaji wa kisasa wa ng’ombe pamoja na samaki lakini ameshindwa kutekeleza makubaliano aliyopatiwa hapo awali.


Akizungumza katika mkutano maalumu wa adhara ambao uliandaliwa kwa ajili ya kujadili sakata hilo Mkuu huyo wa Wilaya amesema eneo hilo mwekezaji huyo alipewa kwa ajili ya kuliendeleza lakini amekuwa akijinufaisha mwenywe na kuwanyonya wakazi wa eneo hilo bila ya kuwaletea maendeleo ya aina yoyote tofauti na makubaliano yao.


Kwa upande wake aliyekuwa Mwenyekiti wa zamani wa kijiji hicho cha Lukenge Seif Maleta ambaye kwa sasa amemaliza muda wake amesema kwamba eneo hilo la hekari 5000 hawakumuuzia mwekezaji huyo ila walimpatia kulitumia kwa muda tu kwa ajili ya kuweza kufanyia shughuli zake mbali mbali za ufugaji wa ng’ombe na samaki kwa makubaliano maalumu.

Naye mwekezaji huyo ambaye analalamikiwa na wananchi anayejulikana kw ajina la Tangono Kashima alisema kwamba eneo hilo la uwekezaji wa ng’ombe alilipata kwa kuzingatia taratibu za serikali ya kijiji kwa kuandika barua maalumu kwa ajili ya kuomba eneo hilo kwa ajili ya kufuga ufugaji wa kisasa wa ng’ombe pamoja na kuchimba bwawa kwa ajili ya ufugaji wa samaki

ENEO hilo la ardhi lililopo katika kijiji cha lukenge kata ya magindu katika halmashauri ya Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani lina ukumbwa wa hekari zipatazo 5000 na kwa sasa limeingia katika mgogoro mkubwa baina ya wananchi pamoja na mwekezaji huyo kutokana na kukiuka kanuni na sheria za umiliki wa ardhi.

JAFO ASHUSHA NEEMA YA LAMI CHANG’OMBE, AMFAGILIA MAVUNDE KWA UCHAPAKAZI WAKE



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mhe.Selemani Jafo akiwa na viongozi mbalimbali katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.
                                              jiwe la msingi la soko la Chang'ombe
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mhe.Selemani Jafo akizungumza katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dk.Binilith Mahenge akizungumza katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.
Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akizungumza katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.
Baadhi ya bidhaa zilizopo soko la Chang'ombe
Soko lenyewe la Chang'ombe
Viongozi mbalimbali katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.
Wafanyabishara wa Soko la Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mhe.Selemani Jafo akitembelea soko la Chang'ombe mara baada ya kuzindua.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mhe.Selemani Jafo akisalimiana na wananchi na wafanyabiashara wa soko la Chang'ombe.




Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mhe.Selemani Jafo, amemfagilia Mbunge wa Jimbo la Dodoma Anthony Mavunde kwa jitihada zake za kuwaletea maendeleo kwa wananchi wake, huku akiuagiza Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) kuhakikisha katika bajeti yao ya mwaka 2018/19 wanaingiza kwenye mpango ujenzi wa barabara ya lami Chang’ombe hadi Chuo cha Mipango. 

Jafo ameyasema hayo leo alipokuwa anazindua soko jipya la kisasa kwa ajili ya wafanyabiashara ndogo ndogo kata Chang’ombe lililojengwa na Serikali kwa kusaidiana na wafanyabiashara na Mbunge Mavunde ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Vijana.

Ujenzi wa soko hilo ulianza mwaka 2017 na kukamilika mapema mwaka huu na litakuwa na wafanyabiashara wa bidhaa mbalimbali takribani 342 na limegharimu kiasi cha Sh.Milioni 70.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Waziri Jafo amesema katika ziara zake za miradi ya maendeleo alizotembelea katika Manispaa ya Dodoma, Mbunge Mavunde ameonekana kushiriki katika kila sekta kwa kusaidiana na wananchi.

“Katika kila taarifa ya mradi wa maendeleo inayosomwa,unaonesha Mbunge wenu Mavunde amechangia kwa kweli nimpongeze sana kwa kushiriki kuleta maendeleo kwa wananchi wake, ni mchapakazi.Nawapongeza katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 mlilamba dume kila eneo ninaloenda nakuta nyayo zake, Naahidi kumpa ushirikiano wa kutosha,”amesema jafo

Amesema katika ujenzi wa soko hilo Mbunge huyo amesaidiana na wananchi na kufanikisha kukamilisha ujenzi wake na kuahidi kuendelea kuboresha miundombinu ya Dodoma ili iendane na hadhi ya Makao Makuu ya nchi.

Waziri Jafo amesema Serikali inawekeza miundombinu ya hali ya juu katika mkoa wa Dodoma ikiwemo mtandao wa barabara za lami katika maeneo mbalimbali pamoja na taa za barabarani ikiwa ni pamoja na ujenzi wa dampo la kisasa.“Kwa kuwa serikali inahamia Dodoma hivyo basi miundombinu mbalimbali lazima iendelee kujengwa na kurekebishwa,” Amesisitiza Mhe. Jafo

Aidha Waziri jafo amewapongeza wananchi kwa kushirikiana na Halmashauri ya Manispaa kukamilisha ujenzi wa soko la kisasa na kwamba limejengwa kwa gharama nafuu sio kama masoko mengine yanayojengwa kwa gharama kubwa. 

Pia ameupongeza Uongozi wa Mkoa wa Dodoma pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge na Mkurugenzi wa Manispaa Godwin Kunambi kwa jitihada za kuwaletea maendeleo wananchi.

Amemuagiza Mkurugenzi Kunambi kukamilisha masoko mbalimbali pamoja na kuanza kutumika kwa machinjio ya kuku yaliyopo soko la majengo ipasavyo kwa kuwa kuna taarifa kuku wanaenda kuchinjwa maeneo mengine na kuacha machinjio ya eneo hilo.

Kwa upande wake, Naibu Waziri Mavunde amesema ujenzi wa soko hilo ni ahadi aliyoitoa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2015 na kwamba yataendelea kujengwa masoko ya kisasa yanayoendana na hadhi ya Makao Makuu ya Nchi.

“Pia kipekee niwashukuru wananchi wangu hasa wafanyabiashara kwa kuchangia ujenzi wa soko hili, pia na Mbunge wa jimbo la Mbarali Mhe.Haroun alinisaidia hapa kifusi malori 70 kwa ajili ya kushindilia chini.Niliahidi kuwatumikia na sitawaangusha nitakuwa nanyi bega kwa bega nanyie nawaomba mniunge mkono,”amesema Mavunde

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amempongeza Mavunde kwa kazi anayoifanya ya kuwaletea wananchi maendeleo na kuwataka wananchi kumuunga mkono ili aweze kuwatumikia ipasavyo.Kadhalika, Mkurugenzi Kunambi amesema Manispaa imepangwa vizuri kwa kuwa kila kata imetengewa eneo kwa ajili ya soko na kwamba Manispaa hiyo imejipanga kutengeneza masoko hayo.

Aidha amesema mwezi Machi mwaka huu utaanza ujenzi wa stendi kubwa ya kisasa ya mabasi yaendayo mikoani na soko la kisasa katika eneo la Nzuguni.