Leo Februari 24,2016 ,Chama cha 
Kimataifa kinachotoa misaada mbalimbali ya Kijamii cha Lions Club 
International chenye makao yake makuu nchini Marekani kimetoa msaada wa 
madawati 165 yenye thamani ya shilingi milioni 18 katika shule ya msingi
 Town na Mwenge zilizopo katika manispaa ya Shinyanga ili kumaliza 
changamoto ya wanafunzi kukaa chini.
 
Pichani viongozi wa wilaya ya Shinyanga,wazazi na maafisa kutoka Lions Club International wakiongozwa na Gavana
 wa Lions Club katika nchi ya Tanzania, Uganda na Sudani ya Kusini bwana
 Hyderali Gangji wakiwa katika shule ya msingi Town...Madawati hayo 165 
yametolewa na Lions Club ya mkoa wa Mwanza.Mwandishi mkuu wa Malunde1 
blog,Kadama  Malunde ametuletea picha 30 kilichojiri mwanzo hadi mwisho.
 Gavana wa Lions Club International 
 katika nchi ya Tanzania na Uganda na Sudani ya Kusini Hyderali Gangji 
alisema wamekuwa wakitoa misaada mbalimbali mkoani Shinyanga ambapo 
mwaka jana walitoa msaada wa chakula kwa wahanga wa mvua ya Mwakata 
wilayani Kahama,pia chakula katika kituo cha walemavu wa ngozi cha 
Buhangija,kutoa madawati katika shule ya msingi Town na Mwenge
Miongoni mwa madawati ya chuma 165 
yaliyotolewa na Lions Club International katika shule ya msingi Town na 
Mwenge katika manispaa ya Shinyanga
 Hapa ni katika shule ya msingi Town 
katika manispaa ya Shinyanga ,aliyesimama ni mwenyekiti wa bodi ya shule
 hiyo Said Juma Issa akiwakaribisha viongozi mbalimbali waliofika katika
 shule wakati wa hafla fupi ya kukabidhi madawati 65 kwa shule hiyo na 
100 katika shule ya msingi Mwenge
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Town wakiangalia madawati waliyopewa na Lions Club International 
 Kulia ni diwani wa kata ya Shinyanga 
mjini,ambaye pia ni meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Hafeez Mukadam 
aliyefanya jitihada za kupatikana kwa madawati katika shule za kata 
yake,Town na Mwenge.Diwani huyo pia ni mwanachama wa Lions Club International 
 Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Town 
Josephine Mabula akisoma risala kwa mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya 
Shinyanga Josephine Matiro ambapo alisema shule hiyo yenye wanafunzi 
1104 sasa haina uhaba tena wa madawati baada ya kupokea kutoka Lions Club International 
 Kulia ni mkurugenzi wa manispaa ya 
Shinyanga Lewis Kalinjuna,katikati ni mgeni rasmi,ambaye ni mkuu wa 
wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akifuatiwa na gavana wa Lions Club International  katika nchi ya Tanzania na Uganda na Sudani ya Kusini Hyderali Gangji
 Mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga 
Lewis Kalinjuna akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi madawati,ambapo
 mbali na kuipongeza Lions Club International 
 kwa kutoa msaada huo,aliwataka madiwani wa manispaa ya Shinyanga 
kufanya kazi badala ya kukalia maneno maneno kwani kiongozi mzuri 
anapimwa kwa maendeleo anayowaletea wananchi wake.
 Mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga 
Lewis Kalinjuna alisema hivi sasa manispaa hiyo imeanza kutoa shilingi 
milioni 10 kila mwezi kwa ajili ya kutatua changamoto ya uhaba wa 
madawati katika shule za manispaa hiyo huku akiwataka wananchi kuendelea
 kuisaidia serikali kwa michango mbalimbali ili watoto wasome vizuri
Gavana wa Lions Club International 
 katika nchi ya Tanzania na Uganda na Sudani ya Kusini Hyderali Gangji 
akizungumza katika hafla hiyo ambapo alisema wameamua kutoa msaada huo 
ili kuwaondolea changamoto wanafunzi ya kukaa chini wakati wa masomo ili
 kuinua kiwango cha elimu hapa nchini ikiwa ni moja ya majukumu yao 
kusaidiaa jamii na serikali.Alitumia fursa hiyo kuwataka wananchi 
kujenga moyo wa kutoa kwani serikali pekee haiwezi kumaliza matatizo ya 
wananchi
 Wanachama wa Lions Club International  mkoa wa Shinyanga wakiwa eneo la tukio,ambao wameahidi kupaka rangi majengo ya shule ya msingi Town
 Wazazi na walezi wa wanafunzi wakishuhudia kilichokuwa kinaendelea
Gavana wa Lions Club International 
 katika nchi ya Tanzania na Uganda na Sudani ya Kusini Hyderali Gangji 
akijiandaa kukata utepe wakati wa hafla fupi ya kukabidhi madawati 165 
kwa shule ya msingi Town na Mwenge zilizopo katika manispaa ya Shinyanga
 Gavana wa Lions Club International  katika nchi ya Tanzania na Uganda na Sudani ya Kusini Hyderali Gangji tayari amekata utepe.... 
 Gavana wa Lions Club International 
 katika nchi ya Tanzania na Uganda na Sudani ya Kusini Hyderali Gangji 
akishikana mkono na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro baada 
kukabidhi madawati 165 
 Wanafurahia jambo.....
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akimshukuru Gavana waLions Club International 
 katika nchi ya Tanzania na Uganda na Sudani ya Kusini Hyderali Gangji 
kwa kutoa msaada wa madawati katika shule za manispaa ya 
Shinyanga,ambapo alitangaza kujiunga na klabu hiyo ili kuungana na 
wanachama wengine wa klabu hiyo ambayo imekuwa msaada mkubwa kwa jamii
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro aliishukuru Lions Club International 
 kwa kuisaidia serikali kuchangia shule hizo huku akipongeza jitihada za
 diwani wa kata hiyo kupigania shule zake kupata msaada huo wa madawati.
 
 
Matiro alitumia fursa hiyo kuwataka 
madiwani wa manispaa ya Shinyanga kuiga mfano wa diwani wa kata ya 
Shinyanga mjini Gulam Hafeez Mukadam ambaye amemaliza tatizo la uhaba wa
 madawati katika shule za msingi katika kata yake huku akiwataka kufanya
  kazi ili kuwaletea maendeleo wananchi  badala ya kuendekeza siasa na 
maneno yasiyokuwa na faida kwa wananchi

 
Aliyesimama
 ni katibu wa Lions Club ya Shinyanga bwana Sandip  Lakhan akizungumza 
katika hafla hiyo ya kukabidhi madawati.Alisema Lions Club ya mkoa wa 
Shinyanga imetoa baiskeli kwa mkazi wa Bubiki wilayani Kishapu mkoani 
Shinyanga Mussa Mipawa,ambaye ni mlemavu wa viungo,iliyotengenezwa na 
mwanachama wa Klabu hiyo
Mussa Mipawa akiwashukuru wanachama wa Lions Club International kwa kumpa msaada wa baiskeli ya magurudumu matatu
 
 
Bwana Mussa Mipawa akishikana mkono na mke wa Gavana wa Lions Club International  katika nchi ya Tanzania na Uganda na Sudani ya Kusini Hyderali Gangji 
Bwana Mussa Mipawa akiwa katika baiskeli yake

 
Bwana Mussa Mipawa akiondoka na baiskeli yake-Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog Shinyanga
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni