Na Raymond Mushumbusi MAELEZO
Kutokana na tabia ya baadhi ya 
mgambo katika Halmashauri za Jijini la Dar es Salaam kujipatia fedha kwa
 njia zisizo za halali, serikali kupitia Halmashauri zake imejipanga 
kuwachukulia hatua za kisheria migambo wote watakaobainika 
kujishirikisha na vitendo vya rushwa.
Akitoa ufafanuzi juu ya madai ya 
wanachi juu ya mgambo wanaochukua rushwa nje ya faini halali 
zinazistahili kutozwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Wilaya ya Ilala,
 Afisa Habari wa Manispaa ya Ilala Tabu Shabibu amesema kuwa zipo baadhi
 ya taarifa wamepewa na watawachukulia hatua kwa kuwasitishia mikataba 
wale wote watakaobainika kukiuka sheria na taratibu za kazi.
“ Wapo mgambo ambao watumia 
vitambulisho feki na kufanya vitendo vya rushwa bado hatujawakamata ila 
 hatutawafumbia macho tutawachukulia hatua kali za kisheria kwa yoyote 
atakayekamatwa akipokea rushwa na hata wale watakaotoa rushwa”
“Napenda kuwaasa watanzania 
kuacha kuwapa fedha mgambo ili kukwepa kulipa faini halali hivyo basi 
nawaasa watu kutii Sheria bila shuruti kama umefanya kosa kwa mujibu wa 
Sheria lipa faini kwa mujibu wa Sheria lipa faini halali ili tuondoe 
vitendo vya rushwa na kuiongezea mapato Serikali ”Alisema Tabu.
Afisa Tabu amewaomba watanzania 
kutoa taarifa za mgambo wote wanaopokea rushwa na kusisitiza kuwa tabia 
hii inayoendelea ikome mara moja na mgambo wote watakaobainika 
kujihusisha na vitendo vya rushwa watasitishiwa mikataba yao ya kazi kwa
 kukiuka maadili ya kazi zao
.
Mgambo katika Jiji la Dar es 
Salaam wamekuwa wakilalamikiwa kwa kuchukua rushwa kuanzia shilingi 
5,000/= mpaka 10,000/= badala ya kutoza faini ya shilling 50,000/= 
inayostahili kutoza kwa wale wanaokiuka kanuni na taratibu za afya na 
mazingira katika Halmashauri mbalimbali.
Katika kupambana na suala la 
mgambo wasio waadilifu,Halmashauri zimejipanga kuwaajiri vijana 
walipitia mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) waliopata mafunzo 
yenye yenye kujenga uadili na uwajibikaji katika kazi ili kudhibiti 
suala la mmomonyoko wa maadili na utendaji kazi mbovu wa mgambo katika 
Halmashauri mbalimbali. 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni