Na Dotto Mwaibale 
KAMPUNI ya Blogu ya Wananchi Media kesho itaadhimisha miaka mitatu tangu
 kuanzishwa kwake, sherehe itakayofanyi Hyatt Regency Kempisky zamani 
Kilimanjaro jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, Mkurugenzi wa 
blogu hiyo, Wiliam Malecela (Le Mutuz), alisema kuwa wameamua kufanya 
sherehe kutokana na mafanikio waliyopata katika kipindi hicho, bendi ya 
muziki wa kizazi kipya ya THT itatumbuiza.
Alisema licha ya kesho kufanya sherehe , leo itakuwa na semina maalumu 
ya vijana 300, ambao watakuwa pamoja na matajiri 6 vijana na vijana 
watatu viongozi wa wa kitaifa kwa lengo la kubadilishana 
mawazo na matajiri na viongozi hao, ambao wataeleza walivyopigana mpaka 
kufikia walipo kimaisha.
Alisema alianzisha blogu hiyo baada ya kuisajili kwa msajili wa 
makampuni (Brela) 2012, ikianza kwa kutembelewa na watu 200 kwa siku 
lakini kwa sasa inatembelewa na watu 70,000 mpaka 100,000 kwa siku kitu 
ambacho anajivunia na kuwashukuru wadau.
Kampuni hiyo ilianza kwa mtaji wa dola ya Marekani 500, ikiwa na usajili
 wa makampuni wa Brela, na inatoa ajira kwa vijana 4 waliomaliza vyuo 
vikuu nchini na ina ofisi yake katika jengo la Tancot House Sokoine 
Drive, Dar es Salaam.
Alisema katika miaka mitatu blogu imeweza kuwa na domain yake wenyewe ya www.williammalecela.com
 na kuingia kwenyeFacebook, Twitter, na Instagram ambapo sasa 
inarusha habari sehemu mbalimbali kwa wakati mmoja na kuweza kuwafikia 
watu hadi 500,000 kwa siku.
Alisema mipango ya baadaye ni kuwekeza kwenye kampuni mpya ya African Swahili Media Radio Television ambayo tayari
 imeshapata leseni ya kufungua radio na televisheni ambayo inatazamiwa 
kuwa hewani Aprili mwaka huu, kituo cha radio kitakuwa 
Morogoro na televisheni Dar es Salaam, anatarajia kutoa ajira 
zaidi angalau kwa vijana 10
Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni