● Aziagiza Halmashauri kushughulikia migogoro ya ardhi .
● 
Azitaka kulisaidia Shirika la Nyumba ili lijenge nyumba za gharama 
nafuu● Asema Halmashauri zinunue nyumba zinazojengwa na NHC kwa ajili ya
 watumishi wao.
● Alipongeza NHC kwa kasi ya ujenzi wa nyumba bora katika Halmashauriza Miji na Wilaya.
Naibu
 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Angeline 
Sylvester Lubala Mabula akisalimiana na Watumishi wa Hamashauri ya Mji 
wa Buchosa alipowasili kusikiliza na kutatua migogoro ya ardhi
Naibu
 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Angeline 
Sylvester Lubala Mabula akipewa maelezo na mtaalam wa mifumo ya uwekaji 
kumbukumbu za umiliki wa ardhi alipotembelea idara ya ardhi Wilayani 
Misungwi. Aliyoko katikati ni Mkurugenzi wa Halmshauri hiyo Bw. Mshana.
Naibu
 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Angeline 
Sylvester Lubala Mabula na Mbunge wa Chato Mhe.Dkt Medard Kalemani 
wakikagua eneo la Kijiji cha Rusungwa lenye mgogoro mkubwa wa ardhi 
unaofanya wananchi wa kijiji hicho kukosa ardhi ya kulima na uwekaji 
huduma za jamii kama shule baada ya eneo la ekari 500 la kupewa 
mwekezaji.
Meneja
 wa NHC Mkoa wa Kagera Bw. Deogratius Batakanwa akimpewa maelekezo na 
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Angeline 
Mabula ya kuhakikisha kuwa anatoa elimu ya kutosha itakayowezesha 
wananchi, taasisi na Halmashauri ya Muleba kukamilisha ununuzi wa nyumba
 zilizojengwa na NHC Wilayani Muleba.Naibu Waziri alitembelea nyumba 
hizo na kulipongeza Shirika la Nyumba kwa ujenzi wa nyumba bora.
Naibu
 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Angeline 
Sylvester Lubala Mabula akiwa katika picha ya pamoja na Madiwani wa 
Halmashauri ya Muleba baada ya kuhutubia Baraza lao na kuliomba 
liwezeshe ununuzi wa nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC 
Wilayani humo. Pia aliagiza Baraza hilo kushiriki kikamilifu katika 
kutatua migogoro mingi ya ardhi iliyoko katika Wilaya hiyo.
Naibu
 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Angeline 
Sylvester Lubala Mabula akikagua nyumba zilizojengwa na NHC eneo la 
Bombambili Mkoani Geita kwa ajili ya kuuza. Amewataka wananchi na 
Halmashauri ya Mji wa Geita kununua nyumba hizo ili kuliwezesha Shirika 
kuendelea kujenga nyumba katika Halmashauri zingine.
Naibu
 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Angeline 
Sylvester Mabula akiwa na Mbunge wa Chato Mhe. Dkt Medard Kalemani 
ambaye pia ni Naibu Waziri wa Nishati na Madini wakikagua nyumba za 
gharama nafuu zinazojengwa na NHC Wilayani Chato. Katika ziara hiyo 
Naibu Waziri ameishauri Halmashauri ya Chato kununua nyumba hizo ili NHC
 iongeze ujenzi wa nyumba zingine kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya 
nyumba Wilayani humo.
Naibu
 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Angeline 
Sylvester Lubala Mabula akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi za NHC 
Mkoa wa Kagera alipotembelea na kusalimiana na wafanyakazi wa Shirika 
hilo.
Meneja
 wa NHC Mkoa wa Mwanza Injinia Benedict Kilimba akitoa maelezo ya mradi 
wa nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC Bombambili Geita, kwa 
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Angeline 
Mabula alipotembelea mradi huo. Mhe. Naibu Waziri ameziagiza Halmashauri
 nchini kusaidia uwekaji wa miundombinu kwenye maeneo ya ujenzi wa 
nyumba hizo pamoja na kutoa ardhi bure kwa NHC ili nyumba zinazojengwa 
ziwe na gharama nafuu kwa mnunuzi.
Mkuu
 wa Wilaya ya Misungwi Bibi Mwajuma Nyiruka akitoa taarifa ya sekta ya 
ardhi ya Wilaya yake kwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya 
Makazi, Mhe. Dkt Angeline Sylvester Lubala Mabula alipoitembelea 
Halmashauri ya Misungwi kusikiliza na kutatua migogoro ya ardhi.
Baraza
 la Madiwani Muleba wakimsikilza Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na 
Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt Angeline Mabula (hayuko pichani) 
alipohutubia Baraza hilo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni