Wananchi
 wa Eneo la Tegeta Nyuki Jijini Dar es Salaam wamelilalamikia Shirika la
 TANESCO kushindwa kutatua Kero ya Nguzo ambayo inahatarisha Maisha ya 
wakazi Hao katika eneo hilo kwa zaidi ya Miaka 8 hivi sasa, nguzo hiyo 
imesogelea Kibanda cha Biashara na kusababisha hali ya Sinto fahamu 
kufuatia usalama wao.

Wakizungumza
 na Mtandao huu wakazi wa Eneo hilo wamedai yakuwa Taarifa walisha 
peleka katika sehemu husika lakini Hadi leo hii ni mwaka wa Nane Bila ya
 Mafanikio.
Mwaka
 2008 wakazi hao waliiandikia Tanesco Barua ya kufanya Marekebisho ya 
Kuomba Kuondoa Mstimu huo lakini hadi leo Mamlaka hiyo haijafanya hivyo,
 Ila Mwaka 2015 mwishoni Tanesco ilifika eneo la tukio na kuangalia tu 
na kuondoka bila ya kufanya Marekebisho yoyote.

Je
 kwa hali hii Tunangojea Maafa au Hasara Itokee Ndio tukimbilie? 
Tunaiomba Mamlaka Husika Iweze Kuchukua Hatua za Haraka kurekebisha hili
 kabla ya Maafa hayajaweza Kutokea.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni