SERIKALI KUTOA LESENI KWA HOSPITALI NA VITUO VYA AFYA

Serikali inatarajia kutoa leseni kwa hospitali na vituo vya afya vya Umma vitakavyokidhi vigezo vya ubora wa kutoa huduma za afya ili mwananchi wajue kituo atakachoenda kina ubora gani wa huduma hivyo nchini.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati akiongea na Viongozi na Watendaji wa afya wa Mkoa na Wilaya zake kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara wakati wa zoezi la kutoa ngao kwa wilaya iliyofanya vizuri na vituo vya afya vilivyofanya vizuri wakati wa zoezi la tathimini ya kutoa nyota kwa vituo vya kutolea huduma za afya.
Dkt. Ndugulile alisema hivi sasa serikali inasisitiza kuweka ubora wa huduma za afya  katika vituo vyote vya afya vya umma ili kukidhi ubora unaotakiwa wa kutoa huduma kwa wananchi,  ”tunakwenda mbali zaidi  usipokuwa na vigezo hospitali yako na kituo chako  hutopewa leseni”
Hata hivyo amewataka wale wote waliopewa maelekezo ya nini wafanye basi viongozi wawajibike kwa kurekebisha changamoto zilizopo na wasingoje idara ya uhakiki ubora  kutoka wizarani waje kukagua kwani Lengo liliowekwa na wizara ni kila kituo cha afya kupata nyota tatu  hadi kufikia mwezi juni mwakani.
“Nyinyi wengine wote hamkustahili kupata cheti hata kimoja hapa,Mkoa wa Mtwara asilimia 3 za vituo vyenu vina nyota mbili na asilimia  51 vina nyota moja na zaidi ya nusu mna nyota 1 na asilimia 46 mna nyota sifuri hali ya utoa huduma bado, nimetoka hapo zahanati ya Ziwani, kwakweli hapana, ubora wa kutoa huduma pale hapana wakati mpo mjini,” alisema Dkt. Ndugulile.
Kwa upande mwingine amewataka kamati za afya ngazi ya Mkoa na Wilaya kufanya kazi na kusimamia katika kuyafanyia kazi maelekezo yote waliyopatiwa kwani maboresho mengine hayahitaji fedha hivyo kamati hizo zitimize wajibu wao.
”Niwaombe mbadilike kwani mambo madogo madogo yatakuja kuwagharimu hivyo msimamie hali ya utoaji wa ubora na huduma za afya kwa mkoa wa mtwara ni mbaya, nikirudi wakati mwingine sitoongea kirafiki hivi,”alisisitiza.
Aidha, aliwataka watendaji hao kubadilika katika utendaji wao na hivyo kusimamia upatikanaji wa dawa katika vituo vyao vya afya ili kusiwepo na malalamiko kutoka kwa wananchi kwamba wamekosa dawa.
“Dhama imebadilika, hivyo kila mmoja awajibike, awamu hii ni nyingine, hatutaki kusikia dawa hakuna na mwananchi analalamika amekosa dawa kwenye kituo cha afya, Mhe. Rais anaipenda sekta ya afya na ameongeza bajeti ya dawa na anatoa pesa zote, sitaki kusikia dawa hakuna na wilaya itakayoshindwa basi viongozi wake nao hawatoshi,” aliongeza Naibu Waziri wa Afya.
Naye Mkurugenzi wa Idara ya Uhakiki Ubora toka Wizara ya afya Dkt. Mohamed Mohamed alisema wizara ilingia kwenye mpango wa kuboresha huduma kwenye vituo vinavyotoa huduma za afya ya Msingi mwaka 2014 kwa kuhusisha kufanya tathimini vituo vyote vya afya nchini na kuvipa kategoria ya nyota  moja hadi tano ikiwemo wa kuandaa mipango ya kuimarisha ubora katika vituo hivyo.
Alitaja maeneo yaliyoangaliwa na kufanyiwa tathimini ni uendeshaji wa vituo, utendaji wa wafanyakazi,u wajibikaji, miundombinu ya kituo, mkataba kwa mteja pamoja na mazingira salama ya kutolea huduma na ubora wa huduma wenyewe.
Jumla ya vituo 6997 vilifanyiwa tathimini nchini na katika Mkoa wa Mtwara tathimini ya awali ilifanyika mwezi mei 2016 na vituo 221 vilifanyiwa tathimini na matokeo ya awali yalikua vituo 6 vilipata nyota 2(3%),vituo 112 vilipata nyota 1(51%) na vituo 103 vilipata nyota 0 (47%).
Katika zoezi hilo Halmashauri ya Wilaya ya  Nanyumbu iliibuka mshindi kwa kupata ngao na kituo cha afya Nanyumbu kilipata cheti. Kituo kingine cha afya kilichopaya cheti ni kituo cha Nagaga cha Masasi pamoja na za zahanati ya Nanjota na Nambaya zote za Halmashauri ya Masasi zilifanya vizuri. Pia zahanati ya Shangani ya halmashauri ya Manispaa ya Mtwara ilipata cheti.
Na WAMJW, Mtwara

Mazungumzo mapya kuhusu mgogoro wa Burundi kuanza Jumatatu hii Arusha

media
Polisi ikipiga doria katika mitaa ya Ngagara, kaskazini mwa Bujumbura, Aprili 25, 2015.
Mazungumzo mapya kuhusu mgogoro wa kisiasa wa Burundi yanaanza tena Novemba 27 hadi Desemba 8, kwa mujibu wa timu ya Mwezeshaji katika mgogoro huo, rais wa zamani wa Tanzania, Benjamin Mkapa.
Mazungumzo hayo mapya yatakayo dumu wiki mbili yatakua ni yenye maamuzi, kwa mujibu wa chanzo kilio karibu na timu ya Mwezeshaji.
Mazungumo haya yatadumu siku 13 ili kujaribu kutafuta suluhu ya mgogoro huo uliibuka baada ya rais Pierre Nkurunziza kutangaza nia yake ya kuwania muhula wa tatu wa urais mwaka 2015.
Hii itakua mara ya kwanza serikali ya Burundi kushiri mazungumzo nje ya nchi. Serikali imemtuma Katibu wa kudumu kwenye wizara ya Mambo ya Ndani, Therence Ntahiraja kushiriki mazungumzo hayo. Pia kiongozi wa chama tawala Evariste Ndayishimiye, akiambatana na viongozi wa vyama vya upinzani vinavyounga mkono serikali na mashirika ya kiraia kutoka Bujumbura watakuepo mjini Arusha ili kujaribu kushawishi Mwezeshaji katika mgogoro wa Burundi Benjamin Mkapa na wasaidizi wake kuhamisha mazungumzo hayo nchini Burundi.
Katika mazungumzo yaliyotangulia, serikali ya Burundi ilikataa kushiriki mazungumzo ya moja kwa moja na upinzani wenye msimamo mkali, ulio uhamishoni (Cnared), ikiushtumu kuhusika katika jaribio la mapinduzi lililotibuliwa Mei 14, 2015. Hata hivyo Mwezeshaji rais mstaafu wa Tanzania, Benjamin Mkapa, alikua akijaribu kukutana na kila upande katika mgogoro huo.
Kwa mujibu wa chanzo kilio karibu na timu ya Mwezeshaji, mazungumzo haya huenda yakawa ya mwisho kuhusu mchakato wa amani nchini Burundi
Wiki mbili zilizipita msemaji wake Pancrace Cimpaye, alitangaza kwamba muungano wao hautashiriki mazungumzo hayo, ukishtumu Mwezeshaji katika mazungumzo hayo Benjamin Mkapa kuegemea upande wa serikali na kutaka baada ya mazungumzo hayo mazungumzo mengine kuendelea nchini Burundi.
Cnared itakua na mkutano kabambe hii leo mjini Brussels, nchini Ubelgiji kuwachagua viongozi wake wapya, kwa mujibu wa chanzo rasmi kutoka muungano huo.
Awali mabalozi kutoka nchi mbalimbali za Ulaya na Marekani katika kanda ya Afrika Mashariki wana wasiwasi na uamuzi huo wa timu ya usuluhishi wa kikanda, ambayo imetenga Umoja wa Mataifa, Umoja wa Afrika, na Umoja wa Ulaya katika maandalizi ya mazungumzo hayo ambayo yanaegemea upande wa rais Nkurunziza, kwa mujibu wa baadhi ya mabalozi.
Machafuko nchini Burundi yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 2000 kwa mujibu wa mashirika mablimbali ya haki za binadamu kutoka Burundi n ayale ya kimataifa, na wengine zaidi ya laki tatu kuyahama makazi yao na kukimbilia uhamishoni.

KONDOA CHEMBA KISIWA CHA WATENDAJI WA MAZOEA MAJIBU YAO NTAFUATILIA HADI MIAKA NENDA RUDI

Ahmad Mahmoud
Mwaka huu Namshukuru mungu kunijaalia kuweza kutembelea maeneo ya vijijini ikiwa ni katika kutekeleza majukumu yangu ya utafiti wa habari kwa jamii zilizopo pembezoni na kuchaguwa wilaya za Chemba,Kondoa Mji na Vijijini.

Suala la kutembelea maeneo hayo ni kufanya utafiti wa kihabari ambao utasaidia kuibua kero mbali mbali wanazokutana nazo wananchi na kujua miradi ya maendeleo ambayo serikali imetekeleza sahemu hizo,za pembezoni mwa jamii hususani vijijini.

Kumekuwa na Changamoto kubwa ndani ya wilaya hizo kiasi kunatakiwa juhudi za mara kwa mara kwa waandishi kufika huko, ambapo waandishi wengi ni nadra sana kufika maeneo ya vijijini sio Kondoa pekee na maeneo mengine hapa nchini kusaidia kuibua matatizo na juhudi za serikali kuatatua kero zao,

Hapa nawashukuru sana Muungano wa klabu za Waandishi wa Habari hapa nchini(UTPC)  kwa kuja na mpango wa mafuzo ya wandishi wa habari za vijijini hii naona ni wakati muafaka na msingi wa kuweza kuwasidia wananchi kuziunganisha na mamlaka zao kuweza kuibua kero zao, japo mimi sio mmojawapo niliepata mafunzo hayo ila natekeleza wajibu.

Mwezi wa 3 mwaka huu tarehe 8 nikiwa mkoani Arusha ambapo ni kituo changu cha kazi Napata simu ikiniomba kwenda kondoa kwenye tukio la Kampuni ya madini ya Kondoa Minning na Kikundi cha wachimbaji wadogo wa madini ya Dhahabu(KUMUCHA) kwenye Kijiji cha Changaa.

Nilifika kondoa majiba ya saa 7 mchana kwa basi la kampuni ya Champion na kupokelewa na wenyeji wangu viongozi wa kikundi cha kumucha na mara moja kuelekea maeneo ya Mtaa wa Tumbelo ambapo yapo machimbo wanaogombea na kampuni ya Kondoa Minning T Ltd kwa mda mrefu sasa bila kupatiwa ufumbuzi wa suala hilo ambapo mamlaka hadi sasa zipo kimya kutoa tafsiri ya nani hasa mmiliki wa eneo hilo la migodi iliyopo Changaa.

Leo Sintazungumzia mgogoro huo ambao kwa sasa upo katika hatua za kutolewa majibu ya kina na mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kondoa Ndugu yangu Fallesy Kibasa kwanza nampa Hongera kwa utekelezaji wa majukumu pili namwambia sheria ifuate mkondo wake katika kuhakikisha wananchi wanyonge wanapata haki yao bila kujali maslahi mapana ya wenye nacho.

 Bila kusahau Ofisi ya madini kanda ya kati na Afisa Madini Makazi Dodoma nao pia wapo katika mikakati hiyo ya kutatua mgogoro huo, Japo wao ndio chanzo cha mgogoro huo kwa kushindwa kutafsiri sheria ya madini ya mwaka2010 kwa vitendo na kuichukulia maamuzi kwa wakati ambayo ingeondoa sintofahamu iliyopo katika ya wachimbaji na kampuni ya Kondoa Minning.

Suala nalotaka kulizungumzia leo ni suala la kampuni za simu za mikononi ambazo zipo hapa nchini zikiwaunganisha wananchi katika suala zima la mawasiliano ili waweze kujiletea mendeleo yao kupitia mawasiliano ya kibiashara na hata sasa wakati serikali inatekeleza sera ya Uchumi wa kati wa Viwanda nayo ni kiungo muhimu wa kufikia malengo hayo.

Kumekuwepo na sintofahamu kubwa katika suala zima la fedha za huduma ambazo makampuni ya simu yanatakiwa kurudisha kwa wananchi na sheria zinazoyataka makampuni hayo kuingia mkataba na vijiji kwenye maeneo ya vijiji hususani hifadhi za milima.

Na maeneo mengi ya Vijijini viongozi wa serikali wanatakiwa kulifuatilia hilo kwenye maeneo mengi ya vijiji kubaini mihutasari mingi walioingia viongozi wa serikali za vijiji mingi haipo kwa maslahi ya wananchi wa kurudisha fedha za huduma na malipo ya maeneo.

Utakuta maeneo mengi yana migogoro ambayo kama viongozi au mwanasheria wa Halmashauri angeshiriki katika kuandaa mchakato mzima wa miongozo ya kisheria, basi kusingetokea matatizo kama hayo ambayo kuna vijiji Takribani 10 ndani ya wilaya ya Kondoa ambavyo havinufaiki na fedha za huduma wala maeneo yao waliowekewa minara ya simu za mkononi na makampuni hayo.

Sehemu nyingine utakuta hawajalipwa Takribani miaka mitano sasa na haijulikani Fedha zinaingia kwa nani na vijiji vimeibua miradi ya maendeleo ambapo kama fedha hizo zingeingia kwenye vijiji hivyo ingasaidia kukuza miradi hiyo na kujikuta vijiji vinapata maendeleo Tarajiwa ikiwemo miradi ya Afya,elimu na maji.

Hapa ntaizungumzia moja ya Kata na Kijiji ambacho kitakuwa mfano wa vijiji hivyo 10 Thawi ni mojawapo ya vijiji hivyo na inakabiliwa na changamoto kubwa ya huduma muhimu ya kijamii Maj,i hawa wanatumia maji ya Mto Bubu, maarufu ndani ya wilaya hiyo, lakini changamoto kubwa wapo hatarini kukumbwa na magonjwa ya mlipuko wanatumia maji hayo kuongea kufulia na mifugo humo humo kwa wakati mmoja hii inaonyesha ni kwakiasi gani fedha hizo zingeweza kuwasaidia kuondokana na adha hizo japo kidogo ingeondoa

 Aidha kama sio Afisa wa Kampuni hiyo na viongozi wachache kuingia makubaliano ya kinyemela kwa afisa wa Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo kufika na kuuhadaa uongozi na wananchi kuwa kampuni hiyo inanunua maeneo ya kuweka minara kinyume na sera ya kampuni hiyo kukodisha kwa wananchi aua kijiji husika, hilo ni  ukiukaji wa mkataba na kuuziwa eneo la mlima  AMASASOO uliopo kijiji cha Thawi kata ya Thawi wilayani Kondoa ,

Hii inaonyesha ni kwa kiasi gani sheria bado nataratibu hazikutumika, na hata viongozi walipohoji waliwaambia ntapeleka eneo lengine hivyo msukumo wa wananchi waliokuwa wanahitaji huduma hiyo ndio uliopelekea maamuzi ya kuumuuzia aliedai ni Afisa kutoka kampuni ya Tigo kwa  makubaliano ya shilingi za kitanzania 500,000 kwa eneo la hifadhi ya mlima huo wa Amasasoo, hapa utaona jinsi misitu inavyouzwa kinyume na sheria.

Narudia ndugu yangu suala hilo lilifuatiliwa na mbunge wa jimbo la Kondoa kaskazini dkta. Ashatu Kijaji ambaye pia ni Naibu waziri wa fedha na Mipango lakini hadi naandika makala haya wananchi hao bado mnara unasumbua huduma walizotarajia hawapati kwa uhakika jambo linalotia simanzi kama kampuni hizo zipo kwa ajili ya kutoa huduma au zipo zipo tu.

Sijaongelea Fedha za Huduma ambazo ni haki yao kisheria kurudishwa kwa ajili ya maendeleo utaona ni kwa jinsi gani utaratibu huo unavyotumika kurisha maendeleo nyuma ndani ya kijiji na hapa utaona na kujua naongelea nini katika suala zima la makubaliano ya makampuni ya simu za mikononi

kwani nina uzoefu wa masuala haya ndani ya ulipaji mfano upo wazi kule Salanka nilifuatilia Fedha walizokuwa wakiidai Kampuni ya Vodacom na Airtel zilikwama kwa mda hadi walipolipwa Stahiki yao baada ya kulifuatilia tena kwa Gharama Hadi Dar es Salaam nikiwa na mwenyekiti wa kijiji hicho wakati huo.

Hata hivyo ilibidi nifike kwa mwanasheria na mkurugenzi wa Halmashauri hiyo ya Kondoa Vijijini kupata ufafanuzi kuhusiana na mbunge wa jimbo hilo alifikia wapi baada ya kumuachia suala hilo mwanasheria wa halmashauri kulifuatilia juhudi ambazo hadi sasa hazijapatiwa ufumbuzi wowote hadi naandika makala hii

 Japo hapo awali Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa Vijijini Fallessy Kibassa tulitofautiana kimtazamo baada ya mimi kuandika story kuhusiana na suala hilo na mkurugenzi huyo kuniita muungo mbele ya Katibu mkuu wa Tamisemi Mussa Iyombe juu ya suala hilo wakati nikizungumza nae akiwa morogoro kwa njia ya simu tena simu ya Bosi ofisini kwa katibu mkuu Dodoma

Ilibidi nifike kwa mwanasheria wa Halmashauri ya Kondoa Vijijini Kuulizia suala hilo na kunieleza kuwa suala hilo wameliachia vijiji kuandaa muhtasari upya na makubaliano mapya ilikuweza kuliendea jambo hilo na majibu yatakuwa hivi karibu kwani juhudi zinaendelea kuhakikisha mbunge anapatiwa majibu ya suala hilo na wananchi wanapata fedha za huduma.

“Ndugu mwandishi hapa kuna mkanganyiko wa kisheria ila vijiji vina mamlaka yake kisheria kuamua matumizi ya ardhi hivyo suala hili wao watakuwa na maamuzi ya kutuletea sisi tuweze kufuatilia” aliongeza mwasheria huyo.

Utaona ni jinsi gani huduma za simu za mikononi zilivyokuwa changamoto vijijini hususani ambapo bado wengi wao taratibu kanuni na sheria kwao vimekuwa ni kama jua na kiza hivyo kukuta sheria zinawapitia kando hata wakuongoza nao wanatoa majibu ya kufikirika zaidi kuliko kisheria.

Kwa upande mwingine nataongelea suala la Tigo pesa huku vijijini ni mwiba mchungu kuna watu wamelizwa fedha zao na wahudumu wa kampuni ya tigo hapa namzungumzia Bi Ziada Abdi Ally mwenye no 0711480481 aliehamishiwa Fedha kiasi cha 970 000 tokea mwezi wa nane na mfanyakazi wa idara ya mauzo ya kampuni ya Tig joseph maginga kwenye namba zake Tofauti 0716123207 na 0710040034.

ambapo Kampuni hiyo  imekuwa ikimzungusha bila majibu wala kumlipa fedha zake za huduma imekuwa deni, wanamwambia aende polisi nako wanamzungusha hadi leo upelelezi haujakamilika na mtuhumiwa anadunda mitaani hapa utaona nayo yazungumza ujue ni kiasi gani wananchi vijijini wanavyoumia.

Hiyo ni tigo kama zitafuatiliwa na kampuni nyingine utaona mlolongo wa matukio hayo yalivyo mengi waswahili wanasema ‘panapofoka moshi ujue moto upo karibu” huo ni msemo wa Kiswahili na una maana kwa serikali yetu kutupia macho sio kondoa tu kwa Tanzania nzima kwa kila aliye na dhamana kuhakikisha anawajibika sio mpaka viongozi wa kitaifa kufika maeneo yao.
Unaweza kusema Kondoa na Chemba zipo Kisiwani kwani kumekuwepo na matukio mengi tena ya ubadhirifu wa miradi ya mendeleo na serikali imekuwa kimya licha ya kutakiwa kutolea maelezo kuanzia ngazi ya wilaya hadi mkoa huu ucheleweshaji wa majibu na kutofika kwa wakati ndio matatizo yanakuwa makubwa na malengo ya mendeleo yanakuwa hayajafikiwa.

Kama masuala ya kisheria yangefuatwa na miongozo kwa viongozi wa serikali za vijiji ingekuwepo hapa suala zima la migogoro mingi ya Ardhi na masuala ya mbalimbali yahusuyo maendeleo na migogoro isingekuwepo na ingekuwa historia naomba viongozi taasisi za kisheria na serikali kutembelea ndani ya wilaya hizo kuwasaidia wananchi katika masuala ya kisheria na kutoa elimu ya mausala hayo na mengine mbalimbali lengo likiwa ni kuondoa dhana ya migogoro iliyopo ambayo inafukuta chini kwa chini na serikali ndani ya wilaya ikidai imetatua migogoro 8 kati ya kumi na tatu

 Endelea kunifuatilia katika makala inayofuatia kuhusu ziara yangu kwenye wilaya hizo.

Ahmad Mahmoud ni mwandishi wa habari Anapatika kwa No.0745159196
Email.ahmad2mahmoud@gmail.com

Mwisho………………….

WAZIRI MKUU AUNGANA NA WANASONGEA KUOMBOLEZA KIFO CHA GAMA


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akisaini kitabu cha maombolezo,Nyumbani kwa aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Songea .Leonidas Gama. Waziri Mkuu aliungana na wanafamilia pamoja na wananchi wa Songea katika kijiji cha Lukuyi Wilayani Songea leo Novemba 25/2017 katika kuomboleza msiba
Waziri Mkuu Kassim. Majaliwa leo Noemba 25/2017 ameungana na wanafamilia, wananchi wa Songea katika kuomboleza kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo la Songea, Bw. Leonidas Gama, nyumbani kwa marehemu Likuyu wilayani Songea.

WAZIRI MHAGAMA AITAKA HALMASAURI YA BAHI KUKAMILISHA UJENZI WA SOKO LA KIGWE

Na. MWANDISHI WETU – DODOMA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Bahi kuhakikisha inamaliza ujenzi wa soko la Kigwe kwa kuhakikisha wanajenga vyoo na vibanda vidogo vitakavyo saidia soko hilo lililojengwa na Programu ya Miundo Mbinu ya Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF).

Ameyasema hayo alipofanya ziara yake Wilayani Bahi Novemba 21, 2017 kwa lengo la kujionea namna uboreshaji wa soko hilo ambalo tayari limekamilika kwa asilimia 90 na kukabiliwa na changamoto za vibanda na vyoo vya kudumu.

“Ninaiagiza Halmashauri hii kuhakikisha inaleta timu ya wataalamu kupima viwanja na kuvigawa kwa wananchi pamoja na kumalizia ujenzi wa Vyoo vya soko ili lianzae utekelezaji wake haraka na kuhakikisha umeme unafungwa ndani ya soko hili”.

Kwa upande wake Mbunge wa Bahi Mhe. Omary Badwel alieleza ujenzi wa soko ni jambo ja muhimu linalogusa wanakigwe wote kwani tangu enzi za mkoloni kumekuwa na changamoto ya soko na kuwataka wananchi kulitunza na kuhakikisha linakuwa msaada kwao wote.

“Soko hili toka utawala wa mkoloni kulikuwa na soko bovu hivyo hatua ya kulikamilisha litavutia wengi na kukuza uchumi wa wana Kigwe wote.”Alisisistiza Badwel

Kwa upande wake mkazi wa Kigwe Bi.Anastazia Mkatato alieleza kuwa kujengwa kwa soko hilo litatatua changamoto iliyopo ya kukosa soko la kudumu kwani yaliyopo ni madogo yanayomilikiwa na watu binafsi.

“Ninaishukuru Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Programu ya Miundo Mbinu ya Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini iliyoamua kutujengea soko hapa Kigwe na hii itatupa nafasi ya kuuza mazao na bidhaa kwa wingi kupelekea kukuza uchumi wetu.”Alieleza Anastazia.

Naye Mratibu wa Mradi Taifa Bw.Walter Swai alieleza kuwa soko hili ni muhimu kwa wana Kigwe na maeneo jirani , hivyo tutaendelea kuunga mkono jitihada za kuhakikisha vifaa vinawekwa ikiwemo Meza za kuuzia mbidhaa sokoni.

“Tayari Ofisi yangu itachukua changamoto hii ya kukosekana kwa meza za kuuzia na kuitatua ndani ya mwezi mmoja hivyo niwaahidi kutekeleza haya.”Alisisitiza Bw.Swai

Ujenzi wa soko la Kigwe umegharimu jumla ya zaidi ya shilingi milioni 68 ambapo Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Programu ya Miundo Mbinu ya Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF) ilitoa kiasi cha zaidi ya shilingi Milioni 50 pamoja na Mfuko wa jimbo kuchangia jumla ya shilingi Milioni 15. Dhumuni la mradi ni kuwa na eneo rasmi la kufanyia biashara na kuwezesha wajasiliamali wa Kigwe na kujikwamua kiuchumi na kukuza maendeleao yao.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akisisitiza jambo kwa wananchi wa Kigwe alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa soko la Kidwe Wilayani Bahi Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana na Mbunge wa Bahi Mhe. Omary Badwel alipowalisi kukagua ujenzi wa Soko la mazao la Kigwe Lililopo Bahi Dodoma.
Afisa Mtendaji Kata Bw. John Mchiwa akikabidhi taarifa ya Ujenzi wa Soko Kigwe kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama alipofanya ziara Bahi kuona maendeleo ya ujenzi huo.
Mbunge wa Bahi Mhe. Omary Badwel akitoa maelezo kuhusu ujenzi wa soko la Kigwe lililofadhiliwa na Programu ya Miundo Mbinu ya Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF) kwa kushirikiana na Halmashauri wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe. Jenista Mhagama Wilayani Bahi Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Wilaya ya Bahi Bi. Rachel Chuwa wakati wa ziara yake Kigwe.
Mratibu Taifa wa Programu ya Miundo Mbinu ya Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF) Bw. Walter Swai akisalimiana na baadhi ya wakazi wa Kigwe walipotembelea Kijiji hicho kuona ujenzi wa soko la Kigwe unavyoendelea.(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU – DODOMA)

VIJANA WASOMI WATAKIWA KUMSAIDIA RAIS MAGUFULI KULILETEA TAIFA MAENDELEO

le

ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Abundant Bressing Centre (ABC), Flaston Ndabila amewataka Vijana wasomi na wanataalumu nchini kumsaidia Rais Dk.John Magufuli kuliletea Taifa maendeleo.

Ndabila ametoa mwito huo jijini Dar es Salaam jana wakati akiwahutubia wasomi wanataaluma katika kongamano la siku moja la vijana wasomi kutoka makanisa mbalimbali ya kikristo lilifanyika Hoteli ya Landmark lenye lengo kwa wasomi hao kutumia taaluma walizonazo katika kuitumikia jamii na taifa kwa ujumla.

"Ninyi wasomi mmesomeshwa kwa ajili ya kuwatumia wananchi na taifa msaidieni Rais wetu John Magufuli kuliletea taifa la Tanzania na kanisa maendeleo kwani hakuna mtu mwingine tunaye mtegemea zaidi yenu" alisema Askofu Ndabila.

Askofu Ndabila aliwataka wasomi hao waende kwa wananchi wakawanoe na kuweza kuwiva kisawasawa ili waendenane na kasi ya maendeleo anayoihitaji Rais Magufuli.

Alisema wasomi ndio kundi pekee linaloweza kuitoa nchi katika hatua moja na kuipeleka katika hatua nyingine ya mbali kimaendeleo na kuwa mambo yao makubwa watakayo yafanya yataweza kuwabadilisha wananchi na nchi ikasonga mbele.

"Wananchi hawahitaji kusikia umahiri wenu wa kuongea kiingereza bali wanataka kuona ni jinsi gani mtafanya kwa vitendo kuwasaidia ili kulipeleka taifa mbele kimaenndeleo" alisema Ndabila.

Askofu Ndabila aliongeza kuwa hivi karibuni hapa nchini ilifika meli kubwa ya kitabibu ambayo ilikuwa na madakatari ambapo walikuwa wakitoa matibabu kwa wagonjwa kazi ambayo hata madaktari wasomi wa hapa nchini wakijipanga wanaweza kuifanya kwa kushirikiana na wadau wengine.

Mtoa mada katika kongamano hilo, Amina Sanga mhitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) alisema vijana wanapaswa kuwa wabunifu badala ya kusubiri kuajiriwa.Aliwataka vijana kuacha kutumia mitandao ya kijamii kwa kujibizana mambo ambayo hayana tija kwa wao na taifa kwa ujuma badala yake waitumie kutafuta fursa za maendeleo.

"Siku hizi vile vijiwe vya kupiga domo mitaani havipo tena vimehamia kwenye makundi ya mitandaoni huko utakuta vijana tena wasomi wakishindani kujibizana vitu ambavyo havina manufaa kwao na taifa" alisema Sanga.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Dk.Philip Sanga alisema mabadiliko ya maendeleo yanaanzia kwa mtu mmoja, jamii na hadi taifa na ili kupata mabadiliko hayo yanawategemea wasomi na si mtu mwingine.

Mratibu wa Kongamamo hilo, Ephrahim Mwambapa alisema kongamanao hilo linaundwa na muungano wa wasomi wa kristo uitwao Tanzania for Jesus Prayer Movement ambao mlezi wake ni Huduma ya I Go Africa for Jesus.

Mwambapa alisema lengo la kongamano hilo ni kuona jinsi gani wasomi na wanataaluma wataweza kutumia taaluma na usomi wao kusaidia jamii badala ya taaluma hiyo kuachwa bila ya kufanyiwa kazi wakati jamii inachangamoto nyingi.


Tunapokuwa vyuoni tunakuwa na mipango mingi ya maendeleo lakini baada ya kumaliza masomo kila mtu anakuwa kivyake wakati tunapaswa kushirikiana na jamii na ndio maana tumeona ni vizuri kuazisha muungano huu lengo likiwa kujumuika na jamii katika shughuli za maendeleo ya nchi na dini" alisema Mwambapa.

Alisema wazo la kuanzisha muungano huo nimatunda ya mkutano mkuu wa kitaifa wa kuliombea taifa ulioratibiwa na Askofu Flaston Ndabila na kuhudhuriwa na watu mbalimbali na vijana kutoka vyuo vikuu uliofanyika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam mapema mwaka huu.
Mhitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Amina Sanga akitoa mada kwenye kongamano la siku moja la vijana wasomi kutoka makanisa mbalimbali ya kikristo lilifanyika Hoteli ya Landmark jijini Dar es Salaam jana lenye lengo wasomi hao kutumia taaluma walizonazo katika kuitumikia jamii na taifa kwa ujumla.
                                              Vijana wasomi wakiwa kwenye kongamano hilo.
                                                                                      Kongamano likiendelea.
         Wanakwaya wa Haleluya Celebration wakiwa kwenye kongamano hilo.
                                            Muonekano wa ukumbi katika kongamano hilo.
Meza kuu katika kongamano hilo. Kutoka kulia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Philip Sanga, Mgeni rasmi wa Kongamano hilo, Askofu Mkuu wa Kanisa la Abundant Bressing Centre (ABC), Flaston Ndabila , Mchungaji John Kanafunzi na Mratibu wa kongamano hilo, Ephraim Mwambapa.

CHUO CHA USIMAMIZI WA WANYAMAPORI-MWEKA KUANZA KUTOA MAFUNZO MAALUM KWA WATOA HUDUMA ZA UTALII NCHINI KUANZIA KESHO NOVEMBA 26

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (wa tatu kulia) akipata maelezo kutoka kwa Mwanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori-Mweka, Brightone Mbilinyi kuhusu mafunzo ya silaha yanavyotolewa chuoni hapo katika mahafali ya 53 ya chuo hicho yaliyofanyika jana katika wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro. Zaidi ya asilimia 60 ya mafunzo chuoni hapo hutolewa kwa vitendo. Wengine Pichani ni Balozi wa Nigeria nchini, Mhe. Sahabi Dada (wa pili kushoto) na Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Jafari Kideghesho (wa nne kulia).

                                                                                  Na Hamza Temba-WMU

Katika kutimiza azma ya Serikali kuboresha huduma za ukarimu kwenye sekta ya utalii nchini, Wizara ya Maliasili na Utalii imekichagua Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori Mweka kilichopo mkoani Kilimanjaro kwa ajili kutoa mafunzo maalum kwa waongoza watalii nchini.

Mafunzo hayo ambayo yanatarajiwa kuanza kesho (Jumatatu) chuoni hapo yatakuwa kwenye mfumo wa kujiendeleza na yamelenga kuwawezesha watoa huduma katika sekta hiyo kupata sifa za kusajiliwa na kupewa leseni ya kuendelea kutoa huduma hiyo kwa mujibu ya sheria ya utalii Na. 11 ya mwaka 2008 kifungu cha 48.

Hayo yamesemwa jana na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga katika mahafali ya 53 ya kuwatunuku vyeti wahitimu 224 wa chuo hicho katika kozi mbalimbali ikiwemo Shahada, Stashahada na Astashada kwenye Usimamizi wa Wanyamapori na Utalii.

"Katika kutambua utaalamu na uzoefu wa chuo chenu, Wizara yangu imeichagua Mweka kutoa mafunzo yatakayowawezesha waongoza watalii nchini kupata sifa ya kusajiliwa (cheti) na kupewa leseni," alisema Naibu Waziri Hasunga.

"Nimefurahi kusikia kuwa mmeshajipanga tayari kuanza kutoa mafunzo hayo baada ya kufanya tathmini ya mahitaji ya mafunzo na kuainisha mapungufu kwenye taaluma, ujuzi na mitazamo pamoja na kuandaa mtaala wa mafunzo hayo.

"Nitoe wito kwa waongoza watalii nchini wajisaji ili wapate mafunzo haya muhimu kwakua katika miaka michache ijayo hawataruhusiwa kutoa huduma hiyo bila kutimiza masharti haya ya kisheria,” alisema Hasunga.

Alisema tafiti mbalimbali zinaonyesha kuwa watalii wengi wanaokuja nchini hupata taarifa kutoka kwa wenzao waliotembelea Tanzania ambao muda wao mwingi wanakuwa na waongoza watalii kwenye maeneo ya vivutio.

"Hivyo ni muhimu wapewe mafunzo maalum waweze kutoa huduma bora zaidi zitakazowafanya watalii wafurahie ukarimu wao waweze kuwa mabalozi wazuri wa kuutangaza utalii wetu watakaporudi nchini kwao" alisema Hasunga.

Alisema licha ya Sekta ya utalii nchini kuchangia asilimia 17 ya pato la taifa na asilimia 25 ya fedha za kigeni (watalii milioni 1.28 na bilioni 2 mwaka 2016), mchango wake unaweza kukua zaidi kupitia mikakati mbalimbali inayowekwa na wizara yake ikiwemo hiyo ya mafunzo ambayo imelenga kuongeza idadi ya watalii kufikia milioni mbili mwaka 2020 na watalii milioni 8 mwaka 2025 pamoja na mapato ya dola za kimarekani bilioni 20 mwaka 2025.

Akizungumzia kuhusu mafunzo ya jeshi usu chuoni hapo, Naibu Waziri Hasunga aliuagiza uongozi wa chuo hicho kuendesha mafunzo hayo muda wote wa masomo tofauti na ilivyo hivi sasa ambapo hutolewa kwa wiki mbili katika kila 'semister'.

"Mafunzo haya yasiishie tu kwa muda wa wiki mbili, ni matarajio yangu kuona yanaendeshwa katika kipindi chote cha mafunzo ikiwemo wanafunzi kuvaa sare za heshima za jeshi usu, kuwa na nidhamu ya kijeshi na muhimu zaidi kuonyesha utayari na uwezo wa kukabiliana na wahalifu ikiwemo majangili," alisema Hasunga.

Aidha, alizitaka taasisi zilizopo chini ya Wizara yake kuajiri wananfunzi wanaomaliza chuoni hapo ikiwa ni pamoja na kutumia fursa ya chuo hicho mahiri kuwaongezea ujuzi wafanyakazi waliopo makazini.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Jafari Kideghesho alimueleza Naibu Waziri Hasunga kuwa Chuo chake kimeshafanya maandalizi yote ya kuanza kutoa mafunzo kwa waongoza watalii nchini kama ilivyoagizwa na wizara yake ambapo tathmini ya mahitaji ya mafunzo hayo imeshafanywa kwa kuainishwa mapungu katika taaluma, ujuzi na mitazamo.

"Tumeshaandaa pia mitaala ya mafunzo ambayo imezingatia kuondoa mapungufu tuliyoyabaini, na tunatarajia kuanza mafunzo yetu ya kwanza kwa wapagazi 100 kwa muda wiki tatu kuanzia jumatatu ijayo (leo)," alisema Prof. Kideghesho.

Alisema ili kufanikisha mafunzo hayo chuo chake kimepokea msaada wa Shilingi milioni 110 kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wapagazi wanaotoa huduma katika mlima Kilimanjaro, fedha ambazo zitatumika kwa ajili ya mafunzo na tafiti mbalimbali.

Mahafali hayo ya 53 yalihudhuriwa pia na Balozi wa Nigeria nchini, Balozi Sahabi Dada, Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Chuo hicho, Prof. Faustin Bee, Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Kippi Warioba, Mkuu wa Wilaya ya Same, Harun Mbogo, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Nebo Mwina, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Prof. Dos Santos Silayo na baadhi ya wawakilishi wa Mamlaka ya Wanyamapori ya Uganda.

Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori, Mweka kilianzishwa mwaka 1963 baada ya azimio la Arusha mwaka 1961 ambalo lilitaka uwepo wa watu waliopewa mafunzo kwa ajili ya kulinda na kusimamia urithi wa rasilimali za Afrika.

Chuo hicho ambacho huendesha mafunzo yake kwa vitendo kwa zaidi ya asilimia 60 kimepata ongezeko la wanafunzi kutoka 25 mwaka 1963/1964 hadi zaidi ya wanafunzi 550 mwaka 2016/2017 kutoka nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Malawi na Cameroon.

Aidha, katika kipindi cha miaka 54 iliyopita chuo hicho kimeweza kufundisha zaidi ya mameneja wa wanyamapori 8,000 kutoka nchi zaidi ya 50 duniani.

Chuo hicho pia kimepewa tuzo na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki kama Kituo cha Ubora wa Taaluma ya Usimamizi wa Wanyamapori (Centre of Excellence).

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (wa pili kushoto) akipata maelezo kutoka kwa mmoja ya Mwanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori, Mweka, Leonard Mgamba kuhusu mafunzo ya taaluma ya wanyamapori yanavyofanywa kwa vitendo chuoni hapo. Wengine pichani ni Balozi wa Nigeria nchini, Sahabi Dada (wa tatu kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Harun Mbogo (kushoto) na Mtenaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu, Prof. Dos Santos Silayo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) akiwa ndani ya handaki linalotumika kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo katika Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori-Mweka muda mfupi kabla ya kuwatunuku vyeti wahitimu 224 wa kozi mbalimbali chuoni hapo.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) akikagua gwaride la wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori-Mweka muda mfupi kabla ya kuwatunuku vyeti wahitimu 224 wa kozi mbalimbali ikiwemo Shahada, Astashahada na Stashada katika taaluma za usimamizi wa wanyamapori na utalii katika mahafali ya 53 yaliyofanyika chuoni hapo jana katika Wilaya ya Moshi Mkoani Kilimanjaro. Zaidi ya asilimia 60 ya mafunzo chuoni hapo hutolewa kwa vitendo na wahitimu 224 wa kozi mbalimbali walitunukiwa vyeti.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Mamlaka ya Wanyamapori ya Uganda ambao walishiriki kwenye mahafali ya 53 ya Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori-Mweka jana.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori Mweka, Prof. Faustin Bee (kulia), Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Mhe. Kippi Warioba (katikati) na Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Harun Mbogo (kushoto) wakiteta jambo wakati wa mahafali ya 53 ya chuo hichao ambayo yalifanyika jana mkoani Kilimanjaro.
Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori Mweka, Prof. Jafari Kideghesho (kulia) akiwasilisha taarifa fupi kuhusu chuo hicho kwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kushoto) wakati wa mahafali ya 53 ya chuo hicho ambayo yamefanyika jana mkoani Kiliamanjaro. Wengine ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Chuo hicho, Prof. Faustin Bee (wa pili kushoto) na Balozi wa Nigeria nchini, Mhe. Sahabi Dada.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kushoto) akizungumza na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori-Mweka, Prof. Faustin Bee (kulia), Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Mhe. Kippi Warioba (wa pili kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Harun Mgogo wakati wa mahafali ya 53 ya chuo hicho ambayo yamefanyika jana mkoani Kilimanjaro. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) na Balozi wa Nigeria nchini, Mhe. Sahabi Dada.
Mkuu wa Chuo chaUsimamizi wa Wanyamapori Mweka, Prof. Jafari Kideghesho (kulia) akiteta jambo na Balozi wa Nigeria nchini, Mhe. Sahabi Dada.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Mwanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori, Mweka, Ebenezer Mollel kuhusu mafunzo ya taaluma ya wanyamapori yanavyofanywa kwa vitendo chuoni hapo. Wengine pichani ni Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Jafari Kideghesho (wa pili kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Mhe. Kippi Warioba.
Sehemu ya taswira ya Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori Mweka.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga akipanda mti wa kumbukumbu chuoni hao.
Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha Usimamizi ya Wanyamapori Mweka, pembeni yao ni mifupa ya miguu ya tembo katika chumba maalum cha mafunzo ya wanyamapori.
Sehemu ya wananfunzi 224 waliopewa vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali katika Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori-Mweka wakiwasili katika viwanja kwa ajili ya mahafali ya 53 yachuo hicho yaliyofanyika jana katika viwanja vya chuo hicho wilayani Moshi Mkoa wa Kiliamanjaro. Vyeti hivyo vilitpolewa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga. 
Gwaride la wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori Mweka wakitoa heshma mbele ya mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (hayuko pichani)

Naibu Waziri wa Maliasi na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (wa pili kulia) akimtunuku cheti Mhitimu wa Shahada ya Usimamizi wa Wanyamapori, katika Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori-Mweka, Valentina Fiasco ambaye ni raia wa Italia katika mahafali ya 53 yaliyofanyika jana chuoni hapo katika wilaya ya Moshi mkoani Kiliamanjaro. Kulia ni Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Jafari Kideghesho. Jumla ya wahitimu 224 wa kozi mbalimbali walitunukiwa vyeti.
Naibu Waziri wa Maliasi na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (wa pili kulia) akimtunuku cheti mmoja ya wahitimu wa Shahada ya Usimamizi wa Wanyamapori, katika Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori-Mweka wakati wa mahafali ya 53 yaliyofanyika jana chuoni hapo katika Wilaya ya Moshi Mkoani Kiliamanjaro. Kulia ni Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Jafari Kideghesho. Jumla ya wahitimu 224 wa kozi mbalimbali walitunukiwa vyeti. 
Naibu Waziri wa Maliasi na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (wa pili kulia) akitoa tamko la kuwatunuku kozi mbalimbali wananfunzi 224 wa chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori Mweka katika mahafali ya 53 ya chuo hicho ambacho yamefanyika jana mkoani Kilimanjaro. Kulia ni Mkuu wa chuo hicho, Prof. Jafari Kideghesho, Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho, Prof. Faustin Bee (wa tatu kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Mhe. Kippi Warioba.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Prof. Dos Santos Silayo (mwenye tai) na washiriki wengine katika mahafali hayo.

WAZIRI MKUU AKABIDHI KOMBE KWA TIMU YA AFISI KUU ZANZIBAR


Waziri Mkuu .Kassim Majaliwa mwenye nguo nyeupe akiwa katika picha ya pamoja na timu ya Afisi Kuu Zanzibar. PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akikabidhi kombe kwa nahodha wa timu ya Afisi Kuu Zanzibar.Bwana Vuai Jecha baada ya timu yake kuibuka mshindi kwakuifunga timu ya Kwahani mabao 3 kwa 1. katika mchezo wa fainali uliochezwa Uwanja wa Aman Zanzibar. Novemba 25/2017. PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU

BancABC yashirikiana na Kitengo cha Dharura Cha Muhimbili kutoa bima ya afya kwa watoto




Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wazee Ummy Mwalimu akikabidhi moja ya kadi za bima kwa watoto zaidi ya 100 wanaoishi kwenye mazingira magumu jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki ikiwa na ushirikiano baina ya Kitengo cha magonjwa ya dharura cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na BancABC Tanzania.

Baadhi wa watoto wanufaika na kadi za bima wakiwa na walezi wao wakisikiliza hotuba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wazee Ummy Mwalimu


Baadhi ya wafanyakazi wa Kitengo cha magonjwa ya dharura kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakifuatilia kwa umakini hotuba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wazee Ummy Mwalimu wakati wa hafla ya kukabidhi kadi za bima kwa watoto zaidi100 ya ambao ni mayatima
Baadhi ya wafanyakazi BancABC Tanzania wakifuatilia kwa umakini hotuba  ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wazee Ummy Mwalimu wakati wa hafla ya kukabidhi kadi za bima kwa watoto zaidi100 ya ambao ni mayatima.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wazee Ummy Mwalimu akiongea na Mkurugenzi wa Kitego cha wateja wakubwa na wadogo wa BancABC Joyce Malai wakati wa kukabidhi kadi za bima kwa watoto zaidi ya 100 jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki ikiwa na ushirikiano baina ya Kitengo cha magonjwa ya dharura cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na BancABC Tanzania.

Picha ya Pamoja
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wazee Ummy Mwalimu aikisisita jambo kwa Mkurugenzi wa Kitego cha wateja wakubwa na wadogo wa BancABC Joyce Malai wakati wa kukabidhi kadi za bima kwa watoto zaidi ya 100 jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki ikiwa na ushirikiano baina ya Kitengo cha magonjwa ya dharura cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na BancABC Tanzania. 

BancABC, ambayo ni sehemu ya Atlas Mara, imeshirikiana na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili kutoa huduma ya bima ya afya itakayofaidisha watoto 100 ambao ni yatima na wanaoishi katika mazingira magumu kupitia mradi mpya wa afya wa Muhimbili uliozinduliwa leo.

Akizindua mpango huo wa Afya wa Muhimbili Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, aliishukuru BancABC kwa kushirikiana na Hospitali ya Muhimbili katika suala hilo la kutoa huduma ya bima ya afya kwa watoto.

Alisema mradi huo wa Muhimbili kushirikiana na BancABC unaendea sambamba kabisa na malengo ya serikali iliyojiwekea katika kuhakikisha kuwa jamii inapata huduma ya Afya kwa uhakika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwani watoto ndio moja ya makundi ambayo huathirika sana wasipopatiwa huduma za Afya za uhakika.

“Natoa wito kwa wazazi watumie fursa hii iliyotolewa na BancABC kwa ushirikiano na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa kuwafungulia watoto wao akaunti BancABC ili kuhakikisha watoto wao wanapata huduma kwa uhakika muda wowote bila ya ulazima wa kuwa na fedha tasilimu pale mtoto anapougua,” alisema.

Alitoa wito pia kwa watoa huduma za kifedha nchini pamoja na mashirika mengine kuhakikisha yanaiga mfano huo wa BancABC kwani wizara yake iko tayarikushirikiana na taasisi ambazo ziko tayari kuimaisha huduma katika sekta ya afya hasa upande wa utoaji huduma.

Naye Mkuu wa Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo wadogo na wafanyabiashara wa kati, Bi Joyce Malai alisema BancABC inatambua umuhimu wa kuwa kampuni inayowajibika katika masuala ya kijamii kwa kurudisha kwa jamii sehemu ya faida na hasa katika sekta muhimu sana ya afya, dhamira hii ya BancABC kusaidia kwenye kuwezesha Afya ya watoto ni yamsingi sana kwa kuwa pia inasaidia serikali kufikia malengo yake.

Alisema baada ya kufungua akaunti hizo, wazazi wa watoto wenye akaunti hizo watakuwa wanahimizwa wakewe hela mara kwa mara kwa ajili ya bima ya watoto wao ili wapate huduma kupitia akaunti hizo za Mwangaza Junio Kids Accountambayo haina tozo ya kila mwezi.

Bi Joyce Malai aliongeza kuwa huduma hiyo ya bima haitakuwa na masharti kuhusu umri. “Wazazi wanaweza kufungua akaunti kwa mtoto zaidi ya moja na kuweka fedha kiasi chochote wanachotaka kwani itasaidia kuhakikisha watoto wao wana bima,”. 

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa, Prof. Lawrence Museru, aliishukuru BancABC kwa ushirikiano huo na kusema hatua hii haitasaidia watoto kupata tu huduma za afya kwa kupitia bima, bali itawajengea pia utamaduni wa kuweka akiba katika benki kuanzia utotoni hadi wanapokuwa watu wazima ili wapange mambo yao vizuri .

“Kwa sasa akaunti hizi zitafunguliwa na wazazi wao ila watakuwa wakitambua umuhimu wa huduma hii na wataendelea nayo hadi ukubwani,"alisema na kutoa rai kwa wazazi watumie fursa hiyo vizuri.