Balozi
 wa Norway nchini Tanzania kupitia kwa Balozi wake Balozi Bi. 
Hanne-Marie Kaarstad leo wameweza kutiliana saini mkataba wa udhamini wa
 donge nono la kiasi cha Dola 128200(USD) ambazo ni sawa na shilingi za 
Kitanzania Milioni 300, ambazo zitaenda kusaidia Shirika lisilo la 
Kiserikali la Busara Promotion kwa ajili ya tamasha la Sauti za Busara 
2018. Halfa hiyo ya kutiliana saini imefanyika mapema leo Novemba 2,2017
 katika Ubalozi wa Taifa hilo la Norway, Jijini Dar es Salaam na 
kushuhudiwa na wadau mbalimbali vikiwemo vyombo vya habari. 
Awali
 Mkurugenzi wa Busara Promotion, Yusuf Mahmoud alishukuru Ubalozi wa 
Norway nchini Tanzania kwa kutoa udhamini huo ambao utasaidia uhai wa 
tamasha hilo ambalo limejizolea sifa kwa muda mrefu. “Sauti za Busara 
imepata msaada, shukrani kwa ubalozi wa Norway nchini Tanzania. Norway 
inaonyesha mfano mzuri wa kuigwa Duniani kwa kuchangia katika maendeleio
 ya kudumu na mazingira rafiki. Kama ilivyo katika malengo yake nchini 
Tanzania. 
Balozi
 wa Norway nchini Tanzania Bi. Hanne-Marie Kaarstad akizungumza katika 
tukio hilo mara baada ya kutiliana saini. Anayemfuatia ni Mkurugenzi wa 
Busara Promotion, Yusuf Mahmoud na kulia ni Ofisa wa Busara Promotions.
Ubalozi
 wa Norway tangu mwaka 2009 unatoa mchango mkubwa wa kifedha kwa shirika
 la Busara Promotions, ili kuliwezesha kutimiza mpango mkakati wake hii 
ni pamoja na kusaidia shughuli za kiutendaaji wa tamasha kwa kila mwaka 
na tunafurahia kwani tunaamini utaendelea pia kwa mwakani” alieleza 
Mkurugenzi huyo Yusuf Mahmoud. Pia akifafanua umuhimu wa tamasha la 
Sauti za Busara, Mkurugenzi huyo Yusuf Mahmoud alibainisha kuwa, tamasha
 hilo limekuwa likiunganisha watu wa rika na asili tofauti huku pia 
likiheshimu uhuru wa kujieleza sambamba na kuleta umoja, Amani na 
kuimalisha jamii. 
“Tamasha
 la Sauti za Busara linatoa fursa kwa wasanii na wadau wa sekta ya 
muziki kukutana na kujifunza. Linaimarisha utaalamu katika sekta ya 
Sanaa nchini hivyo yote haya lengo kuu la tamasha ili ni kuhakikisha 
kutangaza amani, mshikamano na kuheshimu tamaduni tofauti” alimalizia 
Yusuf Mahmoud. 
Kwa
 upand wake, Balozi wa Norway nchini Tanzania Bi. Hanne-Marie Kaarstad 
ameahidi kuendeleza ushirikiano na Busara Promotions katika kusaidia 
Sanaa na Utamaduni ambapo lengo kuu ni kukuza mashirikiano na 
maingiliano ya kitamaduni kupitia sanaa hasa muziki katika jamii kwa 
njia ya tamasha hilo la kila mwaka la Sauti za Busara. “Najisikia furaha
 sana katika siku ya leo katiliana saini udhamini huu mnono. 
Tumekuwa
 na Busara Promotion kwa muda mrefu kuanzia 2008 mpaka sasa tukiendelea 
kukuwa zaidi na kuleta mageuzi kwa jamii hasa kuleta mageuzi makunwa 
sana kwa jamii ya Wazanzibar, Tanzania Bara na Ukanda wa Afrika kwa 
ujumla. Tunaamini Sauti za Busara wamejijengea mizizi imara Visiwani 
Zanzibar na Tanzania Bara kwa ujumla kupitia tamasha lao ambalo linainua
 na kulinda utamaduni wa Mzanzibar huku pia likilinda hutu na utamaduni 
wake ndani ya visiwa hivyo vya Zanzibar.” Alieleza Balozi Bi. Anne-Marie
 Kaarstad. 
Mkurugenzi
 wa Busara Promotion, Yusuf Mahmoud na Balozi wa Norway nchini Tanzania 
Bi. Hanne-Marie Kaarstad wakitiliana saini udhamini huo mapema leo 
Novemba 2, 2017. Wengine wanaoshuhudia ni maafisa kutoka Ubalozi wa 
Norway na Busara Promotions.
Balozi
 huyo aliongeza kuwa, tamasha hilo pia limekuwa na nguvu kubwa ikiwemo 
kukusanya watu wengi zaidi kutoka pande mbalimbali za Dunia na kukutana 
mahala pamoja kufurahia. Aidha, Mkurugenzi wa Busara Promotions, Yusuf 
Mahmoud amebainisha kuwa, msimu wa Sauti za Busara kwa 2018, tayari 
wametangaza listi ya wasanii na vikundi ambapo jumla ya vikundi 20 
kutoka Tanzania Bara, pia vipo kutoka Afrika Kusini, Zimbabwe, DRC, 
Nigeria, Morocco, Algeria, Kenya, Rwanda, Burundi, Malawi, Misri Sudan, 
Gambia. 
Pia
 vipo vikundi kutoka nchi za Reunion, Norway, Denmark na Switzerland. 
Katika vikundi hivyo vinatarajia kuwa na Wasanii 400, ambapo wataonyesha
 uwezo wao kwenye majukwaa matatu tofauti, shoo 46 zote zikiwa asilimia 
100 ‘live’ kwa siku nne mfululizo. Pia kutakuwa na mambo mbalimbali 
ikiwemo warsha na semina kwa wanamuziki wa ndani na nje ambao watapata 
kubadirishana ujuzi na mbinu za kukuza sanaa na masoko ya muziki wao. 
Mkurugenzi wa Busara Promotion, Yusuf Mahmoud na Balozi wa Norway 
nchini Tanzania Bi. Hanne-Marie Kaarstad wakibadilishana hati 
walizotiliana saini udhamini huo mapema leo Novemba 2, 2017. (PICHA ZOTE
 NA ANDREW CHALE).
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni