UJUMBE WA WATAALAMU WA AFYA KUTOKA BRAZIL WAKUTANA NA WAZIRI WA AFYA ZANZIBAR.


6 (5)
BALOZI wa Heshima wa Brazil hapa Zanzibar, Abdulsamad  Abdulrahim (suti buluu) akiwa na Ujumbe wa wataalamu wa Afya kutoka Brazil wakitembelea Kituo cha Afya Fuoni.
1 (4)
 WAZIRI wa Afya Zanzibar Hamad Rashoid Mohamed akizungumza na Ujumbe wa Wataalam wa Afya kutoka Nchi ya Brazil Afisini kwake Mnazi Mmoja Mjini Zanzibar.
7 (3)
UJUMBE wa wataalamu wa Afya kutoka Brazil wakiangalia takwimu za mama wajawazito wanaofika kupata huduma ya kujifungua Kituoni hapo.
Na Ramadhani Ali – Maelezo
Ujumbe wa watu nane wa Wataalamu wa afya kutoka Serikali ya Brazil upo Zanzibar kutekeleza ombi la Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Muhamed Shein kuitaka nchi hiyo kuzidisha ushirikiano  katika sekta ya Elimu, Afya na Utalii.
Ujumbe huo ukiongozwa na Mratibu Mkuu wa Kanda ya Afrika, Asia, nchi za Oceanic na Mashariki ya mbali Fabio Webber umefanya mazungumzo na Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohamed kujifunza changamoto zinazowakabili mama wajawazito na watoto wachanga.
Webber alisema Rais wa Zanzibar alipofanya mazungumzo na Balozi wa Brazil aliomba nchi hiyo kufungua ubalozi mdogo Zanzibar, kusaidia kuimarisha masuala ya afya na kuwajengea uwezo wafanyakazi wa sekta hiyo.
Balozi wa Heshma wa Brazil hapa Zanzibar Abdulsamad Abdulrahim alisema baada ya Serikali ya Brazil kufungua Ubalozi mdogo Zanzibar, wanaelekeza nguvu zao juu ya afya ya mama mzazi na mtoto pamoja na kuwajengea uwezo wafanyakazi wa kitengo hicho.
Alisema ujumbe huo utafanya ziara katika vituo mbali mbali vya afya Unguja na Pemba kuangalia changamoto zinazowakabili mama wajawazito wakati wa kujifungua na watoto wachanga na hatiamae kuzitafutia ufumbuzi.
Waziri wa Afya aliueleza ujumbe huo kuwa Serikali inaendelea kuimarisha huduma za afya ya msingi vijijini ili vituo vya afya vya huko viwe na uwezo na vifaa vya kutosha na wananchi waviamini na wavitumia.
Alisema hivi sasa kumekuwa na msongamano mkubwa wa wazazi katika Hospitali kuu ya Mnazimmoja huku vituo vya afya vijijini vyenye uwezo wa kutoa huduma za kuzalisha vinakosa wazazi kutokana na dhana kuwa huduma ni ndogo.
Alisema kuimarika kwa vituo vya afya vya vijijini vinavyotoa huduma ya mama na mtoto kutaipunguzia hospitali hiyo msongomano wa wazazi na kumudu kutoa huduma zilizo bora zaidi.
Ujumbe huo umeanza kazi ya kutembelea vituo vya afya vinavyotoa huduma ya kuzalisha kuona hali halisi na kujua changamoto zinazovikabili vituo hivyo na baadae kufanya uchambuzi wa kujua masuala yanayopaswa kutekelezwa kuongeza mashirikiano .

UTEKELEZAJI WA MRADI WA KUUNGANISHA GESI ASILIA KWA MATUMIZI YA MAJUMBANI WASHIKA KASI


utekelezaji 2
Sehemu ya eneo la barabara ya Ubungo Maziwa inayochimbwa kitaalamu bila kuvunja barabara ili kuruhusu bomba la gesi kuvuka barabara hiyo. 
utekelezaji 3
Bomba lenye kipenyo cha 315mm likiwa limelazwa katika mtaro tayari kufukiwa, hii ni sehemu ya bomba linalochukua gesi asilia kutoka kwenye bomba kuu linalotoka Mtwara hadi Dar es Salaam na kuunganisha na bomba linalotoka Ubungo kuelekea Mikocheni. 
Na Mwandishi Wetu.
Ni miezi mitatu sasa tangu Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani alipozindua rasmi mradi wa kuunganisha bomba kubwa la gesi asilia linalotoka Mtwara hadi Dar es Salaam na bomba la kipenyo kidogo linalotoka Ubungo kuelekea Mikocheni.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC, Mha. Kapuulya Musomba alifafanua kwamba utekelezaji wa mradi huo unalenga kuongeza matumizi ya gesi asilia kwa jiji la Dar es Salaam kwa kuwaunganisha wateja zaidi wa matumizi ya majumbani na viwandani.
Mradi huu unahusisha ujenzi wa msingi kwa ajili ya kusimika mtambo wa kupunguza mgandamizo, uunganishaji wa vipande vya mabomba, kuthibitisha njia ya bomba, uchimbaji na ulazaji wa bomba litakalochukua gesi kutoka bomba kubwa, uwekaji wa viainisho vya bomba linapopita na ujenzi wa daraja la waenda kwa miguu kuvuka mto Ubungo.
Akizungumza juu ya hatua za utekelezaji, Meneja Mradi Ndg. Denice Byarushengo alisema “mradi umepiga hatua kubwa na muhimu ambapo hadi sasa ujenzi wa msingi kwa ajili ya kusimika mtambo wa kupunguza mgandamizo umekamilika kwa asilimia 97%, uthibitisho wa njia ya bomba na zoezi la kuchimba mitaro kwa ajili ya mabomba umekalimilika kwa asilimia 76.8%, uunganishaji wa mabomba umekamilika kwa asilimia 88.6%, ulazaji na ufukiaji wa mabomba umekamilika kwa asilimia 56.9%, viainisho sita (6) vya bomba linapopita vimeshawekwa na ujenzi wa dara la waenda kwa miguu umekamilika kwa asilimia 90%”.
Aidha, Meneja Mradi aliongeza kwamba utekelezaji wa mradi huu unahusisha kuvuka mto Ubungo pamoja na barabara ya Ubungo Maziwa na ya Mandela ambapo hadi sasa kazi ya kuvuka mto Ubungo imekamilika kwa asilimia 100% na ile ya kuvuka barabara ya Ubungo Maziwa imekamilika kwa asilimia 50% wakati ya kuvuka barabara ya Mandela ikiwa mbioni kuanza.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC, Mha. Kapuulya Musomba ambaye alifanya ziara ya ukaguzi wa maendeleo ya mradi huo hapo jana alionyesha kuridhishwa na kazi na ubora wa utekelezaji wa mradi, Mha. Kapuulya alisema “pamoja na changamoto zilizopo, ninayo furaha kwamba kazi zinafanyika kwa kasi na ubora wa hali ya juu na ni matumaini yangu baada ya kuongea na mkandarasi pamoja na msimamizi wa mradi kwamba mradi utamalizika ndani ya wakati”.
Mradi wa kuunganisha bomba kubwa la gesi asilia na lile la Ubungo kuelekea Mikocheni lenye urefu wa kilomita 7.8 na uwezo wa kusafirisha gesi kiasi cha futi za ujazo milioni 7.5 kwa siku unalenga kuunganisha kiwanda cha Coca Cola Kwanza Ltd na BIDCO pamoja na wateja takribani 1000 wa majumbani ambao wataunganishwa kwa awamu.
Mradi huu utawezesha upatikanaji wa gesi asilia ya kutosha katika bomba litokalo Ubungo kuelekea Mikocheni kupitia barabara ya Sam Nujoma kusambaza gesi kwa wateja wa majumbani katika maeneo ya Ubungo, Shekilango, Mlalakuwa, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Sinza na Mikocheni. Mkandarasi wa mradi huu ni kampuni ya SINOMA kutoka Jamhuri ya Watu wa China na mradi unagharimu shilingi za kitanzania bilioni 4.2 ambazo ni fedha za ndani kutoka TPDC.
Vile vile mradi huu unatoa fursa kwa kampuni za wazawa kutoa huduma mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuuza bidhaa za ujenzi kama vile mabomba ambapo kwa sasa kampuni ya Plasco ndio mshindi zabuni hiyo. Mkandarasi wa mradi pia ana fursa ya kutoa kazi kwa mkandarasi mwingine (sub-contracting) lengo likiwa ni kuchochea ushirikishwaji wa wazawa katika sekta ya mafuta na gesi hapa nchini.

Shughuli za uchimbaji madini ya Kaolin zasimamishwa mgodi RAK Kaolin


IMG_20180725_140602_6_1532547173029
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kulia) akiongozana na mmoja wa wazee(katikati) katika kijiji cha Kimani wilayani Kisarawe baada ya kusimamisha shughuli za uchimbaji madini ya Kaolin katika mgodi unaomilikiwa na kampuni RAK Kaolin. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Happyness Seneda.
IMG_20180725_141707_4_1532547095741
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kulia), akionyeshwa jambo na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Happynes Seneda( wa pili kulia) wakati wakikagua migodi ya uchimbaji madini ya Kaolin wilayani humo.
IMG_20180725_142057_2
Moja ya maeneo yaliyokuwa yakichimbwa madini ya Kaolin katika Wilaya ya Kisarawe ambayo uchimbaji wake umesimamishwa kutokana na kutofuata sheria ya uchimbaji wa madini.
Na Zuena Msuya Pwani,
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo, amesimamisha shughuli za uchimbaji madini ya Kaolin katika mgodi unaomilikiwa na kampuni ya RAK Kaolin hadi pale wahusika watakapoeleza thamani halisi ya bei ya madini hayo yanayouzwa na kutumika viwandani, leseni ya mgodi, uchimbaji pamoja na umiliki ardhi.
Pia, alimtaka mmiliki wa leseni ya mgodi huo kuwasilisha wizara ya madini nakala ya mkataba walioingia kati yake na wachimbaji wa madini hayo katika mgodi huo, na namna ambavyo aliweza kumiliki eneo husika.
Nyongo alisimamisha shughuli za uchimbaji katika mgodi huo ulipo katika Kijiji cha Kimani wilayani Kisarawe mkoani Pwani, wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uchimbaji madini ya ujenzi Julai 25,2018.
Akizungumzia uamuzi wa kufunga mgodi huo ambao baadhi ya viwanda hutumia madini hayo kutengeneza bidhaa mbalimbali, Nyongo alisema kuwa, haridhishwi na shughuli za uchimbaji zinazofanya katika mgodi huo ikiwepo suala la umiliki wa ardhi, leseni ya mgodi, uchimbaji pamoja na biashara ya madini hayo viwandani.
Alifafanua zaidi kuwa, shughuli za uchimbaji na biashara ya madini katika mgodi huo hazionyeshi wazi taratibu wa ulipaji serikalini, mrabaha na tozo mbalimbali zilizowekwa kwa mujibu wa sheria ya madini ya mwaka 2010 iliyofanyiwa marekebisho 2017.
“Shughuli za uchimbaji wa madini hapa nchini ni lazima ziwanufaishe watanzania na taifa kwa ujumla kwa kuwawekea mazingira mazuri wamiliki wa ardhi, wamiliki wa leseni pamoja na wachimbaji na siyo kuwanyonya, pia kulipa mrabaha na tozo mbalimbali kwa lengo la kuongeza mapato serikalini, sasa mgodi huu taarifa zake zinakinzana licha yakuwawepo kwa muwekezaji kufanya shughuli za uchimbaji na kuendelea na biashara ya madini,” alisisita Nyongo.
Aidha, aliiagiza ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe kushirikiana na maafisa madini kufuatilia maeneo yote yenye madini ya Kaolin na kuhakiki leseni zilizopo pamoja na uhalali wake ili kufahamu idadi ya zilizokuwa hai na zilizomaliza muda wake.
Pamoja na mmbo mengine, aliendelea kusisitiza kuwa serikali itayafutia leseni zote sizoendelezwa na kuwa maeno hao wale wenye nia ya kuendeleza maeneo hayo kwa shughuli za uchimbaji madini.
Sambamba na hilo kuwataka wachimbaji na wamiliki wa migodi na wafanyabiashara ya madini kulipa mrabaha na tozo mbalimbali zilizowekwa kwa mujibu wa sheria ya madini ya mwaka 2010 na kufanyiwa marekebisho 2017 pamoja na kushiriki shughuli za kimaendeleo na kijamii katika maeneo yanayowazunguka.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Happyness Seneda alimuhakikishia Naibu Waziri Nyongo kuwa, kwa kushirikiana na Wizara ya Madini,anaimani mapato yote yaliyokuwa yakipotea sasa yataingia serikalini.
Seneda aliwaonya wawekezaji uchwara, wamiliki wa leseni na wachimbaji wasiowaaminifu kuwa kuanzia sasa kuacha    kufanya udanganyifu au ujanja ujanja katika sekta ya madini baada ya sheria ya madini ya 2010 kufanyiwa marekebisho 2017, kwa lengo la kuifanya sekta hiyo kuwanufaisha watanzania na taifa kwa ujumla.
Mkoa wa Pwani hasa katika Wilaya ya Kisarawe unasifika zaidi kwa upatikanaji wa madini ya Kaolin yanayotumika viwandani kutengeza bidhaa mbalimbali zikiwepo,Malumalu( Tiles) zinazotumika katika shughuli za ujenzi, karatasi, rangi ya nyumba n.k.

KURUGENZI YA TIBA SHIRIKISHI TAASISI YA MOYO YA JAKAYA KIKWETE YASHIKA NAFASI YA KWANZA KWA UFANYAJI KAZI BORA


Mkurugenzi wa Tiba kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Doroth Gwajima akimkabidhi tuzo ya kushika nafasi ya kwanza katika utendaji kazi bora wa kutoa huduma kwa wagonjwa  kwa Kurugenzi ya Tiba Shirikishi Kaimu Mkurugenzi wa Idara hiyo ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo Delila Kimambo wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza washindi iliyofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji Prof. Mohamed Janabi.
Picha 2
Mkurugenzi wa Tiba kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Doroth Gwajima akimkabidhi tuzo ya kushika nafasi ya kwanza katika kuwezesha utendaji kazi bora wa  kutoa huduma kwa wagonjwa kwa Kurugenzi ya Uuguzi Kaimu  Mkurugenzi wa Idara hiyo Robert Mallya wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza washindi iliyofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji Prof. Mohamed Janabi.
Picha 3
Baadhi ya Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Prof. Mohamed Janabi (hayupo pichani) akielezea kuhusu kazi zilizofanywa na Taasisi hiyo kwa mwaka 2018 katika kikao cha  wafanyakazi  na viongozi wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kilichofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo uliopo Jijini Dar es Salaam.
Picha 4
Baadhi ya Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Prof. Mohamed Janabi (hayupo pichani) akielezea kuhusu kazi zilizofanywa na Taasisi hiyo kwa mwaka 2018 katika kikao cha  wafanyakazi  na viongozi wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kilichofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo uliopo Jijini Dar es Salaam.

FREEDOM HOUSE YATOA MAFUNZO KWA WAANDISHI WA HABARI WA MITANDAO YA KIJAMII


1
Clerance Kipobota kutoka Shirika la Freedom House  ambaye amemwakilisha mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo akifungua semina ya (Alternative Media) kwa  waandishi wa habari za Mitandao ya kijamii (Online Platform Reporters) inayofanyika kwenye Hoteli ya  Flomi mjini Morogoro.
……………………………………………………………
Shirika la Kimataifa la Freedom House linaendesha mafunzo kwa waandishi wa habari wa  mitandao ya kijamii ‘bloggers’ kutoka mikoa mbalimbali nchini kwa ajili ya kuwajengea uwezo kuhusu namna kuendesha vyombo vya habari mbadala.
Mafunzo hayo ya siku mbili ‘Julai 26 – 27,2018’ kuhusu Vyombo vya habari mbadala ‘Alternative Media’ yaliyoratibiwa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari  Tanzania (UTPC) yanafanyika katika ukumbi wa Flomi Hotel mkoani Morogoro.
Awali akifungua mafunzo hayo,Mwakilishi wa Mkurugenzi wa shirika la Freedom House Clarence Kipobota alisema kupitia mafunzo hayo waendeshaji wa mitandao ya kijamii watajifunza mbinu mbalimbali kuhusu namna ya kuendesha mitandao yao.
“Tutajengeana uwezo na kujadili na kuunda jukwaa moja la waandishi ambao wanatumia Alternative Media”,alieleza.
4
Mwezeshaji wa semina hiyo Bw. Daniel Lema akitoa mada kwa waandishi wa habari katika semina inayofanyika katika hoteli ya Flomi mjini Morogoro.
kadam
Mwezeshaji John Kaoneka akitoa mada katika semina hiyo kuhusu mitandao ya kijamii.
23
567  1011121314151617
Victor Maleko Afisa Mafunzo , Utafiti na Machapisho UTPC akiwa katika semina hiyo.
18
Picha mbalimbali zikionyesha washiriki wa semina hiyo
1920
9
Waandishi wa habari wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua semina hiyo.
9

WAZIRI KIGWANGALLA ATOA SIKU 90 KWA TAWIRI KUFANYA SENSA YA MAMBA ZIWA RUKWA NA TFS KUANDAA MPANGO WA KITAIFA WA UVUNAJI MISITU



Na Hamza Temba, Songwe
…………………………………………………………..
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla ametoa miezi mitatu kwa Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) kufanya utafiti na sensa ya mamba katika ziwa Rukwa ili kubaini idadi yake na hatimaye kuishauri Serikali namna ya kudhibiti madhara yanayosababishwa na mamba hao kwa wananchi hususan wa jimbo la Songwe ikiwemo kuwavuna kama idadi yao itabainika kuwa kubwa kupita kiasi.
 
Dk. Kigwangalla ametoa agizo hilo jana katika kijiji cha Maleza, kata ya Mbangala, wilaya ya Songwe mkoani Songwe alipokuwa akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani humo kwa ajili ya kutatua mgogoro uliopo baina ya wananchi na Mamba wa ziwa Rukwa.
 
“Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori ambayo ipo chini ya wizara yangu, nawaagiza wafike hapa mara moja, ndani ya miezi mitatu wanipe majibu nini kifanyike kupunguza madhara yanayotokana na mamba kwenye ziwa Rukwa, wafanye sensa watuambie kuna Mamba wangapi lakini pia watushauri nini tufanye ili kudhibiti mamba hao wasiendelee kusababiaha athari kubwa kwenye maisha ya watu wanaoishi jirani, lakini pia wanaoutumia ziwa.
 
“Kwa sababu madhara yanaweza yakawa mengi, inawezekana mamba wameshakuwa wengi na samaki wamebaki wachache, kwahivyo hata mamba nao mwishowe wataanza kufa ama wataanza kutafuta chanzo kingine cha chakula pengine ndio maana wameanza kutafuta binadamu wanakwenda ziwani kwasababu wanakuwa na njaa, inabidi wasogee ufukweni wawinde chochote kinachosogea karibu na maji” alifafanua Dk. Kigwangalla. 
 
Dk. Kigwangalla ametoa agizo hilo kufuatia malalamiko mbalimbali yaliyowasilishwa kwake na mbunge wa Jimbo la Songwe, Phillipo Mulugo ambaye amesema kumekuwepo na matukio mengi ya mamba kushambulia na kuuwa wananchi wa vijiji jirani wanaofata huduma mwambao wa ziwa Rukwa. 
 
Katika hatua nyingine Dk. Kigwangalla ametoa miezi mitatu kwa Wakala wa Huduma za misitu Tanzania kuandaa mpango wa kitaifa kwa kila wilaya na vijiji nchini utakaoweka utaratibu maalum wa namna na sehemu wananchi watakayopata huduma ya kuni mkaa.
 
“Utaratibu uwekwe na muuweke nchi nzima, kila wilaya, kila kata, kila kijiji uwekwe utaratibu wananchi watapata wapi mkaa, watapata wapi kuni, kibali cha kuvuna kitapatikana wapi, utaratibu uwe wazi, sio kusubiri kwenye mageti unakamata, hapana weka utaratibu kwanza, ukishaweka utaratibu atakayevunja sheria hata ukimkamata ukimpeleka polisi utakuwa umemrahisishia OCD kazi. 
 
“Kwa sababu hata OCD atakuwa anajua kwamba katika hii wilaya ninayoiongoza hapa ndio mipaka ya mkaa, hapa ni mipaka ya kuni, wewe umetoa wapi, kibali chako kiko wapi, umevunja sheria, mahakamani” ameeleza Dk. Kigwangalla. 
 
Wakati huo huo, Dk. Kigwangalla ametangaza kutaifishwa kwa greda ambalo limekutwa likiwa limetelekezwa na watu wasiojulikana ambao walikuwa wakichimba mchanga wa dhahabu (makinikia) kinyume cha sheria ndani ya Hifadhi ya msitu wa Patamela wakati wa ziara yake wilayani Songwe.
 
Kufuatia tukio hilo, amemuagiza Kamanda wa Polisi wa wilaya hiyo kulinda eneo hilo na kutafuta dereva atakayeendesha greda hilo hadi kituo cha polisi kwa ajili ya kufuata taratibu za sheria za kulitaifisha na wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akizungumza na wananchi wa kijiji cha Maleza kata ya Mbangala wilaya ya Songwe mkoani Songwe alipofanya ziara ya kikazi katika kijiji hicho jana kwa ajili ya kutatua mgogoro wa mamba wa ziwa Rukwa ambao wamekuwa wakidhiru wananchi wa kijiji hicho na vijiji jirani.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akitoa agizo la kutaifishwa kwa greda (pichani nyuma) lililokutwa ndani Hifadhi ya Msitu wa Patamela baada ya kutelekezwa na watu watu wasiojulikana waliokuwa wakichimba mchanga wa dhahabu (makinikia) kinyume cha sheria ndani ya Hifadhi hiyo katika wilaya ya Songwe mkoani Songwe jana.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akitoa maelekezo kwa uongozi wa wilaya ya Songwe kufuatia greda lililokutwa ndani Hifadhi ya Msitu wa Patamela ambalo limetelekezwa na watu wasiojulikana waliokuwa wakichimba mchanga wa dhahabu (makinikia) kinyume cha sheria ndani ya Hifadhi hiyo katika wilaya ya Songwe mkoani Songwe jana.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akishirikiana na baadhi ya viongozi wa wilaya ya Songwe kuzima moto uliokutwa ukiwaka ndani ya Hifadhi ya Msitu wa Patamela wakati wa ziara yake ya kikazi wilayani humo jana.
Dk Hamisi Kigwangalla akishirikiana na baadhi ya viongozi wa wilaya ya Songwe kuzima moto uliokutwa ukiwaka ndani ya Hifadhi ya Msitu wa Patamela wakati wa ziara yake ya kikazi wilayani humo jana.
Juhudi za kuzima moto zikiwa zinaendela.
Dk Kigwangalla akiwa anazungumza na wananchi wa kijiji Maleza.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Songwe, Philipo Mulugo alipokuwa akiwasilisha malalamiko ya wananchi wa jimbo lake ambao wamekuwa wakipata madhara makubwa ya mamba wa ziwa Rukwa.

MAMLAKA HIFADHI YA NGORONGORO KULIPENDEZESHA JIJI LA DODOMA


????????????????????????????????????
Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Profesa Davis Mwamfupe (katikati), Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi na Kaimu Meneja Uhusiano Mamlaka Hifadhi ya Ngorongoro, Joyce Mgaya wakisaini hati ya makubaliano ya kuboresha mandhari ya mizunguko ya magari kwenye barabara kuu za jiji hilo. Kwenye uboreshaji huo wa mandhari Mamlaka Hifadhi ya Ngorongoro itaweka vivutio mbalimbali kutangaza utalii
……………………
Na: Abuu Kimario
Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imeingia makubaliano na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuboresha mandhari ya mizunguko ya magari (roundabout) kwenye barabara kuu za jiji hilo.
Makubaliano hayo yamefikiwa leo kwenye hafla ya fupi ya kutiliana saini ambapo jiji la Dodoma liliwakilishwa na Meya, Profesa Davis Mwamfupe na Mkurugenzi Mtendaji,  Godwin Kunambi na upande wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro iliwakilishwa na Kaimu Meneja Uhusiano, Joyce Mgaya kwa niaba ya Mhifadhi Mkuu wa mamlaka hiyo Dkt. Fredy Manongi.
Kwenye makubaliano hayo Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imekubali kuifanyia ukarabati mizunguko mitatu ya magari ambayo ni mizunguko ya barabara kuu za Dar-es-Salaam (Shabiby), Singida na Arusha.
Akiwasilisha salamu za Mhifadhi Mkuu, Kaimu Meneja Uhusiano Mgaya amesema, uongozi wa jiji la Dodoma kuichagua mamlaka hiyo ni heshima kubwa na wanaipokea kwa mikono miwili na pia mamlaka hiyo itaendelea kushirikiana na halmashauri ya jiji kwenye kuibua fursa mbalimbali za kitalii.
Aidha, Mgaya ameongeza kuwa makubaliano hayo yaliyofikiwa ni fursa ya Halmashauri ya jiji la Dodoma na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kubadilishana uzoefu kwenye maeneo ya uhifadhi wa mazingira na kuboresha mandhari.  
Kwa upande wake Meya wa Jiji la Dodoma, Mstahiki Davis Mwamfupe amesema nia ya uongozi wa jiji la Dodoma ni kulifanya liwe jiji la mfano wa kuigwa na majiji mengine ya Tanzania, barani Afrika na duniani kwa kuwa na mazingira bora kuishi na mandhari yenye kuvutia.
Nae Mkurugenzi Mtendaji, Godwin Kunambi ameishukuru Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa kukubali ombi la kutengeneza sanamu kubwa ya tembo kama ishara ya kuhifadhi historia ya chimbuko la jina la mkoa wa Dodoma. Kwa mujibu ya maelezo ya wenyeji wa mkoa huo jina Dodoma limetokana na neno la kigogo “idodomya” baada ya tembo kudidimia ardhini miaka mingi iliyopita.

DAKTARI BINGWA WA MAGONJWA YA MOYO WA HEAMEDA MEDICAL CLINIC ATOA USHAURI NAMNA YA KUEPUKA MAGONJWA YA MOYO


1
DAKTARI Bingwa wa magonjwa ya moyo nchini kutoka Heamedia Medical Clinic Dk.Hery Mwandolela akimuelezea mwandishi wa habari mambo mbalimbali yanayosababisha watu kukumbwa na magonjwa ya moyo katika banda la Kliniki hiyo lililopo kwenye viwanja vya maonyesho vya Sabasaba Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam.
2
 DAKTARI Bingwa wa magonjwa ya moyo nchini kutoka Heamedia Medical Clinic Dk.Hery Mwandolela akionyesha mfano wa moyo wa binadamu.
3
DAKTARI Bingwa wa magonjwa ya moyo nchini kutoka Heamedia Medical Clinic Dk.Hery Mwandolela akifafanua jambo katika banda hilo kulia ni Julieth Mutabiilwa Afisa Uhusiano na Huduma kwa wateja Heameda Medical Clinic
4
DAKTARI Bingwa wa magonjwa ya moyo nchini kutoka Heamedia Medical Clinic Dk.Hery Mwandolela akizungumza na mmoja wa wananchi waliotaka kupata ufafanuazi mbalimbali wa magonjwa ya moyo alipotembelea katika banda hilo.
……………………………………………………………….
DAKTARI Bingwa wa magonjwa ya moyo nchini kutoka Heamedia Medical Clinic Dk.Hery Mwandolela amesema kuna umuhimu mkubwa wa kila mmoja wetu kuhakikisha anapima afya yake mara kwa mara huku akitaja sababu zinazosababisha ugonjwa wa moyo.
Pia amesema ni vema kila mtu akafahamu namba saba muhimu kwa afya yako na kusisitiza kitendo cha kuchelewa kutambua ugonjwa mapema kunasababisha gharama kubwa zaidi ya ungetambua mapema na kukika ugonjwa husika.
Dk.Hery Mwandolela amesema hayo leo kwenye mahojiano maalum wakati anazungumza kwenye  Maonesho ya Sabasabua  ya Bishara ya kimataifa yanayoendelea viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Amesema lengo la uwepo wake kwenye banda hilo kwanza unalenga kuwakumbusha wananchi mbalimbali kutambua umuhimu wa kupima afya mara kwa mara kwani inasaidia kupunguza gharama za matibabu.
Pia amesema yupo kwenye maonesho hayo kwasababu anataka kuwafahamisha Watanzania huduma bora na za kiwango cha juu katika kutibu magonjwa ya moyo ambayo yaafanywa na madaktari wabobezi waliopo Heameda Medical Clinic iliyopo mtaa wa Fubu maeneo ya Bunju B jijini.
Dk.Mwandolela amesema pamoja na kutoa huduma kwa kiwango cha hali ya juu wameweka gharama nafuu ambazo kila mmoja anaweza kumudu ukilinganisha na maeneo mengine.
Akifafanua zaidi kuhusu kupima afya mara kwa mara amesema magonjwa kama ya kupanda kwa shinikizo la damu na kisukari huweza kuja bila dalili yeyote na wakati mwingine yanagundulika baada ya mhusika kupata madhara makubwa.
“Njia pekee ya kukabiliana na magonjwa haya ni kujenga tabia ya kupima afya zetu hata kama hatusikii dalili zozote za ugonjwa, kwani hii itsaidia kugundua tatizo mapema na kuchukua hatua madhubuti za kukabiliana nalo.
“Ugonjwa kama kupanda kwa shinikizo la damu hupewa jina muuaji kimya kimya kutokana na tabia yake ya kuwepo bila kuonesha dalili zozote za ugonjwa wakati ukiharibu viungo kama moyo, macho, figo na hata ubongo,”amesema Dk.Mwandolela.
Ameongeza unaweza kuwa na tatizo la kupanda kwa shinikizo la damu bila kuwa na dalili zozote na njia pekee ni kupima shinikizo la damu.
Amesema kupanda kwa shinikizo la damu bila kudhibitiwa huweza kusababisha madhara makubwa katika moyo, mishipa ya ya damu, macho, figo na ubongo.
“Hivyo tupo hapa katika maonesho pamoja na kutoa ushauri wa masuala ya afya tunaenelimisha Watanzania umuhimu wa kupima afya zao.Ukipima afya mapema ni rahisi kutatatua tatizo kwa kupata dawa za kukinga ambazo gharama yake ni nafuu kuliko dawa za kutibu.
“Ukigundua tatizo mapema ni rahisi kwenda kwa hospitali ukiwa mwenyewe na hivyo hata gharama ya usafiri itakuwa ya kawaida lakini ukichelewa hadi tatizo litokee maana yake itabidi ubebwe na hautaweza kupanda hata daladala, hivyo gharama zitaongezeka.Ndio maana tunashauri upimaji wa afya wa mara kwa mara,”amesema Dk.Mwandolela
Kuhusu afya ya moyo wako , Dk.Mwakandolela amesema ni vema ukaonana na daktari ili kufanya vipimo vitakavyosaidia kufahamu hali halisi ya moyo wako.Endapo huna tatizo lolote ni vizuri kufanya vipimo vinavyokutaarifu kuhusu afya ya moyo na mishipa ya damu angalau kila baada ya miaka miwili.
Akizungumzia namna ya kufahamu namba saba muhimu kwa afya yako , amesema mhusika anatakiwa kufahamu uzito unaokubalika kwa afya bora, kufahamu shinikizo la damu , kufahamu ukubwa wa mzunguko wa kiuno chak na  kiwango cha sukari katika damu.
Pia kufahamu kiwango cha mafuta katika damu na kufahamu kiwango cha mapigo ya moyo wako
Amezungumzia umuhimu wa kufanya mazoezi angalau nusu saa kwa siku, au mara tano kwa juma na kwamba mazoezi hayo yanaweza kuwa ni kwa kutembea, kukimbia ,kuendesha baiskeli, kufanya kazi zinazotumia nguvu na kushiriki katika michezo.
Ametoa rai kwa Watanzania ni vema wakapata muda wa kupumzika, kukabiliana na msongo wa mawazo, kujumuika na unawapenda na kupunguza kiasi cha chumvi kwenye chakula.