RAIS DONALD TRUMP AMFUKUZA KAZI KAIMU MWANASHERIA MKUU

Rais Donald Trump amemfukuza kazi Kaimu Mwanasheria Mkuu Bi. Sally Yates aliyeteuliwa kushika wadhifa huo wakati wa Barack Obama.

Ikulu wa Marekani imemtuhumu Bi. Yates kwa kuisaliti Idara ya Sheria kwa kukataa kuunga mkono agizo la rais la kuwapiga marufuku raia wa Mataifa ya Kiislam kuingia Marekani.

Bi. Yates aliwaagiza wanasheria wa Idara ya Sheria kutotetea agizo la kuzuia wahamiaji, kutokana na kuona agizo hilo linakiuka sheria.
Rais Donald Trump akitia saini moja ya maagizo yake kwa kutumia mamlaka yake ya urais
                                             Dana Boente ameteuliwa kushika kwa muda wadhifa huo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni