MAVUNDE AAHIDI KUZITATUA KERO ZA WAFANYABIASHARA NDOGO NDOGO

MBUNGE wa Jimbo la Dodoma mjini, Anthony Mavunde leo amefanya ziara ya kutembelea maeneo ya katikati ya mji na kusikiliza kero zinazowakabili wananchi hasa wafanyabiashara ndogo ndogo.

Hatua hiyo ya Mavunde imetokana na Ofisi yake ya Mbunge kuweka utaratibu wa kuwasikiliza wananchi kero zao na matatizo yao kila Alhamis(kero za Ardhi) na Ijumaa(Mambo ya kijamii).

Hata hivyo kwa siku ya leo kutokana na mapumziko ya Sikukuu ya Eid El Fitr, Mavunde ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu ameamua kutembea maeneo mbalimbali ya mjini katikati na kusikiliza kero za wananchi.

Maeneo aliyotembelea ni pamoja na eneo la ‘One way’ ambalo kuna wafanyabiashara wengi wakubwa na wadogo na barabara ya sita ambako ni maarufu kwa maduka ya simu katika kata ya Madukani.

Akizungumza mara baada ya kuwatembelea wananchi hao, Mavunde ameahidi kuzipatia ufumbuzi baadhi ya kero zinazowasibu wafanyabiashara hao.
Mbunge wa Dodoma mjini, Anthony Mavunde akiwasikiliza wafanyabiashara ndogo ndogo(machinga) katika eneo la ‘One way’.
Mbunge wa Dodoma mjini, Anthony Mavunde akiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyabiashara katika maduka ya simu barabara ya sita.
Mbunge wa Dodoma mjini, Anthony Mavunde akiwa kwenye moja ya maduka ya simu eneo la barabara ya sita.
Mbunge wa Dodoma mjini, Anthony Mavunde akimsikiliza mmoja wa wakazi wa Dodoma wakati alipotembelea maeneo mbalimbali ya mji.
Mbunge wa Dodoma mjini, Anthony Mavunde akisalimiana na mmoja wa walinzi katika eneo la barabara ya sita.
Mbunge wa Dodoma mjini, Anthony Mavunde akiwasikiliza wafanyabiashara ndogo ndogo(machinga) katika eneo la ‘One way’.
Mbunge wa Dodoma mjini, Anthony Mavunde akisalimiana na wananchi katika maeneo aliyotembelea.

MAKAMU WA RAIS AZINDUA MWONGOZ KWA WAPELELEZI NA WAENDESHA MASHITAKA WA KESI ZA WANYAMAPORI NA MISITU


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu  Hassan akikata utepe kuashiria Uzinduzi Kitabu cha Mwongozo kwa Wapelelezi na Waendesha Mashitaka wa Kesi za Wanyamapori na Misitu kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, wengine pichani ni Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Profesa Jumanne Maghembe (kulia),Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Bw.  Alvaro Rodrigues na kushoto ni Muendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali Biswalo Mganga na Naibu wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Masauni (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais - Ikulu) Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Naibu wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Masauni Kitabu cha Mwongozo kwa Wapelelezi na Waendesha Mashitaka wa Kesi za Wanyamapori na Misitu kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, katikati ni Muendesha Mashitaka Mkuu wa Serikali Biswalo Mganga. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais - Ikulu)Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu  Hassan akihutubia wakati wa Uzinduzi wa Mwongozo kwa Wapelelezi na Waendesha Mashitaka wa Kesi za Wanyamapori na Misitu kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais - Ikulu)
 
Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

Makamu wa Rais Samia Suluhu azindua muongozo kwa watumishi katika kesi za wanyamapori.

MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan amewataka waendesha mashitaka, polisi na wapelelezi wa kesi za wanyamapori na misitu kubadilika katika kazi zao ili kulinda rasilimali hizo kwa vizazi vya sasa na vijavyo.Aidha, ameitaka mahakama kutoa muongozo kwa watumishi wake kuhusu namna ya kuendesha kesi zinazohusiana na nyara za serikali kwa lengo la kuwa na uwiano sawa katika utoaji amri.

Samia amesema hayo leo mjini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Mwongozo kwa wapelelezi, waendesha mashitaka na Polisi wa kesi za wanyamapori na misitu ulioandaliwa na Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP).

Amesema wote hao wanatakiwa kufanya kazi zao ipasavyo kuhakikisha usalama wa wanyamapori na misitu kwani kwa kupoteza maloiasili hizo kunafanya uchumi wa nchi kushuka na kwamba wasifanye kazi hiyo kwa kuweka mazingira ya rushwa.

Amesema, kazi za kupeleleza na kuendesha kesi za wanyamapori zimekuwa na ushawishi mkubwa wa rushwa kutoka kwa wahusika na kuwataka kufikiria maslahi mapana ya nchi na sio wao binafsi.

"Jamani, msiogope kufa, kifo kipo na kila mmoja wetu atakufa hata mnyama ikiwemo huyo FaruJohn, muhumu ni namna ya kujua aina ya kifo utakachokufa, lakini Jambo la kusikitisha mmekuwa mkiponzwa na fedha, wahenga walisema 'fedha ni sabuni ya roho lakini pia walisema fedha ni fedheha," amesema Samia.

ameongeza kuwa, Rais Magufuli ana lengo kubwa la kulinda maliasili za nchi hii na kwamba kutaka kwake kuwepo kuwepo kwa miongozo hiyo katika mahakama kutasaidia mahakimu na majaji kutoa adhabu na dhamana zinazowiana.

Ameongeza, mara kadhaa kumejitokeza majaji na mahakimu kutoa adhabu zinazotofautiana au masharti yanayo tofautiana katika kesi zenye mazingira sawa.

Aidha amemtaka DPP kufanya namna ya kuwapeka watumishi hao kwenye mbuga za wanyama, vyanzo vya maji na maeneo ya mbali mbali yenye misitu ili kujionea ni kwa namna gani rasilimali za nchi zinavyopotea kwa wanyama kuuawa kwa kukosa maji.

Amesema, mwongozo huo uliotolewa utasaidia kuboresha upelelezi na uendeshaji wa mashitaka na kwamba mapambano dhidi ya ujangili na uhalifu yatakoma na matokeo chanya yatakuwa yakipatikana katika kesi mbali mbali na serikali kuweza kupata mapato yake katika sekta ya utalii.

Akitoa takwimu za sekta ya wanyamapori, Samia amesema, Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) ya mwaka 2009, ilionesha kuwa Tanzania ilikuwa na tembo 109,051 na sensa ya mwaka 2014 ilionesha idadi ya tembo imepungua na kufikia tembo 43,330 ambao sawa na asilimia 60.3 ya tembo wote.

Alisema sababu kuu ya kupungua kwa tembo hao ni ujangili na kwamba takwimu rasmi za Sekretarieti ya Maktaba wa Kimataifa unaoratibu biashara ya wanyama waliohatarini kutoweka (CITES), ilionesha asilimia 70 ya meno ya tembo yaliyokamatwa duniani kote kati ya mwaka 2008 na 2013, yalitokea Afrika Mashariki nchi za Tanzania na Kenya ambapo kiasi kikubwa  kilitokea Tanzania.

Kwa mujibu wa sensa ya Taasisi ya International Union for the Conservation of Nature (IUCN) ya mwaka 2013, Tanzania ilishuka hadi namba tatu kwa idadi ya tembo kwa asilimia 13 ya tembo wote waliopo barani Afrika ikiwa nyuma ya Botswana (asilimia 33) na Zimbabwe (asilimia 16).

Naye DPP Biswalo Mganga amesema katika kipindi cha mwaka 2014 na 2017,  washitakiwa 100 walihukumiwa kulipa faini ya bilioni 1.1 na vifungo virefu ambazo tayari imeshalipwa serikalini.Aidha, watuhumiwa 80 walihukumiwa kifungo cha miaka 20 na 30 gerezani na faini ya bilioni 164.7 ambayo bado haijalipwa.

Alisema suala la dhamana kwa makosa makubwa yanayohusu wanyamapori  waliohatarini kutoweka ikiwemo tembo na faru, watuhumiwa wengi wamekuwa wakitoroka na kusababisha kesi kutoendelea dhidi yao.

Ameongeza mwaka kati ya 2010 na 2015 mashauri 13 yanayohusiana na nyara za serikali zenye thamani ya milioni 800 yalifikishwa katika Mahakama za Mkoa wa Dar es Salaam lakini watuhumiwa wake walitoweka baada ya kupewa dhamana.

Hata hivyo, alisema asilimia 69 ya watuhumiwa hao ni raia wa kigeni na asilimia 31 ni Watanzania; wakati mahakama inapotoa dhamana, moja ya masharti yake ni kunyang'anywa hati zao za kusafiria.Alifafanua kuwa kati ya kesi hizo 13 watuhumiwa waliua jumla ya tembo 300, chui nane, Kobe 210, twiga,kiboko, pundamilia na ndege wa aina mbalimbali wenye thamani ya milioni 800.


Amesema, takwimu zinaonesha kuwa asilimia 70 ya washitakiwa huruka dhamana na kukimbia kesi pindi wanapopewa dhamana kwa hiyo, anajitahidi kuchukua hatua madhubuti kwenye suala la dhamana hasa kwenye kesi zinazohusu meno ya tembo na faru wanaokaribia kutoweka nchin.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AKISALIMIANA NA MBUNGE SERUKAMABA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisikiliza jambo kutoka kwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini Peter Serukamba (CCM). walipo kutana katika viwanja vya Bunge Mjini Dododma leo June 28, 2017. Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

MJAMZITO SERENA WILLIAMS AJIANIKA UTUPU KATIKA JARIDA LA VANITY FAIR

Mjamzito Serena Williams amepiga picha akiwa utupu itakayotumika katika ukurasa wa mbele wa jarida la Vanity Fair.

Nyota huyo wa tenesi alibaini kuwa ni mjamzito akitarajia kupata mtoto wake wa kwanza na muasisi wa Reddit, Alexis Ohanian kabla ya michuano ya Australian Open, Januari.

Serena ameliambia jarida la Vanity Fair kuwa alikuwa hajahisi jambo lolote kuhusu ujauzito wake hadi pale alipojisikia kuugua akiwa uwanjani akifanya mazoezi.

POLISI MUASI ASHUSHA MAKOMBORA KATIKA JENGO LA MAHAKAMA KUU

Mahakama ya Kuu ya Venezuela imeshambuliwa kwa mabomu yaliyodondoshwa na helkopta katika kile rais wa nchi hiyo Nicolás Maduro alichokiita kuwa ni shambulizi la kigaidi.

Picha zilizowekwa kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha helkopta ya polisi ikizunguka angani kabla ya kuachia mabomu na kusikika mlipuko mkubwa, kitendo kilichofanywa na polisi.

Afisa wa polisi anayesemekana kuiba helkopta hiyo, alitoa taarifa akiishutumu serikali kwa kuiita kuwa ni ya kihalifu. Rais Maduro amekuwa akikabiliwa na maandamano ya umma.
Polisi wa Venezuela wakiwa wamelizingira jengo la Mahakama Kuu baada ya kulipuliwa mabomu

SERIKALI WILAYANI KOROGWE YAAPA KUKOMESHA MIMBA ZA UTOTONI



MKUU wa wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga,Mhandisi
Robert Gabriel akizungumza wakati makabidhiano ya vyumba vya madarasa vitano na vyoo ishirini na nne,mradi maji na uzio wa shule ya msingi jitengeni iliyopo Mji mdogo wa Mombo uliofanywa na taasisi isiyo ya kisherikali A better World ya Canada ikishirikiana na Vuga development Initiative kulia ni Founder wa A Better World Canada Eric Rajabu na  Mkurugenzi wa Taasisi ya A Better Worild Canada
nchini Tanzania,Aizidi Kaoneka
Founder wa A Better World Canada Eric Rajabu kushoto akizungumza katika halfa hiyo kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya A Better Worild Canada nchini Tanzania,Aizidi Kaoneka
Mkurugenzi wa Taasisi ya A Better Worild Canada nchini Tanzania,Aizidi Kaoneka akizungumza katika halfa hiyo
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Korogwe Vijijini,Gorge Nyaronga akizungumza katika halfa hiyo  
MKUU wa wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga,Mhandisi Robert Gabriel kushoto akimpatia zawadi ya kitenge  Founder wa A Better World Canada Eric Rajabu akimshukuru kwa msaada wa ujenzi wa madarasa na vyoo na uzio

RAIS DKT.MAGUFULI AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

ilu1
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza kikao cha Baraza la Mawaziri leo tarehe 26/06/2017 Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU
ilu2Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza kikao cha Baraza la Mawaziri leo tarehe 26/06/2017 Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA ASHIRIKI SWALA YA IDD EL FITRI KATIKA MSIKITI WA RIADHA MJINI MOSHI.

Waziri Mkuu wa Tanzania,Kassim Majaliwa akiwasili katika msikiti wa Riadha mjini Moshi kwa ajili ya Swala ya Eid el Fitri iliyofanyika kitaifa mjini Moshi.
Waumini wa Dini ya Kiislamu wakiwa....soma zaidiwww.manyaraleotz.blogspot.com katika Msikiti wa Riadha mjini Moshi.
Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa aikishiriki Swala ya Idd el Fitri iliyofanyika kitaifa katika msikiti wa Riadha mjini Moshi.
Baadhi ya waumini wa Dini ya Kiislamu wakishitiki Swala Idd.
Swala ya Idd ikifanyika katika msikiti wa Riadha mjini Moshi.
Waziri Mkuu wa Tanzania,Kassim Majaliwa,akiwa na Sheakh Mkuu wa Tanzania ,Mufti Abubakary Zubery ,Waziri wa Maliasili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu ,Said Mwema.
Mshindi wa kuhifadhi Quran tukufu ,Ibrahim Mitigo akionesha namna ambavyo alivyohifadhi Quran wakati wa Swala ya Idd el Fitry iliyofanyika katika msikiti wa Riadha mjini Moshi.
Waumini wa Dini ya Kiislamu wakishiriki Swala ya Idd mjini Moshi.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa ,akizungumza wakati wa Swala ya Idd el Fitry iliyofanyika kitaifa katika Msikiti wa Riadha mjini Moshi.
Mufti wa Tanzania na Sheakh Mkuu,Abubakary Bin Zubery akitoa nasaha zake wakati wa Swala ya Idd iliyofanyika kitaifa mjini Moshi.
Waumini wa Dini ya Kiislamu wakishiriki katika Swala ya Idd El Fitry iliyofanyika mskiti wa Riadha mjini Moshi

                                 Na Mahmoud Ahmad Kilimanjarowww.manyaraleotz.blogspot.com.

SERIKALI imeahidi kuongeza kasi katika zoezi la ukamataji wa wahusika wa matukio ya mauaji yaliyotokea Kibiti,Rufiji na Mkuranga mkoani Pwani na kuhakiksha wanafikishwa mbele ya vyombo vya sheria.
 

Waziri Mkuu wa Tanzania ,Kassim Majaliwa aliyasema hayo jana katika baraza la Idd lililofanyika kitaifa katika mji wa Moshi mkoani Kilimanjaro lkitanguliwa na Swala ya Idd El Fitri iliyofanyika kitaifa katika msikiti wa Riadha.
 

“Kinachofanyika sasa nikuhakikisha kwanza tunawapata waharifu halisi ilikuepuka kuingiza watu wasio husika, kama vile hao wenye hisia kwamba mauaji haya yanafanywa labda na waislamu hapana .”alisema Mh Majaliwa .
Alisemakaz kubwa inayofanywa sasa ni kuchuja na kujua nani hasa anshiriki katika mauaji hayo huku akiwashukuru watanzania ambao tayari wameanza kutoa ushirikiano kwa kuanza kueleza nani wanahusika katika tukio hilo.
 

“Kazi yetu ni kuwapeleleza pale ambapo tunauthibitisho wa ushiriki wao na hatua kali zitachukuliwa dhidi yao na kazi hiyo inaendelea vizuri.”alisema Majaliwa.
Mapema katika taarifa ya Baraza kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) iliyosomwa na kaimu katibu Mkuu,Sheakh Salim Amir Abeid alisema Bakwata imeshtushwa na matukio ya mauaji ya kutisha ya watu wasio na hatia katika maeneo ya mkoa wa Pwani.
Alisema kutokana na matukio hayo Baraza kuu linatoa pole kwa familia zilizopoteza ndugu na jamaa zao katika matukio hayo aliyoyataja kutokuwa na hata chembe ya kibinadamu .
 

“Kumekuwepo na matukio ya kutisha ya mauaji ya watu wasio na hatia katika maeneo ya mkoa wa Pwani,matukio ambayo yametushtua sana na kuisikitisha mioyo yetu,baraza kuu la waislamu la Tanzania kwanza kabisa linatoa pole kwa familia zilizopoteza ndugu na jamaa zao katika matukio hayo ya kinyama yasio na chembe ya kibinadamu hata kidogo.”alisema Abeid
Alisema Bakwata inasikitishwa na vitendo vyenye viashiria vya kutaka kuichafua dhima nzuri ya Tanzania kuwa ni kisiwa cha amani na utulivu hasa pale matukio hayo yanapo husishwa na na Dini ya Kiislamu.
 

“Uislamu ni dini ya amani upendo kuvumilia na nakuishi pamoja na watu wa imani tofauti na kwamba yeyote afanyae matendo yoyote na kinyama kama hayo katu haiwakilishi uislamu na baraza linawataka waislamu kushikamana.”alisema Abeid.

WANAWAKE WAWEKA REKODI YA KUCHEZA SOKA KATIKA KILELE CHA UHURU,MLIMA KILIMANJARO.

Timu za Gracier fc na Volcano fc zikijiandaa kwa mchezo wa kirafiki katika eneo la Kreta,kilele cha Uhuru ,Mlima Kilimanjaro.
Kundi la Wanamichezo 60 wakiwemo wachezaji 30 wa timu za taifa za wanawake kutoka mataifa zaidi ya 20 walioshiriki kuweka rekodi ya kucheza soka katika eneo la kreta lililopo katika kilele cha Uhuru.
Baadhi ya wachezaji walioshiriki mchezo wa soka katika Kilele cha uhuru ,Mlima Kilimanjaro.
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro(KINAPA) Betrta Loibook akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii nchini ,Devota Mdachi walipowapokea wachezaji wa timu za taifa za wanawake wakati wakishuka kutoka Mlima Kilimanjaro kupitia geti la Mwika.
Mhifadhi Mkuu KINAPA,Betrita Loibook pamoja na Afisa Uhusiano Mkuu wa Bodi ya Utalii,Geofrey Tengeneza wakifurahia mara baada ya wachezaji wa timu za taifa za wanawake kutoka mataifa mbalimbali duniani kuweka rekodi ya kucheza mpira katika kilele cha Uhuru .
Wachezaji wa timu za Taifa wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Bodi ya utalii pamoja na Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro.
Wachezaji wakiweka pozi la picha katika Kreta ya Uhuru katika kilele cha Uhuru juu ya Mlima Kilimanjaro.

                       Na Mahmoud Ahmad Kilimanjaro
Wachezaji 30 wa timu za soka za mataifa mbalimbali wameshiriki kuweka rekodi ya kwanza Duniani kwa kucheza mchezo wa kirafiki katika mlima Kilimanjaro ,umbali mita 5731 kutoka usawa wa bahari.
Rekodi nyingine iliyowekwa ni ile ya mwamuzi wa kike wa Tanzania anayetambulika na Shirikiho la Soka Duniani (FIFA) Jonesia Rukyaa kuchezesha mchezo huo wa dakika 90 uliomalizika kwa sare ya bila kufungana

RAIS WA ZAMANI WA BOTSWANA, KETUMILE MASIRE AMEFARIKI DUNIA

Sir Ketumile Masire enzi za uhai wake

Rais wa zamani wa Botswana, Sir Ketumile Masire amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 91.

Taarifa zilizotolewa zinasema Sir Masire alifariki dunia usiku wa kuamkia leo akiwa hospitali alikokuwa amelazwa toka wiki iliyopita.

Sir Ketumile Masire alikuwa Rais wa Botswana kuanzia mwaka 1980 hadi 1998 na enzi za uhai wake aliongoza juhudi mbalimbali Barani Afrika ikiwa ni pamoja kuongoza tume iliyochunguza mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994.

MD KAYOMBO ABAINISHA MPANGO MKAKATI JUU YA UKUSANYAJI MAPATO MWAKA 2017/2018


Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake Kibamba CCM Jijini Dar es salaam
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake Kibamba CCM Jijini Dar es salaam

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo amebainisha kuwa Manispaa ya Ubungo imejipanga vyema kukusanya mapato makubwa katika kipindi Cha Mwaka mpya wa Fedha 2017/2018.

Akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake Kimbamba CCM, Mkurugenzi Kayombo alisema kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo imeanza kutoa elimu ya Kodi kwa wananchi ikiwemo ugawaji wa vipeperushi vyenye kufafanua kodi mbalimbali zinazotozwa na Manispaa zikiwemo zile za Sevice Levy, Leseni za vileo na Biashara.

Alisema kuwa tayari vipeperushi vimeanza kusambazwa katika Kata zote za Manispaa na sehemu mbalimbali zenye mikusanyiko ili watu waweze kupata elimu hiyo ya kodi.

"Ili kuonyesha umakini katika hili la elimu kuhusu kodi nanyi waandishi wa habari nitawagawia vipeperushi hivyo vya elimu ya kodi hi leo Ili mkawe mabalozi wazuri katika kuhabarisha Umma wa Watanzania" Alisema Kayombo.

Mkurugenzi kayombo alisema kuwa Manispaa ya Ubungo inatengeneza mabango maalumu ambayo yatasimikwa maeneo mbalimbali yakielezea baadhi ya kodi zinazotozwa, sambamba na mpangp wa kufanya ufuatiliaji wa mara kwa mara kwenye ukusanyaji wa mapato.

Sambamba na hayo pia Mkurugenzi Kayombo aliwaeleza waandishi wa habari kuwa Manispaa hiyo imeanza kutoa mafunzo ya siku nne kwa Wenyeviti, na Watendaji wa Kata na Mitaa ili kuwajengea uelewa juu ya matumizi mazuri ya fedha ambazo zinapelekwa kwao katika kutekeleza miradi ya maendeleo.

Alisema kuwa Kwa bajeti inayoisha kabla ya Mwezi wa saba zimepelekwa Bilioni 1.8 katika Kila Kata kwa ajili ya kutengeneza Barabara zote ambazo ziliharibika kipindi cha Mvua na wasimamizi wakuu ni viongozi hao.

IMETOLEWA NA:
KITENGO CHA HABARI NA UHUSIANO
HALMASHAURI YA MANISPAA YA UBUNGO