LIVERPOOL YAMNG'OA WINGA MOHAMED SALAH KUTOKA ROMA


Liverpool imekamilisha usajili wa paundi milioni 34 na kunasa saini ya mchezaji wa Roma aliyewahi kuichezea Chelsea winga Mohamed Salah.

Mchezaji huyo raia wa Misri mwenye umri wa miaka, 25, aliyemwaga wino kuitumikia Liverpool kwa mkataba wa miaka mitano amekuwa akiwindwa mno na kocha Jurgen Klopp.

Salah alikaribia kutua Liverpool akitokea timu ya Basle mwaka 2014 kabla ya kuamua kwenda Chelsea.
                          Mohamed Salah akionyesha jezi yake aliyokabidhiwa na Liverpool 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni