POLISI MUASI ASHUSHA MAKOMBORA KATIKA JENGO LA MAHAKAMA KUU

Mahakama ya Kuu ya Venezuela imeshambuliwa kwa mabomu yaliyodondoshwa na helkopta katika kile rais wa nchi hiyo Nicolás Maduro alichokiita kuwa ni shambulizi la kigaidi.

Picha zilizowekwa kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha helkopta ya polisi ikizunguka angani kabla ya kuachia mabomu na kusikika mlipuko mkubwa, kitendo kilichofanywa na polisi.

Afisa wa polisi anayesemekana kuiba helkopta hiyo, alitoa taarifa akiishutumu serikali kwa kuiita kuwa ni ya kihalifu. Rais Maduro amekuwa akikabiliwa na maandamano ya umma.
Polisi wa Venezuela wakiwa wamelizingira jengo la Mahakama Kuu baada ya kulipuliwa mabomu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni