DAWASCO YABAINI WIZI WA MAJI KIWANDA CHA BAHARI CHEMICALS LTD

Moja ya kisima kinachodaiwa kutumika kuhifadhi maji yanayodaiwa kuibwa kutoka katika mtandao wa maji wa Dawasco.
Madumu ya Maji ambayo yame3kuwa yakitumika katka utengezaji wa maji ya Betri katika kiwanda cha Bahari Chemicals  Ltd . 
Sehemu ya wizi wa maji kutoka katika mtandao wa DAWASCO unavyoone3kana kufanywa katika kiwanda cha kutengenezea Betri cha Bahari Chemicals Ltd.

Ikiwa siku chache tu zimepita baada ya shirika la Majisafi na Majitaka Dar es salaam (Dawasco) kubaini wizi mkubwa wa Maji kutumika katika shamba la mboga mboga na matunda katika chuo cha Islamic kilichopo Boko ununio jijini Dar es salaam. Dawasco imebaini wizi mwingine wa Maji katika kiwanda cha kutengeneza Maji ya betri cha Bahari Chemicals Ltd kilichopo kurasini wilaya ya Temeke jijini Dar es salaam.

Akizungumzia tukio hilo meneja wa Dawasco Temeke, Bw. Deogratius Rwegasira, amethibitisha kutokea kwa wizi huo ambapo kiwanda hicho kilikuwa kimejiunganishia Maji bila kibali cha Dawasco na kwamba hawakuwa na mita wala akaunti namba inayoonyesha kiasi cha Maji kinachopita katika system ya Maji iliyopo, na baada ya kufanya mawasiliano na Mkurugenzi wa kiwanda hicho Bw.Devendra Singh Parmar amekiri kutumia Maji hayo kinyume na taratibu .

“Baada ya kufanya uchunguzi tumebaini kuwa kiwanda hiki kimekuwa kikituibia Maji yetu kwa muda mrefu, mmiliki wa kiwanda amekubali kosa,lakini akisema kwamba wenyewe ni wageni hapa hawana zaidi ya mwaka mmoja tangu waanze kazi.hivyo hawakujua taratibu za kufuata”. Alisema Bw. Rwegasira.

Aidha meneja wa kiwanda hicho, Bw. Abdul Gulam, amekiri kuihujumu Dawasco kwa kuiibia Maji, lakini amesema kuwa wao ni wapangaji tu wamepanga katika eneo hilo na wana muda wa miezi saba tangu wahamie kiwandani hapo, walikuta wizi huo wa Maji ukifanyika katika kiwanda hicho   na hawakujua taratibu husika za kufuata ili wapate huduma ya Maji kihalali.

“Sisi tumekubali kuwa tulikuwa tunatumia Maji ya DAWASCO bila kuyalipia, lakini sio sisi ambao tuliounganisha bomba hili, wapangaji waliopita walijiunganishia Maji haya hivyo tunaomba tulimalize hili, ili tuanze kuwa wateja wenu rasmi” alisema Bw.Gulam.

Aidha bwn Gulam ameainisha kuwa wao kama wamiliki wa kiwanda wamekubali kulipa faini iliyotolewa na DAWASCO ya Shiling million 3.5 ili warudishiwe huduma kama wateja wengine na waweze kuendelea na biashara.

Vitendo vya uhujumu wa Miundombinu ya Maji hususani wizi wa Maji unaendelea kuwa changamoto kwa DAWASCO licha ya kampeni na elimu inayotolewa kila siku juu ya uhalali na utaratibu wa kuungiwa huduma ya Maji inayotolewa na DAWASCO.

Imeandaliwa na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii.

JAMES KATORO AWASHUKURU WAKAZI WA KATA YA KAYENZE MANISPAA YA ILEMELA KWA MAAMUZI YAO


Wazee wakimsimika James Katoro baada ya kuchaguliwa kuwa Diwani wa Kata ya Kayenze katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza.

Na:George Binagi-GB Pazzo @BMG 



Katoro alichaguliwa kuwa diwani wa Kata hiyo katika uchaguzi uliofanyika Novemba 25,2015 kupitia Chama cha Mapinduzi CCM. Tukio hili limejiri jana katika Mkutano wa hadhara wa CCM kuwashukuru wakazi wa Kata hiyo kwa kumchagua Katoro kuwa diwani wa Kata hiyo.
Wazee wakimsimika James Katoro baada ya kuchaguliwa kuwa Diwani wa Kata ya Kayenze katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza. 
Mchungaji Elias Lutalamamila (wa pili kulia) kwa niaba ya viongozi wa dini akimsimika James Katoro baada ya kuchaguliwa kuwa Diwani wa Kata ya Kayenze katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza. 
Diwani wa Kata ya Kayenze Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza James Katoro (CCM) akihutubia katika mkutano wa kuwashukuru wakazi wa Kata hiyo kwa kumchagua kuwa diwani wao. Aliahidi kushughulikia kero mbalimbali zilizo katika Kata hiyo ambazo ni pamoja na kero ya maji, ujenzi wa zahanati na vituo vya afya, miundombinu pamoja na ujenzi wa shule za msingi na Sekondari.
Salum Abdallah Said ambae ni Mwenyekiti wa CCM Kata ya Kayenze akizungumza katika mkutano wa chama hicho wa kuwashukuru wakazi wa Kata hiyo kwa ushindi waliokipa chama hicho katika uchaguzi uliofanyika Novemba 25,20515.
Kulia ni Jeremiah Mtoni ambae ni Katibu wa CCM Kata ya Kayenze akizungumza katika mkutano wa chama hicho wa kuwashukuru wakazi wa Kata hiyo kwa ushindi waliokipa chama hicho katika uchaguzi uliofanyika Novemba 25,20515.
Elias Makaranga (mwenye kinasa sauti) ambae alikuwa Meneja Kampeni wa Diwani Katoro katika uchaguzi uliopita akizungumza jambo katika mkutano wa kuwashukuru wananchi uliofanyika jana.
Wakazi wa Kata ya Kayenze wakifuatilia Mkutano wa Chama cha Mapinduzi CCM katika Kata hiyo wa kuwashukuru kwa kukichagua chama hicho katika uchaguzi uliofanyika Novemba 25, mwaka jana.

JANET MWENDA NA MARAFIKI ZAKE WA "MENTORING AND NETWORKING" WATOA MSAADA KWA KITUO CHA WATOTO WETU TANZANIA


Bi. Janet Sosthenes Mwenda (wa pili kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi wa kituo cha Watoto Wetu Tanzania, Bw. Evans Tegete moja ya vitu vilivyowasilishwa kwenye kituo hicho ndoo ya sabuni ya unga. Kushoto ni Muhamasishaji na mchangishaji fedha wa “Mentoring and Networking”, Bi. Mary Sanga na wengine wanaoshuhudia ni watoto wa kituo hicho. (Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog).

Mmiliki na Mwendeshaji wa kipindi cha ‘Ongea na Janet’ Bi. Janet Sosthenes Mwenda ambaye pia ni mmiliki wa programu maalum ya vipindi vya watoto katika kutoa elimu katika televisheni kiitwacho ‘Tuwalinde Watoto Wetu’ kwa kushirikiana na marafiki zake wa kundi la “Mentoring and Networking” kupitia mitandao ya kijamii wametoa misaada mbalimbali ya vyakula na vinywaji kwa kituo cha Watoto Wetu Tanzania.

Akizungumza wakati wa kutoa misaada hiyo mapema jana 17 Januari, wakati wa tukio hilo lililofanyika kwenye kituo hicho kilichopo Kimara jijini Dar es Salaam, Janet Mwenda ambaye aliambatana na baadhi ya marafiki zake hao wa “Mentoring and Networking” wameweza kutoa misaada hiyo ya vyakula, vinywaji ambavyo vitasaidia kituo hicho.
“Kwa kuja hapa kutoa msaada huu ni kutokana na kuguswa na hali ya watoto wanaolelewa hapa na kwingineko kote. Naamini msaada huu utasaidia watoto wetu hapa kituoni naamini kwa hiki kidogo kitasaidia kwa siku kadhaa” alieleza Janet Mwenda.
Janet Mwenda ameongeza kuwa, amekuwa akifikiria zaidi kutoa misaada hivyo kufika hapo ni kutokana na kuguswa kwake kwa muda mrefu na amekuwa pia akitembelea kituo hicho kipindi cha nyuma hivyo kuwa miongoni mwa wanafamilia.
Kwa upande wake Muhamasishaji na mchangishaji fedha wa “Mentoring and Networking”, Bi. Mary Sanga ambaye aliambatana na Janet Mwenda katika kituo hicho ametoa wito kwa jamii kujitokeza kusaidia watoto wanaolelewa kwenye vituo kama hivyo na kuchangia chochote walicho nacho.
Pia amepongeza watu mbalimbali kwa kuguswa na hali ya watoto wanaolelewa kwenye vituo hivyo ameomba waendelee kujitokeza zaidi pindi wanapoguswa na masuala ya kusaidia jamii isiyo jiweza.
Naye Mkurugenzi wa kituo hicho, Ndugu Evans Tegete akitoa neno la shukrani mara baada ya kupokea msaada huo ambapo alishukuru kwa kuguswa kwa Janet Mwenda na marafiki zake kwani hadi sasa kituo hicho hakina Mfadhili wa kudumu zaidi wakitegemea kuendesha kituo kwa michango ya misaada ya watu mbalimbali wanaofika kituoni hapo.
“Tunashukuru kwa msaada huu. Kwani ni mkubwa sana na utasaidia kuendesha kwa siku kadhaa ndani ya kituo chetu. Kituo chetu kwa sasa tuna watoto na vijana zaidi ya 89 wakiwemo wale wanaosoma shule za Bweni na wa kutwa ambao wapo hapa kituoni.” Alieleza Mkurugenzi huyo.
Pia alieleza kuwa changamoto mbalimbali zinawakabili ikiwemo suala la ada za shule kwa watoto na vijana waliochini ya kituo hicho.
Kituo hicho kinacholea Watoto na vijana wa mitaani na wanaoishi katika mazingira magumu kina jumla ya watoto pamoja na vijana 120 kilianzishwa mnamo mwaka 1998 Kwa lengo la kuwasaidia watoto waliokosa malezi na huduma mbalimbali za kijamii. Kituo hicho kinapatikana Kimara Suka pamoja na Kijiji cha Mazizini Msata wilayani Bagamaoyo kinakabiliwa na changamoto mbalimbali hivyo uongozi wa kituo hicho kinawaomba watu binafsi na wafadhili mbalimbali kujitokeza kuwasaidia pindi waguswapo.
Mkurugenzi wa kituo cha Watoto Wetu Tanzania, Bw. Evans Tegete akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) wakati wa utambulisho wa kituo hicho.
Bi. Janet Sosthenes Mwenda (kushoto) akipata fursa ya kuwa na watoto wanaolelewa kwenye kituo hocho cha Watoto Wetu Tanzania, kulia kwake ni Mary Sanga kutoka kundi la marafiki wa “Mentoring and Networking”.
Muhamasishaji na mchangishaji fedha wa “Mentoring and Networking”, Bi. Mary Sanga akitoa nasaha na kushukuru wale wote walioguswa kwa kuchangia mpango huo.
Bi. Janet Sosthenes Mwenda akipata fursa ya kuwa na watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho cha Watoto Wetu Tanzania.
Bi. Janet Sosthenes Mwenda akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) ambapo ameiomba jamii kuwa na tabia ya kusaidia jamii isiyojiweza ikiwemo watoto wanaolelewa kwenye vituo.
Binti Cecilia Sospita anayelelewa kwenye kituo hicho cha Watoto Wetu Tanzania, akishukuru kwa niaba ya watoto wenzake wanaolelewa kituoni hapo kwa msaada uliowasilishwa na Bi. Janet Mwenda.
Msaada uliotolewa kusaidia kituoni hapo.
Kijana Samson Furgence akishukuru kwa niaba ya watoto wenzake wa kituo hicho.
Zoezi la utoaji wa zawadi likiendelea.
Watoto na vijana wanaolelewa katika kituo hicho. Wengine ni wageni wa kujitolea "Volunteer" wa kituo hicho kutoka nchini Ujerumani wakiwa pamoja na watoto hao kituoni hapo.
Muhamasishaji na mchangishaji fedha wa “Mentoring and Networking”, Bi. Mary Sanga akitoa msaada katika tukio hilo.
Baadhi ya watoto na walezi wao wakifuatilia shughuli hiyo.
Janet Mwenda akishukuru watu mbalimbali kwa kumtia moyo katika kufanikisha shughuli hiyo.
Baadhi ya watoto hao.
Baadhi ya watoto hao.
Sala maalum ya kuombea vitu hivyo vilivyoletwa kituoni hapo pamoja na Baraka kwa waliofanikisha ikitolea na mmoja wa watoto wa kituo hicho.

HAKUNA ATAKAYEBOMOLEWA NYUMBA ALIYEJENGA KATIKA UMBALI UNAORUHUSIWA KISHERIA -KALUA

Na Skolastika Tweneshe-MAELEZO
Mbunge wa Jimbo la Segerea kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Mh. Bonna Kalua amesema kuwa hakuna nyumba ya mwananchi itakayobomolewa ambayo imejengwa katika umbali unaohitaji
kisheria wa mita 60 kutoka mtoni.
Mh.Kalua alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es salaam wakati akizungumza na wananchi wa Karakata kwenye mkutano wa hadhara.
Aidha alitoa wito kwa wale ambao wamejenga ndani ya mita 60 na nyumba zao zimewekewa X kujiorodhesha majina yao kwa wenyeviti wa mitaa ili wamfikishiea Ofisi kwake kwa ajili ya kulifuatilia jambo hilo kwa ukaribu na hatimaye wapate haki zao.
Mh.Bonna aliwatahadharisha wananchi kutodanganywa na watu wanaowachangisha fedha kwa kigezo cha kufungua kesi mahakamani kuwa ni uongo na hawana nia nzuri kwa wananchi kwa sababu kesi ya bomoa bomoa tayari ilishafunguliwa kwa niaba ya nchi nzima.
Aliwataka wananchi kuwa wavumilivu mpaka hapo shauri lilipo mahakamani litakapotolewa tamko .

SERIKALI YALIFUTA GAZETI LA MAWIO

nape1
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye (mwenye suti ya kijivu) akiwaeleza Waandishi wa Habari (hawapo pichani) juu ya Uamuzi wa Serikali wa kulifuta Gazeti la MAWIO katika Daftari la Msajili wa Magazeti mara alipokutana na waandishi hao 17 Januari 2016 katika Ukumbi wa Idara ya Habari uliopo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari, Bw. Assah Mwambene, wa pili kulia ni Mkurugenzi Msaidizi anayeshughulikia usajili wa Magazeti, Bw. Raphael Hokororo na anayemfuatia ni Mwanasheria wa Wizara Bw. Patrick Kipangula
nape2
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakifuatilia taarifa ya Serikali toka kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye (hayupo pichani) juu ya Uamuzi wa Serikali wa kulifuta Gazeti la MAWIO katika Daftari la Msajili wa Magazeti mara alipokutana na waandishi hao 17 Januari 2016 katika Ukumbi wa Idara ya Habari uliopo jijini Dar es Salaam.
 
(PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-MAELEZO)
………………………………………………………………………………………………..
Na Benedict Liwenga-Maelezo.
 
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeamua kulifuta kutoka katika Daftari la usajili wa magazeti, gazeti lijulikanalo kama “MAWIO”.
 
Amri ya kulifuta Gazeti hilo imetolewa leo na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye wakati alipokutana na Waandishi wa Habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) uliopo Jijini Dar es Salaam.
 
Mhe. Nnauye amesema kuwa kupitia Tangazo la Serikali Na. 55 lililotolewa tarehe 15 Januari, 2016 Serikali imelifuta Gazeti hilo ikiwa ni uamuzi uliotolewa kwa mujibu wa Sheria ya Magazeti Sura ya 229, kifungu 25(1).
 
Alieleza kuwa, hatua ya kulifuta gazeti hilo inazuia pia gazeti la Mawio kuchapishwa katika njia nyingine yoyote ikiwa ni pamoja na mitandao (Online publication) kwa mujibu wa Sheria ya Mawasiliano ya Kieletroniki na Posta Sura ya 306.
 
‘’Serikali kwa masikitiko makubwa, imechukua uamuzi huu kutokana na mwenendo wa uandishi wa gazeti hilo usioridhisha wa kuandika na kuchapisha habari zenye mwelekeo wa uchochezi na kuhatarisha amani, utulivu na usalama wa nchi yetu’’, alisema Nnauye.
 
Aidha, alifafanua kuwa hatua hiyo ya kulifuta gazeti hilo imechukuliwa baada ya Msajili wa Magazeti kufanya juhudi kubwa za muda mrefu kuanzia Juni, 2013 hadi Januari,  2016  kumtaka Mhariri wa gazeti hilo kubadili aina ya uandishi wa habari na makala katika gazeti lake, bila mafanikio.
 
‘’Msajili wa magazeti kwa juhudi zake alifanya mawasiliano na Mhariri wa gazeti hilo mara nane kwa lengo la kutaka afanye marekebisho ya  mtindo wa kutoa habari zake lakini mhariri wa gazeti hilo hakuzingatia ushauri mzuri aliopewa na Msajili wa Magazeti,
Ninatoa wito kwa wamiliki, wahariri, waandishi na watangazaji wa habari kuzingatia sheria, Kanuni na taratibu za taaluma ya uandishi wa habari ambazo zikizingatiwa hakutakuwa na migogoro yoyote. Aidha Serikali inasisitiza kwamba inaheshimu uhuru wa vyombo vya habari unaozingatia maadili, weledi na Sheria za nchi na kwamba Serikali itaendelea kushirikiana navyo’’ alisisitiza Mhe. Nnauye.
 
Katika hatua nyingine, Waziri nape alitoa pongezi kwa Vyombo vyote vya habari nchini vinavyozingatia maadili, weledi na Sheria zinazosimamia taaluma ya habari na sheria nyingine za nchi. 
 
‘’Kwa namna ya pekee Serikali inawapongeza wamiliki na wahariri wa vyombo vya habari ambavyo vinapofanya makosa vikielekezwa hujirekebisha na kutoa ushirikiano kwa Serikali na pia kubadili mwenendo wao; hawa ni pamoja  na wahariri wa magazeti ya; Mwananchi Tanzania, Mtanzania, The East African, Magazeti ya Daily News na Habari Leo, Uhuru na mengineyo’’, alisema Mhe. Nnauye.

Nape akutana na Balozi wa Israel nchini na kukubaliana kushirikiana katika sekta za Habari na Utamaduni

pe1
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye(kulia) akifurahia jambo na Balozi wa Israel nchini Tanzania Bw.Yahel Vilan alipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam.Katika maongezo yao wamekubaliana kuimarisha ushirikiano uliokuwepo na kuangalia sehemu zaidi za kushirikiana katika sekta za Habari na Utamaduni.
pe2
Balozi wa Israel nchini Tanzania Bw.Yahel Vilan(kushoto) akimpongeza Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe,Nape Nnauye(kulia) kwa kuchaguliwa kuwa Waziri  pamoja na kumpatia zawadi ya kitabu na kikombe kutoka Israel alipomtembelea leo jijini Dar es Salaam.
pe3
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe,Nape Nnauye(kushoto) akimkaribisha ofisini kwake Balozi wa Israel nchini Tanzania Bw.Yahel Vilan(kulia) alipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

WAZIRI NAPE:HONGERA SANA BWANA MICHUZI KWA KUWA MWENYEKITI WA FK


mwenyekiti
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye (mwenye suti ya kijivu) akimpongeza mwenyekiti mpya wa FK aliyeteuliwa hivi karibuni Bw. Ahmed Michuzi ambaye pia ni Mmiliki  wa Blogu ya Jiachie na mkurugenzi mwandamzi  wa Michuzi  Michuzi Media alikuwa mwanachama mwaminifu wa FK, tukio hilo limetokea leo wakati alipokutana naye kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo  jijini Dar es salaam, Cheo hicho kilikuwa kikishikiliwa na Kamanda Richard Mwaikenda.

WALIONYIMWA HIFADHI YA UKIMBIZI NCHINI KENYA KUREJESHWA BURUNDI JANUARY 16


ARUSHAMahmoud Ahmad Arusha
…………………………………….
IDARA ya Uhamiaji mkoa wa Arusha, January 16 inawarejesha kwenye kambi ya wakimbizi raia wa Burundi 21 ,akiwemo mwanamke mtanzania,walionyimwa hadhi ya ukimbizi nchini Kenya..
Afisa Uhamiaji mkoa wa Arusha, Ndelema Mwakipesile, alisema hayo ofisini kwake kuwa wakimbizi hao akiwemo mwanamke mtanzania ambae ameolewa na raia wa Burundi, walikataliwa kuingia nchini Kenya kutokana na kutokuwa na sifa za ukimbizi.
Mwakipesile,alisema raia hao wa Burundi, waliingia nchini wakipitia mpaka wa Kabanga uliopo mkoani Kigoma na kudai wamekuja kuwatembelea ndugu zao lakini mara baada ya kuingia nchini walibadirisha mawazo na kuamua kwenda nchini Kenya kutafuta hifadhi kwenye kambi ya Kakuma nchini Kenya.
Raia hao 21 wakiwemo watoto 14 walipofika mpakani Namanga wakitaka kuingia nchini humo walidai wanatafuta hifadhi ya ukimbizi na serikali ya Kenya iliwazuia na kuwarejesha Tanzania ,ambako ndiko walikopitia kuelekea Kenya.
Mwakipesile, alisema cha kushangaza raia hao wa Burundi kila mmoja ana hati ya kusafiria jambo ambalo linaonyesha walikuwa wamejiandaa kwa kuwa sheria za kimataifa za ukimbizi haziruhusu mkimbizi kuwa na hati bali mkimbizi anakuwa na vitu vichache tu pia mkimbizi hachagui kambi ya kupelekwa .
Alisema walipoulizwa kulikoni waende Kenya, wakimbizi wamesema kuwa wamekuwa wakiingia nchini mara kwa mara kwenye kambi ya wakimbizi ya Kibondo,na wamekuwa wakirejeshwa kwao mara kwa mara wanapoingia nchini.
Mwakipesile, alisema wakimbizi hao hataki kurejeshwa kwao sasa wamebadirisha mawazo na kuamua kutafuta hifadhi nchini Kenya ili kukwepa kurejeshwa kwao.
Alisema wanarejeshwa makwao kwa kuwa hawana kosa lolote kwa mjuibu wa taratibu za kimataifa hivyo watapelekwa kwenye kambi ya wakimbizi ya Kibondo, ili wasubiri taratibu zingine .
Mwakipesile alisema kulingana na sheria mkimbizi hawezi kuomba nchi ya kwenda, pia haruhusiwi kwenda nchi ya tatu kutoka kwao bali anatakiwa kukimbilia nchi wanayopakana nayo
Raia hao wa Burundi, walikutwa ndani ya Basi la Tahmeed Coach, lililokuwa likitokea Dar es Salaam kwenda Nairobi nchini Kenya na walipofika mpaka wa Namanga, wakazuiliwa kuingia nchini Kenya .
Rai mmoja wa Burundi,ambae hakutaka jina lake liandikwe kwa sababu ya usalama ,ambae ni dereva wa malori,amesema wamekuwa wakiingia nchini mara kwa mara kwenye kambi ya wakimbizi na wamekuwa wakirejeshwa kwao sasa wanataka kwenda kuishi kwenye kambi iliyo mbali na kwao kwa kuhofia usalama wao.
Alisema mwezi Desemba mwaka jana akiwa nyumbani kwake nchini Burundi,watu watatu waliuliwa mbele ya nyumba yake na watoto wake wamekuwa wakiogopa kuishi kutokana na kutokuwepo amani nchini mwao na hiyo ni sababu ya msingi ya kuomba ukimbizi.
Alisema kuwa yeye amekuwa ni dereva wa malori kwa miaka 20 amekuwa akisafirisha mizigo kata ya Tanzania na Burundi, lakini kutokana na ukosefu amani nchini mwao ameamua kikimbia kutafuta hadhi ya ukimbizi nchini Kenya.
Alisema Tanzania anaipapenda tatizo ni kuwa Tanzania imekuwa ikiwarudisha mara kwa mara nchini Burundi hivyo wanaomba kwenda nchi ya mbali ili wasirudishwee mwakwao.
Ameongeza kuwa maafisa wa Burundi wamekuwa wakienda kwenye kambi ya wakimbizi na kuwatambua na kasha huuliwa hivyo wanahofia usalama wao.
Kwa upande wake Mtanzania aliyeolewa na raia huyo wa Burundi, Eva Michael Magumula,(37) mzaliwa wa Dodoma, alisema ana watoto 6 inalazimika aambatane na mume wake ili waweze kulea familia yao.

T.I.B YAKUBALI KUTOA FEDHA UJENZI WA HOSPITALI ARUSHA


ARUSHANa Mahmoud Ahmad Arusha
………………………………………
BENKI ya uwekezaji nchini TIB, imekubali kutoa shilingi bilioni 31 kugharimia ujenzi wa hospital ya rufaa ya mkoa wa Arusha, ambayo itajengwa kwenye eneo la hospital ya mkoa ya Mount Meru mapema mwaka huu.
Mkuu wa mkoa wa Arusha, Felix Ntibenda, amesema kuwa tayari taratibu za kupatikana kwa fedha hizo ambazo ni mkopo zimekamilika na hivi karibuni kutasainiwa mkataba kati ya benki hiyo na ofisi ya katibu tawala mkoa ili ujenzi huo uweze kuanza mara moja.
Ntibenda, amesema mkoa unaendelea wa kuboresha,majengo na huduma ya afya kwenye hospital hiyo ya mkoa wakati wakisubiri hospital ya rufaa ijengwe.
Amesema,ukarabati wa hospital hiyo unaofanywa kwa kushirikiana na wadau umewezesha kuirejesha hadhi ya hospital hiyo.
Amesema kuwa mkoa umewezesha kuanzishwa kwa bohari la dawa la MSD,ambalo tayari maandalizi yamefikia 95% na itafunguliwa wakati wowote na kuanza kutoa huduma za dawa kwa bei nafuu zaidi kuliko zinavyouzwa kwenye maduka binafsi.
Kwa upande wake,Katibu tawala mkoa wa Arusha, Adoh Mapunda, amesema kuwa wiki ijayo mkoa utasaini makubaliano ya kupatiwa mkopo na benki hiyo na kufuatiwa na hatua ya kutangaza zabuni ili kumpata mkandarasi atakae jenga hospital hiyo yenye majengo ya ghorofa tano ya hospital hiyo ya rufaa.
Amewapongeza wadau ambao wamejitokeza kuchangia ukarabati wa hospital hiyo ya mkoa unaoendelea na tayari jengo la wadi ya Grade one ,ambalo lilikuwa likihudumia kulaza wagonjwa katika hospital hiyo ya mkoa limefungwa likisubiri kubomolewa kutokana na uchakavu.
Akiwasilisha mpango kazi na mchoro wa jengo hilo, Mhandisi wa mkoa, Edward Amboka ,amesema kuwa hospital hiyo iliyojengwa mwaka 1915 majengo yake yamechakaa sana na hayafai kuendelea kutumika kama hospital .
Hospital hiyo ilijengwa ikiwa ni kambi ya kutibia majeruhi wa vita ya kwanza ya dunia hivyo mpango uliopo ni kujenga majengo mapya ya ghorofa na kubomoa ya zamani ambayo yamechakaa.
Amesema ujenzi huo utahusisha maeneo manane zikiwemo nyumba za watumishi ,mafunzo, mapumziko na maegesho ya magari.na mipango mingine ya uendelezaji wa hospitali hiyo
Amesema lengo la kujenga majengo hayo ni kupunguza mzigo wa wagonjwa mkoani Arusha ikiwemo vizazi na vifo vinavyotokana wakati wa kujifungua hivyo wanajenga jengo moja la ghorofa tano ambalo litatosheleza mahitaji badala ya kuwa na utitiri wa majengo
Kwa upande wake mganga mfawidhi wa hospital hiyo, Dakta Jacklin Urio, amesema hospital hiyo ina vitanda 500 na ina hudumia watu milioni 1.6 kwa mwaka lakini kutokana na ukuaji wa mji na ongezeko la watu hospital hiyo kwa sasa haitoshelezi mahitaji kutokana na wingi wa watu.
Amesema kuwa ujenzi wa hospital mpya ya rufaa utaiwezesha hospital ya rufaa kuwa na vitanda 600 ,kutakuwa ni vitanda 50 kwa ajili ya wagonjwa mahututi, ICU, na kati yake vitatu ni kwa ajili ya watu maalumu (VIP) wakiwemo viongozi wa kitaifa na kimataifa .
Jengo la Grade A,lilikuwa na vitanda 6,lakini kwa sasa halikidhi mahitaji na jengo jipya litakuwa na maabara ,wataalam, vitanda 50 vya wagonjwa wa Mahututi,(ICU) na huduma zingine .

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Atembelea Idara ya Uhamiaji Zanzibar.


Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe Hamad Masauni, akisalimiana na Maofisa wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar wakati wa ziara yake kutembelea Idara hiyo ya Uhamiaji Zanzibar.kushoto Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe Hamad Masauni, akisalimiana na Maofisa wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar wakati wa ziara yake kutembelea Idara hiyo ya Uhamiaji Zanzibar.Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe Hamad Yussuf Masauni akipata maelezo kutoka kwa Afisi wa Uhamiaji Zanzibar wakati wa ziara yake katika Idara ya Uhamiaji Zanzibar. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Tanzania Mhe Hamad Yussuf Masauni akitembelea Vitengo vya Idara ya Uhamiaji Zanzibar wakati wa ziara yake na kuangalia Utendaji wa Idara hiyo Zanzibar.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani akimsikiliza Afisa Uhamiaji Zanzibar akitowa maelezo ya jinsi ya kuweka kumbukumbu za Passport wakati wa ziara yake.
Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar akitowa maelezo kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe Hamad Yussuf Masauni, wakati wa ziara yake katika Idara hiyo Zanzibar. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Tanzania Mhe Hamad Yussuf Masauni akizungumza na Maofisa wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar baada ya ziara yake ya kujitambulisha na kuangalia ufanisi wa kazi za Idara hiyo Zanzibar.
Maofisa wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar wakimsikiliza Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe Eng Hamad Yussuf Masauni akizungumza na Maofisa hao baada ya ziara yake kutembelea Idara hiyo kuina ufanisi wa Kazi zake kwa Wananchi wanaofika kupata Passport.
Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot
Zanzinews.com

WAZIRI MBARAWA AWATAKA MAKANDARASI MKOANI MTWARA KUKAMILISHA MIRADI YA UJENZI WA BARABARA KWA WAKATI.


Z1
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,Profesa Makame Mbarawa akiweka saini kwenye kitabu cha kumbukumbu mara alipowasili Mkoani Lindi kwa Ziara ya Kukagua miradi inayotekelezwa na Wizara hiyo.Kulia ni ni Bi.Mariam Mtima Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa.
Z2
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,Profesa Makame Mbarawa akipokea taarifa ya Ujenzi wa barabara ya Mangaka-Mtambaswala (KM 62.7), kutoka kwa Mhandisi Mkazi Anold Msengezi (Katikati) anayesimamia ujenzi wa barabara hiyo.
Z3
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo juu ya Ujenzi wa barabara ya Mangaka-Mtambaswala (KM 62.7), ambapo amemtaka Mkandarasi kukamilisha Ujenzi huo kwa wakati na ubora unaokusudiwa.
Z4
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (Wa kwanza kulia) akipokea taarifa ya Ujenzi wa barabara ya Mangaka –Nakapanya (KM70.5) kutoka kwa Mhandisi mkazi Dkt.Chaurasia inayojengwa na kampuni ya Jiangxi Geo Engineering (Group) Cooperation ya China.
Z5
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akisalimiana na wakazi wa Nakapanya alipopita kukagua bujenzi wa barabara ya Mangaka-Mtambaswala (KM 62.5).
Z6
Sehemu ya barabara ya Mangaka –Mtambaswala (KM 62.5) ambayo Ujenzi wake unaendelea kwa kiwango cha lami.
Z7
Tingatinga likiwa linaendela na kazi za ujenzi barabara ya Mangaka –Mtambaswala (KM 62.5) ambayo Ujenzi wake unaendelea kwa kiwango cha lami.
…………………………………………………………………………
Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amewataka makandarasi wanaojenga barabara za Mangaka-Mtambaswala KM 62.7 na Mangaka-Nakapanya Km 70,5 kukamilisha ujenzi huo ifikapo Juni mwaka huu.
Amewataka makandarasi hao kuongeza rasilimali watu na vifaa ili ujenzi huo ukamilike kama ilivyopangwa katika mkataba wa ujenzi wake.
“Hakuna muda utakaoongezwa nataka miradi yote miwili iwe imekamilika ifikapo juni mwaka huu tena iwe kwenye ubora unaowiana na thamani ya fedha,”amesema Waziri Prof. Mbarawa.
Barabara hizo ambazo ujenzi wake kwa kiwango cha lami ulianza mwaka 2014 zitafungua fursa za kiuchumi mkoani Mtwara ikiwemo kuiunganisha Tanzania na Msumbiji kwa lami kupitia daraja la umoja lililoko Mtambaswala.
Akizungumza katika ziara hiyo Meneja wa Wakala wa Barabara TANROADS mkoa wa Mtwara Eng. AISHA SALIM amesema hawata kubali maombi yoyote ya kuongeza muda wa ujenzi wa barabara hizo ambapo ujenzi wa barabara ya Mangaka –Mtambaswala Km 62.7 unatarajiwa kukamilika mwezi Mei na ule wa Mangaka-Nakapanya KM 70.5 ukitarajiwa kukamilika mwezi julai mwaka huu.
Mapema Prof. Mbarawa alikagua hali ya barabara wilayani Ruangwa,Nachingwea na Masasi na kusisitiza kuwa ujenzi wa barabara na madaraja katika wilaya hizo utaendelea katika kipindi kifupi baada ya Serikali kuanza kutoa fedha kwa miradi inayotumia fedha za Mfuko wa Barabara (RFB).
Waziri Mbarawa yuko katika ziara ya mikoa ya lindi na mtwara kukagua miradi ya Barabara,Mawasiliano na Bandari ili kuona ufanisi uliopo katika sekta hizo.
Imetolewa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano