DC ATOA WIKI MBILI WANAFUNZI WAENDE SHULE



Na Mahmoud Ahmad
Mkuu wa Wilaya ya SimanjiroMkoani Manyara, Mahmoud Kambona ameagiza
wanafunzi wote waliofaulu kujiunga nashule za sekondari wilayani humo
wawe wamewasili kwenye shule zao na kuanzamasomo baada ya wiki
mbili.Kambona alitoa agizo hilo juzialipokuwa anakagua shule ya
sekondari Msitu wa Tembo na kuzungumza na watendajiwa vijiji, kata,
madiwani na maofisa Tarafa, kuhusiana na wanafunzi waliofaulukujiunga
na masomo ya sekondari. Alisema wanafunzi wote waliofaulukujiunga na
sekondari wanatakiwa wafike kwenye shule zao baada ya muda wa
wikimbili kwa ajili ya masomo na endapo wasipotekeleza hilo
atawachukulia hatuakali viongozi wa eneo husika. “Nitawachukulia hatua
kali viongoziwote wakiwemo madiwani, maofisa tarafa, watendaji wa
kata, vijiji na wenyevitiwa vijiji wa sehemu husika ambao wanafunzi
wote waliofaulu watakuwa hawajafikashuleni,” alisema Kambona.Pia,
aliwaagiza wakuu wa shule zasekondari za wilaya hiyo kuwaelekeza
wazazi na walezi wa watoto ambao wamefaulukujiunga na shule zao, juu
ya majukumu yao na majukumu ya serikali kuhusiana naelimu bure.Baadhi
ya wazazi wa wanafunziwaliofaulu Joseph Odoyo na Mustafa Seif walisema
dhana ya elimu bure ya RaisJohn Magufuli bado hawajaielewa kwani
iliondolewa ni ada pekee ila chakula na mahitajimengine
wanachangia.“Ada ya sh20,000 ndiyo pekee iliyofutwaila tunachangia
huduma nyingine za mpishi sh15,000 kuni sh15,000 kusaga na
kukoboash15,000 kulima shamba la shule sh15,000 na viungo sh10,000 kwa
muhula mmoja,”alisema Odoyo.  Alisema pia wazazi wanatakiwa
kuchangiakilo 80 za mahindi, kilo 35 za maharage, kilo tano za sukari,
kilo 12 za mchelena lita tano za mafuta ya kula kwa muhula mmoja ila
sh5,000 ya muhuri wa nemboya shule imetolewa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni