DEONTAY WILDER ATETEA TAJI LAKE LA UZITO WA JUU KWA USHINDI WA KO

Bondia Deontay Wilder ametetea taji lake la uzito wa juu la kwa ushindi wa KO dhidi ya Artur Szpilka, huku Tyson Fury akivamia uliongoni kutaka pambano na bondi huyo Mmarekani.

Hii ni mara ya tatu kwa Wilder kutetea taji lake hilo, ingawa haikuwa rahisi safari hii ambapo alihangaika mno kuweza kumshinda Szpilka.

Hata hivyo ngumi kali ya kidevu aliyoirusha Wilder, ilitosha kumaliza pambano hilo na kumuacha bondia Szpilka akiwa chali na kulazimika kupatiwa msaa wa matibabu.
                         Bondia Szpilka akitupa ngumi ya kushoto iliyompata usoni Wilder
             Wilder akiachia kombora la ngumi ya kushoto iliyompeleka chini Szpilka
     Szpilka akiwa amelala chali na kupoteza fahamu baada ya kupigwa na Wilder
  Bondia Tyson Fury akimpiga mkwara Deontay Wilder na kutaka kuandaliwa pambano naye

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni