![]()  | 
| Meya wa Jiji la Arusha,Calist Lazaro akizungumza baada ya hafla kuweka saini makubaliano kati ya pande mbili. | 
![]()  | 
| Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Jiji la Arusha,Juma Idd akifafanua umuhimu wa ushirikiano kati ya Jiji na kampuni hiyo. | 
![]()  | 
| Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Jiji la Arusha,Juma Idd(kulia) akifafanua umuhimu wa ushirikiano kati ya Jiji na kampuni hiyo,kushoto ni Meya wa Jiji la Arusha,Calist Lazaro. | 
![]()  | 
| Diwani wa Kata ya Moshono ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mipango miji ya Jiji la Arusha,Metson Paul(kushoto) akiwa Mwanasheria na Mkurungezi wa kampuni ya Bondeni Seeds Limited. | 
![]()  | 
| Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini,Goodbless Lema akizungumza katika hafla hiyo. | 
Halmashauri
 ya Jiji la Arusha imesaini makubaliano na kampuni ya Bondeni Seeds 
Limited kupima eneo linalomilikiwa na kampuni hiyo lenye ukubwa wa 
Hekari 750 ili liwe sehemu ya Master Plan ya  Jiji .
Meya
 wa Jiji la Arusha,Calist Lazaro amesema wameshawishika kuingia 
makubaliano hayo na mwekezaji huyo ili kuwezesha wananchi kuishi kwenye 
maeneo yaliyopimwa yanayoendana na hadhi ya Jiji na kulipatia mapato 
yanayotokana naupimaji huo.
Mkurugenzi
 Mtendaji wa Halmashauri ya Jiji,Juma Idd amesema wamekubaliana na 
mwenye eneo hilo kulipanga na kuliendeleza kama sheria ya makazi 
inavyotaka.
"Hatutaweza
 kuendelea na makazi ambayo hayajapimwa kama Unga Limited ,Ngarenaro na 
mengine ,Arusha ni eneo lenye umuhimu wake katika sekta ya utalii,madini
 na ukizingatia hapa ndio Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika 
Mashariki(EAC) na taasisi za kimataifa.
Amesema baada ya kusaini makubaliano utekelezaji unaanza mara moja ili kufikia malengo ya kuweka mji uliopangika.
Mbunge
 wa Arusha Mjini,Goodbless Lema amewataka wananchi wenye maeneo makubwa 
kushirikiana na uongozi wa Jiji ili maeneo yao yapimwe kuepusha makazi 
holela na kuwataka waliojenga maeneo ya mabondeni na kwenye vyanzo vya 
maji kubomoa nyumba zao.







Hakuna maoni:
Chapisha Maoni