Baadhi ya
 wafanyakazi wa  Gazeti la Jambo Leo na familia zao, wakigongeana glasi 
zenye vinywaji ikiwa ni ishara ya kutakiana heri wakati wa hafla ya 
kuuaga mwaka 2015 na kuukaribisha ya Mwaka Mpya 2016, katika Mgahawa wa 
City Sports Lounge, Dar es Salaam
Wafanyakazi
 wa Jambo Leo na familia zao pamoja na wageni waalikwa wakiburudika kwa 
muziki uliokuwa ukiporomoshwa wakati wa hafla hiyo iliyofanyika kwenye 
Mgahawa wa kisasa wa City Sports Lounge, katikati ya Jiji la Dar es 
Salaam.
Mhariri 
wa Michezo na Burudani wa Gazeti la Staa Spoti ambalo ni gazeti dada la 
 Jambo Leo, Zahoro Mlanzi akigawa ‘champagne’ kwa wafanyakazi wenzake 
wakati wa hafla hiyo.
Mpiga 
Picha Mkuu wa Gazeti la Jambo Leo, Richard Mwaikenda (wa pili kulia), 
akijadiliana jambo na wakurugenzi wa Kampuni za Jambo Concerpts Tanzania
 Limited na Jambo Communication, Theophil Makunga (kushoto), Benny 
Kisaka (wa pili kushoto) na Juma Pinto wakati wa hafla hiyo.
Baadhi ya
 wafanyakazi wa gazeti la Jambo Leo, wakiwa na furaha wakati wa hafla 
hiyo ya kuuaga mwaka 2015 na kuukaribisha Mwaka Mpya 2016, Dar es Salaam
 juzi. Kutoka Kushoto ni Stellah Kessy,  Magendela Hamis, Salha Mohamed,
 Celina Mathew, Suleiman Msuya na Edith Msuya.
Wakipata mlo wa usiku
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Jambo Concepts, Juma Pinto  (kushoto),
 akimuelezea Mpiga Picha Mkuu wa Gazeti la Jambo Leo, Richard Mwaikenda 
kuwa wakati gazeti la Jambo Leo lilipoanzishwa 2009, alikuwa mfanyakazi 
wa kwanza kujiunga na gazeti hilo akitokea Kampuni ya Business Times.
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Jambo Concepts, Juma Pinto  (kushoto),
 akimuelezea Mhariri wa Habari wa Gazeti la Jambo Leo, Said Mwishehe 
kuwa wakati gazeti la Jambo Leo lilipoanzishwa 2009, alikuwa miongoni 
mwa wafanyakazi wa kwanza kujiunga na gazeti hilo akitokea Kampuni ya 
Business Times.
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Jambo Concepts, Juma Pinto  (kushoto),
 akimuelezea Mwandishi Mwandamizi wa Michezo na Burudani, Asha Kigundula
  kuwa wakati gazeti la Jambo Leo lilipoanzishwa 2009, alikuwa miongoni 
mwa wafanyakazi wa mwanzo  kujiunga na gazeti hilo akitokea Kampuni ya 
Business Times.
Mpigapicha
 Mkuu wa Jambo Leo na magazeti mengine ya Staa Spoti na Jambo Brand 
Tanzania, Richard Mwaikenda, akitoa shukrani wakati wa hafla hiyo/
Mfanyakazi Moi Dodo akiwa na wife wake
Champagne zikifunguliwa
Asha Kigundula akiwamiminia champagne wanahafla
Mwishehe na Kigundula wakikumbatiana kwa furaha
Sasa ni wakati wa kusakata muziki
Ni furaha tele
 PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni