…………………………………….
IDARA ya Uhamiaji mkoa wa Arusha, January 16 inawarejesha kwenye kambi ya wakimbizi raia wa Burundi 21 ,akiwemo mwanamke mtanzania,walionyimwa hadhi ya ukimbizi nchini Kenya..
IDARA ya Uhamiaji mkoa wa Arusha, January 16 inawarejesha kwenye kambi ya wakimbizi raia wa Burundi 21 ,akiwemo mwanamke mtanzania,walionyimwa hadhi ya ukimbizi nchini Kenya..
Afisa Uhamiaji mkoa wa Arusha, 
Ndelema Mwakipesile, alisema hayo ofisini kwake kuwa wakimbizi hao 
akiwemo mwanamke mtanzania ambae ameolewa na raia wa Burundi, 
walikataliwa kuingia nchini Kenya kutokana na kutokuwa na sifa za 
ukimbizi.
Mwakipesile,alisema raia hao wa 
Burundi, waliingia nchini wakipitia mpaka wa Kabanga uliopo mkoani 
Kigoma na kudai wamekuja kuwatembelea ndugu zao lakini mara baada ya 
kuingia nchini walibadirisha mawazo na kuamua kwenda nchini Kenya 
kutafuta hifadhi kwenye kambi ya Kakuma nchini Kenya.
Raia hao 21 wakiwemo watoto 14 
walipofika mpakani Namanga wakitaka kuingia nchini humo walidai 
wanatafuta hifadhi ya ukimbizi na serikali ya Kenya iliwazuia na 
kuwarejesha Tanzania ,ambako ndiko walikopitia kuelekea Kenya.
Mwakipesile, alisema cha 
kushangaza raia hao wa Burundi kila mmoja ana hati ya kusafiria jambo 
ambalo linaonyesha walikuwa wamejiandaa kwa kuwa sheria za kimataifa za 
ukimbizi haziruhusu mkimbizi kuwa na hati bali mkimbizi anakuwa na vitu 
vichache tu pia mkimbizi hachagui kambi ya kupelekwa .
Alisema walipoulizwa kulikoni 
waende Kenya, wakimbizi wamesema kuwa wamekuwa wakiingia nchini mara kwa
 mara kwenye kambi ya wakimbizi ya Kibondo,na wamekuwa wakirejeshwa kwao
 mara kwa mara wanapoingia nchini.
Mwakipesile, alisema wakimbizi hao
 hataki kurejeshwa kwao sasa wamebadirisha mawazo na kuamua kutafuta 
hifadhi nchini Kenya ili kukwepa kurejeshwa kwao.
Alisema wanarejeshwa makwao kwa 
kuwa hawana kosa lolote kwa mjuibu wa taratibu za kimataifa hivyo 
watapelekwa kwenye kambi ya wakimbizi ya Kibondo, ili wasubiri taratibu 
zingine .
Mwakipesile alisema kulingana na 
sheria mkimbizi hawezi kuomba nchi ya kwenda, pia haruhusiwi kwenda nchi
 ya tatu kutoka kwao bali anatakiwa kukimbilia nchi wanayopakana nayo 
Raia hao wa Burundi, walikutwa ndani ya Basi la Tahmeed Coach, lililokuwa likitokea Dar es Salaam kwenda Nairobi nchini Kenya na walipofika mpaka wa Namanga, wakazuiliwa kuingia nchini Kenya .
Raia hao wa Burundi, walikutwa ndani ya Basi la Tahmeed Coach, lililokuwa likitokea Dar es Salaam kwenda Nairobi nchini Kenya na walipofika mpaka wa Namanga, wakazuiliwa kuingia nchini Kenya .
Rai mmoja wa Burundi,ambae 
hakutaka jina lake liandikwe kwa sababu ya usalama ,ambae ni dereva wa 
malori,amesema wamekuwa wakiingia nchini mara kwa mara kwenye kambi ya 
wakimbizi na wamekuwa wakirejeshwa kwao sasa wanataka kwenda kuishi 
kwenye kambi iliyo mbali na kwao kwa kuhofia usalama wao.
Alisema mwezi Desemba mwaka jana 
akiwa nyumbani kwake nchini Burundi,watu watatu waliuliwa mbele ya 
nyumba yake na watoto wake wamekuwa wakiogopa kuishi kutokana na 
kutokuwepo amani nchini mwao na hiyo ni sababu ya msingi ya kuomba 
ukimbizi.
Alisema kuwa yeye amekuwa ni 
dereva wa malori kwa miaka 20 amekuwa akisafirisha mizigo kata ya 
Tanzania na Burundi, lakini kutokana na ukosefu amani nchini mwao 
ameamua kikimbia kutafuta hadhi ya ukimbizi nchini Kenya.
Alisema Tanzania anaipapenda 
tatizo ni kuwa Tanzania imekuwa ikiwarudisha mara kwa mara nchini 
Burundi hivyo wanaomba kwenda nchi ya mbali ili wasirudishwee mwakwao. 
Ameongeza kuwa maafisa wa Burundi wamekuwa wakienda kwenye kambi ya wakimbizi na kuwatambua na kasha huuliwa hivyo wanahofia usalama wao.
Ameongeza kuwa maafisa wa Burundi wamekuwa wakienda kwenye kambi ya wakimbizi na kuwatambua na kasha huuliwa hivyo wanahofia usalama wao.
Kwa upande wake Mtanzania 
aliyeolewa na raia huyo wa Burundi, Eva Michael Magumula,(37) mzaliwa wa
 Dodoma, alisema ana watoto 6 inalazimika aambatane na mume wake ili 
waweze kulea familia yao.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni