Na. Mwandishi Maalum
Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu na Bunge; 
Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama 
(Mb) ameuagiza uongozi wa Shirika la Tija la Taifa kuwa wabunifu katika 
utoaji wa elimu kwa umma ili jamii iweze kujua kazi na huduma 
zinazotolewa na shirika hilo.
Mhe.
 Mhagama ametoa agizo hilo alipotembelea Shirika la Tija la Taifa (NIP) 
Januari 15,2016 kwa lengo la kujionea  kazi zinazotekelezwa pamoja na 
changamoto zinazolikabili shirika hilo.
“Uongozi
 lazima uangalie changamoto zinazolikabili shirika hili na kuangalia 
namna ya kugeuza changamoto hizo kuwa fursa muhimu na kutoa elimu kwa 
umma wa Watanzania ili wajue umuhimu wa kutumia huduma yenu kwa lengo la
 kujiletea maendeleo,”alisema Mhagama
Waziri
 alielekeza kuwa lazima viongozi wa NIP wawe wabunifu katika kutumia 
vyombo mbalimbali vya habari vinavyoweza kuwafikia wananchi wa aina zote
 huku akisisitiza kuangalia vipindi ambavyo havihitaji kulipiwa.
"Nendeni
 mkaongee na wadau wa vyombo vya habari maana utakuta kuna fursa nyingi 
mngeweza kuzitumia bila gharama yoyote. kuna vipindi kama vile Kipindi 
cha Jambo Tanzania cha TBC 1, kipindi cha Kumekucha cha ITV, kipindi cha
 360 Clouds Tv na Tuongee asubuhi cha Star Tv na vingine vingi amabavyo 
mnaweza kuvitumia kuwafikia wananchi wengi," alisisitiza Mhe. Mhagama.
Waziri
 alisema kuwa kwa kutumia ubunifu na  fursa zilizoko kwenye vyombo vya 
habari shirika litapata kujitangaza bila kutumia gharama na kuweza 
kuyafikia malengo kama kuboresha ujuzi na uelewa wa usimamizi wa  
rasilimaliwatu, kuchapisha na kusambaza fasihi na kuboresha utendaji wa 
Taasisi za umma na zisizokuwa za umma.
Wakati
 akimkaribisha waziri, Mkurugenzi Mtendaji wa NIP  Bw.Novatus Massao 
alieleza kuwa miongoni mwa changamoto zinazokabili shirika hilo  ni 
suala la taswira hasi kwa jamii na uelewa mdogo wa jamii kuhusu faida  
na umuhimu wa Shirika hilo.
Kwa
 upande wake mwenyekiti wa Bodi ya NIP, Prof.Samwel Wangwe aliahidi kuwa
 shirika hilo litahakikisha linatekeleza maagizo yote ya Mhe. Mhagama 
ili kuwezesha watanzania kuelewa na kutumia huduma za shirika hilo.
Aidha,
 Mkurugenzi wa Fedha na Utawala Bw.Raphael Loishiye alimshukuru Mhe. 
Waziri kwa kufanya ziara katika Shirika hilo na kujionea mazingira na 
changamoto wanazokabiliana katika utekelezaji wa majukumu yao.






Hakuna maoni:
Chapisha Maoni