Wazee wakimsimika James Katoro baada ya kuchaguliwa kuwa Diwani wa Kata ya Kayenze katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza.
Na:George Binagi-GB Pazzo @BMG 
Katoro
 alichaguliwa kuwa diwani wa Kata hiyo katika uchaguzi uliofanyika 
Novemba 25,2015 kupitia Chama cha Mapinduzi CCM. Tukio hili limejiri 
jana katika Mkutano wa hadhara wa CCM kuwashukuru wakazi wa Kata hiyo 
kwa kumchagua Katoro kuwa diwani wa Kata hiyo.
Wazee wakimsimika James Katoro baada ya kuchaguliwa kuwa Diwani wa Kata ya Kayenze katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza. 
Mchungaji
 Elias Lutalamamila (wa pili kulia) kwa niaba ya viongozi wa dini 
akimsimika James Katoro baada ya kuchaguliwa kuwa Diwani wa Kata ya 
Kayenze katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza. 
Diwani
 wa Kata ya Kayenze Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza James Katoro (CCM)
 akihutubia katika mkutano wa kuwashukuru wakazi wa Kata hiyo kwa 
kumchagua kuwa diwani wao. Aliahidi kushughulikia kero mbalimbali zilizo
 katika Kata hiyo ambazo ni pamoja na kero ya maji, ujenzi wa zahanati 
na vituo vya afya, miundombinu pamoja na ujenzi wa shule za msingi na 
Sekondari.
Salum
 Abdallah Said ambae ni Mwenyekiti wa CCM Kata ya Kayenze akizungumza 
katika mkutano wa chama hicho wa kuwashukuru wakazi wa Kata hiyo kwa 
ushindi waliokipa chama hicho katika uchaguzi uliofanyika Novemba 
25,20515.
Kulia
 ni Jeremiah Mtoni ambae ni Katibu wa CCM Kata ya Kayenze akizungumza 
katika mkutano wa chama hicho wa kuwashukuru wakazi wa Kata hiyo kwa 
ushindi waliokipa chama hicho katika uchaguzi uliofanyika Novemba 
25,20515.
Elias
 Makaranga (mwenye kinasa sauti) ambae alikuwa Meneja Kampeni wa Diwani 
Katoro katika uchaguzi uliopita akizungumza jambo katika mkutano wa 
kuwashukuru wananchi uliofanyika jana.
Wakazi
 wa Kata ya Kayenze wakifuatilia Mkutano wa Chama cha Mapinduzi CCM 
katika Kata hiyo wa kuwashukuru kwa kukichagua chama hicho katika 
uchaguzi uliofanyika Novemba 25, mwaka jana.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni