PICHA ZA TAFRIJA YA FUTARI YA BAKWATA





























KITWANGA AKABIDHI RASMI OFISI KWA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA, JIJINI DAR ES SALAAM LEO.

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba (kushoto) akipokea taarifa ya makabidhiano kutoka kwa aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo, Charles Kitwanga kwenye ofisi ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, jijini Dar es salaam leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba akizungumza na aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo, Charles Kitwanga (kushoto) pamoja na Watendaji Wakuu wa Wizara hiyo, kwenye ofisi ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, jijini Dar es salaam leo, mara baada ya Wizara Mwigulu kupokea taarifa ya makabidhiano.  Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba (kushoto meza kuu) akimsikiliza aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo, Charles Kitwanga alipokuwa anazungumza na Waziri huyo pamoja na Watendaji Wakuu wa Wizara hiyo, kwenye ofisi ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, jijini Dar es salaam leo, mara baada ya Wizara Mwigulu kupokea taarifa ya makabidhiano ofisini humo.  Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba (kushoto) akimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira (wa pili kulia) alipokuwa anazungumza kabla ya aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo, Charles Kitwanga (wa tatu kulia) kukabidhi ofisi kwa Waziri Mwigulu. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Balozi Simba Yahya.  Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba (kushoto) akimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira (kulia) mara baada ya aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo, Charles Kitwanga (katikati) kukabidhi ofisi kwa Waziri Mwigulu. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba (kushoto), aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo, Charles Kitwanga wakifurahi jambo mara baada ya Waziri Mwigulu kupokea taarifa ya makabidhiano katika tukio lililofanyika ofisini kwa Waziri huyo, jijini Dar es salaam leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba (wa pili kushoto) akipokea taarifa ya makabidhiano kutoka kwa aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo, Charles Kitwanga kwenye ofisi ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, jijini Dar es salaam leo. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira. 
Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

SOBER HOUSE YAADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA KUPIGA VITA MATUMIZI MABAYA YA DAWA ZA KULEVYA.

 Mkuu Wa Wilaya ya Bagamoyo, Alhaj Majid Hemed Mwanga akizungumza na wananchi (hawapo pichani) katika siku ya Kimataifa ya Kupiga Vita Matumizi Mabaya ya Dawa za Kulevya, jana Mkoa wa Pwani kulia ni Mkuu wa Kituo  cha Life and Hope Bagamoyo Sober House,Al-Kareem Bhanji.
 Mkuu Wa Kituo  cha Life and Hope Bagamoyo Sober House, Al-Kareem Bhanji aki akizungumza na wananchi (hawapo pichani) waliofika kwenye siku ya Kimataifa ya Kupiga Vita Matumizi Mabaya ya Dawa za Kulevya, jana Mkoa wa Pwani kushoto ni Mkuu Wa Wilaya ya Bagamoyo,Alhaj Majid Hemed Mwanga.
 Wananchi wakifatilia mada mbalimbali  kwenye siku ya Kimataifa ya Kupiga Vita Matumizi Mabaya ya Dawa za Kulevya, jana Mkoa wa Pwani.
 Waathirika wa Dawa za Kulevya akiandamana siku ya Kupiga Vita Matumizi Mabaya ya Dawa za Kulevya, jana Mkoa wa Pwani.
 Maandamano yakeendelea.
 Kikundi cha Sana cha Bagamoyo wakiigiza kama Waathirika wa Dawa za Kulevya.
 Mkuu Wa Wilaya ya Bagamoyo,Alhaj Majid Hemed Mwanga akiwa kwenye picha ya  Waathirika wa Dawa za Kulevya.
Mkuu Wa Kituo  cha Life and Hope Bagamoyo Sober House,Al-Kareem Bhanji  akiwa kwenye picha ya  Waathirika wa Dawa za Kulevya
(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii)

Na Bakari Madjeshi,Globu ya Jamii
Kituo cha Usaidizi Wa Watu walioathirika na Dawa za Kulevya cha Life and Hope Bagamoyo Sober House leo,June 26,2016 kimeadhimisha siku ya Kimataifa ya Kupiga Vita Matumizi Mabaya ya Dawa za Kulevya.

Maadhimisho hayo hufanyika kila mwaka June 26 lakini kwa Mwaka huu Kituo cha Sober kimeadhimisha siku hiyo Wilayani Bagamoyo.

Akizungumza katika Maadhimisho hayo,Mkuu Wa Wilaya ya Bagamoyo,Alhaj Majid Hemed Mwanga amesema vita vya Mapambano ya Dawa za Kulevya si vya Serikali pekee wala vya mtu mmoja bali ni vita vya kila mtu,ambaye anapaswa kuwajibika katika eneo husika ili kutokomeza kabisa uingizwaji Wa Dawa hizo.

Pia,Mkuu huyo Wa Wilaya ametoa wito kwa Viongozi Wa Dini ,Wananchi pamoja na Vyombo vya Ulinzi na Usalama kushirikiana kwa pamoja katika kutoa taarifa za kuwafichua waingizaji Wa Dawa hizo ili Serikali kuwachukulia hatua kali za kisheria.

Amesema,Serikali imeahidi kupatikana kwa eneo kubwa ili kuendeleza kituo hicho na kuwasaidia vijana ambao ndio waathirika wakubwa Wa janga hilo na kuitaka jamii kuwatambua na kuwabaini waathirika wa Dawa hizo.

Kwa upande wake,Mkuu Wa Kituo hicho cha Life and Hope Bagamoyo Sober House,Al-Kareem Bhanji amesema kituo hicho kimesaidia watu zaidi ya 100 mpaka sasa,ambapo ametoa Changamoto za ukosefu wa Majengo kituoni hapo  jambo ambalo limepelekea kwa sasa kulipa kodi kubwa ya pango.

Pia ameiomba Serikali kupatikana Ardhi ya kutosha ili kuweza kuongeza majengo na kukidhi haja ya kupokea Waathirika 200 ikiwa Wanaume 150 na Wanawake 50.

AIRTEL YAZINDUA MSIMU WA 6 WA MICHUANO YA AIRTEL RISING STARS 2016

 Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano akimuonesha Waziri wa Habari, Utamanduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye  baadhi ya wachezaji wa timu ya taifa chini ya umri wa miaka 17 Serengeti Boys waliopatiakana kupitia michuano ya Airtel Rising Stars wakati wa uzinduzi wa awamu ya sita ya michuano hiyo uliofanyika Dar es Salaam Jumapili Juni 26 2016.
 Waziri wa Habari, Utamanduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye akipinga mpira kuashiria uzinduzi wa rasmi wa michuano ya Airtel Rising Stars 2016. Uzinduzi huo umefanyika Jumapili 26 Juni 2016 kwenye makao makuu ya Airtel Tanzania Dar es Salaam.
 Waziri wa Habari, Utamanduni ,Sanaa na Michezo Nape Nnauye akisisitiza jambo wakati wa ufunguzi wa michuano ya Airtel Rising Stars 2016 jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano akiongea wakati wa uzinduzi wa msimu wa 6 wa Airtel Rising Stars.
 Rais wa TFF Jamal Malinzi akiongea wakati wa uzinduzi wa msimu wa 6 wa Airtel Rising Stars.
 Waziri wa Habari, Utamanduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye akiwa katika picha ya pamoja na viongezi wa TFF pamoja na Airtel Mara baada ya uzinduzi wa Msimu wa sita wa michuano ya Airtel Rising Stars
Wafanyakazi wa Airtel wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Habari, Utamanduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye wakati wa uzinduzi wa wa Msimu wa sita wa michuano ya Airtel Rising Stars.
Airtel yazindua msimu wa 6 wa michuano ya Airtel Rising Stars 2016
Dar es Salaam, Jumapili 26 Juni 2016  Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mheshimiwa Nape Nnauye leo amezindua msimu wa sita wa mashindano ya soka ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars na kuwapongeza Airtel Tanzania kwa kuendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali pamoja na shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) za kukuza mchezo wa soka.

“Programu za soka za vijana ndiyo muhimili wa maendeleo ya soka popote pale duniani. Ndiyo maana nasisitiza umuhimu wa mashindano ya Airtel Rising Stars ambayo matunda yake yameonekana dhahiri katika kipindi cha miaka mitano iliyopita”, alisema Nnauye.   

Alitoa mfano wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 Serengeti Boys ambayo wachezaji wake 10 wa kutumainiwa wametokana na Airtel Rising Stars. “Matunda ya Airtel Rising Stars vilevile yanaoneka dhahiri kwenye timu ya taifa ya wanawake Twiga Stars ambayo wachezaji wake wote wanatokana na programu hii ya vijana”, alisema Nnauye. Klabu za daraja la kwanza na ligi kuu Tanzania bara pia zinafaidi matunda ya Airtel Risings Stars. 

Waziri amewataka viongozi wa soka kusimamia vizuri pragarmu ya Airtel Rising Stars ili kuweza kubaini vipaji vingi zaidi kupitia mashindano haya ya vijana ya kila mwaka yakishirikisha timu za wasichana na wavulana kuanzia ngazi ya mkoa na kuhitimishwa kwa fainali ya Taifa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla hiyo ya uzinduzi, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano alimhakikishia waziri kuwa kampuni ya Airtel Tanzania ina nia thabiti ya kuendelea kudhamini michuano hiyo ambayo imesaidia kuzalisha wachezaji wengi chipukizi hivyo kuendeleza mchezo huo marufu hapa nchini.

Alisema Airtel Rising Stars mwaka inafanyika chini ya mwanvuli wa kampeni ya Airtel RURSA iliyozinduliwa mwaka jana kwa lengo la kuwahamasisha vijana kutumia fursa mbalimbali walizonazo ili kujiendeleza kiuchumi. “Airtel Rising Stars yenyewe ni Airtel FURSA kwa kuwa inawawezesha vijana kutumia vipaji vyao kujikwamua kimaisha kupitia mpira. Mpira ni chano cha kipato cha kuaminika”, alisema.
“Kwa kuwa na wateja wengi nchi nzima Tanzania bara na Zanzibar, Airtel Tanzania tunawiwa kuendelea kutoa sehemu ya faida yetu kwa jamii kupitia mchezo wa mpira wa miguu ambao ni marufu kuliko michezo yote hapa Tanzania. Ni njia ya kuwashukuru wateja wetu kwa kuedelea kutuunga mkono”, alisema.  

Kwa upande wake, Rais wa TFF Jamal Malinzi alisema programu ya Airtel Rising Stars imeleta mapinduzi na kubadilsha kabisa sura ya mchezo wa soka hapa nchini. “Nawapongeza Airtel Tanzania kwa kuendelea kutuunga mkono. Naamini kwamba tutapata mafanikio makubwa zaidi siku za usoni”, alisema.
Airtel Rising Stars mwaka huu itashirkisha timu kutoka mikoa ya Mwanza, Morogoro, Mbeya, Temeke, Ilala, Morogoro (wavulana) wakati mikoa itakayoshirikisha timu za wasichana ni Ilala, Kinondoni, Temeke,  Arusha, Lindi na Zanzibar.

BENKI YA CRDB YAFADHILI UJENZI WA KITUO CHA MAWASILIANO CHA JESHI LA POLISI

Jiwe la Msingi la Kituo cha Mawasiliano cha Jeshi la Polisi lililowekwa na Rais Dk. John Magufuli. Kituo hicho kimefadhiliwa na Benki ya CRDB kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 300. (Picha na Francis Dande)
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kushoto) akiteta jambo na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Esther Kitoka.
Brass Band ya Polisi ikitumbuiza katika hafla ya uzinduzi wa Kituo cha Mawasiliano cha Jeshi la Polisi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhandisi Hamad Masauni akimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk.Charles Kimei.
Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba akisalimia na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk.Charles Kimei.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba (wa kili kulia) akifurahia jambo na Naibu wake (kulia), IGP,Ernest Mangu, wapili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akisalimia na Rais John Magufuli.
 Rais John Magufuli akisalimia na Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja, Tully Esther Mwambapa.
 Mkurugenzi wa Utawala wa Benki ya CRDB, Beatus Segeja akisalimiana na Rais Dk. John Magufuli
 Naibu Mkurugenzi Mtendaji, Esther Kitoka akisalimiana na Rais Dk. John Magufuli.
 Rais John Magufuli akizindua rasmi Kituo cha Mawasiliano cha Jeshi la Polisi Dar es Salaam.
 Rais Magufuli akipata maelezo ya namna kituo hicho kinavyofanyakazi.
  Rais Magufuli akipata maelezo ya namna kituo hicho kinavyofanyakazi.
 Wakurugenizi wa Benki ya CRDB wakifuatilia uzinduzi huo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk.Charles Kimei akitoa hotuba yake.
Rais John Magufuli akimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk.Charles Kimei baada ya kutoa hotuba yake. 
 Rais John Magufuli akifurahia jambo wakati akimkabidhi Tuzo ya Ufadhili Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei, wakati wa uzinduzi wa Kituo cha Mawasiliano cha Jeshi la Polisi, uliofanyika katika viwanja vya Biafra jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki. ambapo benki hiyo imetoa zaidi ya shs. milioni 300. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba. 
 Rais John Magufulia (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Serikli. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk.Charles Kimei.