TTB KUTANGAZA UTALII KWA NJIA YA MITANDAO

P twoNa  Geofrey Tengeneza
Bodi ya Utalii Tanzania imeanzisha touvuti maalumu iitwayo Destination Tourism Portal pamoja na nyenzo (App) kwa watumiaji wa simu za mikononi na hivyo kuendelea kujikita zaidi katika matumizi ya tovuti na mitandao ya Kijamii (e-marketing) katika kutekeleza majukumu yake ya utangazaji wa vivutio vya Utalii vya Tanzania duniani kwa lengo la kuvutia watalii wengi zaidi.
“Tovuti hii inalenga zaidi katika kuwasaidia wajasiriamali wadogo na wa kati katika sekta ya utalii kufanya biashara zao kwa urahisi na kukuza mapato yao na faida zaidi” alisema Bw. Chitaunga.
Ameongeza kuwa Tovuti hii inatumia anuani ya www.tanzaniatourism.com ina taarifa nyingi sana za
vivutio vya utalii vinavyopatikana hapa nchini lakini pia taarifa kuhusu malazi (accommodation) na huduma nyinginezo na kwamba inamwezesha mtalii kufanya malipo online.
Mkurugenzi huyo wa Masoko amesema kuwa sambamba na uanzishaji wa tovuti hiyo, tumeanzisha pia nyenzo rasmi ya Utalii iitwayo Tanzania Tourism App ambayo kama ilivyo kwa portal ina taarifa nyingi za utalii ikiwa ni pamoja na vivutio vya utalii, malazi na namna ya kupanga safari kwa mtalii anayetaka kutembelea Tanzania, na kufanya malipo online.
Amesema kuwa Nyenzo (App) hii inapatikana katika Google play store kwa watumiaji wa simu za Android duniani kote na muda si mrefu itapatikana pia katika AppStore kwa watumiaji wa simu za Iphone.
Amedokea kuwa zipo nyenzo (Apps) kadhaa zilizoanzishwa na makapuni au watu binafsi kama vile Tanzania Safari Guide; Tanzania Travel Safari; Destination Tanzania: Tanzania Travel and Tourism n.k lakini hii ya kwetu ndiyo hasa rasmi ya Serikali.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni