Bodi ya Utalii Tanzania 
imeanzisha touvuti maalumu iitwayo Destination Tourism Portal pamoja na 
nyenzo (App) kwa watumiaji wa simu za mikononi na hivyo kuendelea 
kujikita zaidi katika matumizi ya tovuti na mitandao ya Kijamii 
(e-marketing) katika kutekeleza majukumu yake ya utangazaji wa vivutio 
vya Utalii vya Tanzania duniani kwa lengo la kuvutia watalii wengi 
zaidi.
“Tovuti hii inalenga zaidi katika
 kuwasaidia wajasiriamali wadogo na wa kati katika sekta ya utalii 
kufanya biashara zao kwa urahisi na kukuza mapato yao na faida zaidi” 
alisema Bw. Chitaunga. 
Ameongeza kuwa Tovuti hii inatumia anuani ya www.tanzaniatourism.com ina taarifa nyingi sana za
vivutio vya utalii 
vinavyopatikana hapa nchini lakini pia taarifa kuhusu malazi 
(accommodation) na huduma nyinginezo na kwamba inamwezesha mtalii 
kufanya malipo online.
Mkurugenzi huyo wa Masoko amesema
 kuwa sambamba na uanzishaji wa tovuti hiyo, tumeanzisha pia nyenzo 
rasmi ya Utalii iitwayo Tanzania Tourism App ambayo kama ilivyo kwa 
portal ina taarifa nyingi za utalii ikiwa ni pamoja na vivutio vya 
utalii, malazi na namna ya kupanga safari kwa mtalii anayetaka 
kutembelea Tanzania, na kufanya malipo online.
Amesema kuwa Nyenzo (App) hii 
inapatikana katika Google play store kwa watumiaji wa simu za Android 
duniani kote na muda si mrefu itapatikana pia katika AppStore kwa 
watumiaji wa simu za Iphone.
Amedokea kuwa zipo nyenzo (Apps) 
kadhaa zilizoanzishwa na makapuni au watu binafsi kama vile Tanzania 
Safari Guide; Tanzania Travel Safari; Destination Tanzania: Tanzania 
Travel and Tourism n.k lakini hii ya kwetu ndiyo hasa rasmi ya Serikali.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni