MKOA
 wa Arusha, utaadhimisha siku ya mazingira duniani June 5 kwa kupanda 
miti aina mbalimbali ya matunda ,vivuli na ya asili kwenye shule za 
msingi na vyanzo vya maji ili kutunza na kuhifadhi mazingira.
Katibu tawala mkoa wa 
Arusha,Richard Kwitega, amesema kwenye maadhimisho hayo ambayo kilele 
chake kitakuwa ni Juni 5 mwaka huu mkoa utapanda miti kwenye maeneo yote
 ya mkoa huo lengo ni kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na 
kutekeleza jukumu la  shirika la mazingira duniani, UNEP.
Amesema shirika la umoja wa 
mataifa la mazingira UNEP, limepanga juni 5 kila mwaka ni siku ya 
maadhimisho ya mazingira duniani,ili watu wajue umuhimu wa kutunza na 
kusimamia mazingira yao.
Alisema kila nchi mwanachama 
ikiwemo Tanzania, inayo sauti katika kikao cha baraza la mazingira 
duniani  juu ya mazingira endelevu .
Kwitega,alisema mwaka huu 2016 
maadhimisho ya mazingira kimataifa yanaadhimishwa nchini Angola,yakiwa 
na kauli mbiu isemayo uvumilivu  ufike mwisho juu ya biashara haramu ya 
wanyama pori ambayo hupelekea wanyama pori kutoweka kwenye IKolojia.
Alisema kaulimbiu hiyo inatutaka kuacha kuwauwa wanyamapori  kwa lengo la kuuza viungo vyao  na kuharibu mazingira .
Kwitega,amesema katika 
kutekeleza jukumu hilo mkoa huo, unashirikiana na wadau mbalimbali wa 
maendeleo zikiwemo halmashauri na asasi binafsi kuadhimisha siku hiyo ya
 mzngira duniani kwa kupanda miti maeneo mbalimbali.
Alisema kwa kuanza mkoa 
utapanda miti ya matunda kwenye shule tano za msingi za jijini Arusha, 
ambazo ni Makumbushi, Arusha school, Naura, Meru na Levolosi,na kwenye 
chanzo cha maji cha Kiranyi, kutapandwa miti ya asili  ambayo ni rafiki 
wa mazingira ili kutunza chanzo hicho.
Alisema maadhimisho hay mwaka 
huu hayataadhimishwa kitaifa bali kila mkoa kila mkoa umepewa jukumu la 
kuadimisha maadhimisho hayo kwa kushirikiana na halmashauri zake na 
wadau wake wa maendeleo.
Alisema kauli mbiu ya taifa 
mwaka huu inasema tuhifadhi vyanzo  vya maji  kwa uhai wa taifa  letu 
 na mkoa utaendelea kutoa elimu ya uhifadhi wa mazingira kwa jamii 
kuanzia juni 2 hadi siku ya kilele juni 5
Kwitega, alisema  katika 
maadhimisho hayo wananchi na wadau watafanya usafi kwenye maeneo 
mbalimbali ikiwemo soko la Kilombero, na kwenye makazi kuanzia ngazi ya 
kaya ,kitongoji,kijiji,mtaa na kata ,na akatoa wito kwa kila mwananch na
 taasisi mbalimbali kuhakikisha wanapanda miti kwenye maeneo yao.
Alisema kuwa siku ya kilele ya 
maadhimisho hayo ya mazingira duniani,mkuu wa mkoa wa Arusha, Felix 
Ntibenda,(KIJIKO)ataongoza wananchi kupanda mti wa kumbukumbu kwenye 
bustani ya Peace Park, iliyopo mzunguko wa Impala hotel jijini hapa .
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni