Balozi
 wa India hapa nchini, Sandeep Arya akizungumza na waandishi wa habari 
(hawapo pichani) juu ya watanzania wajitokeze  kwa wingi kufanya mazoezi
 siku ya Juni 19 mwaka huu kwenye ufukwe wa Coco beach jijini Dar es 
Salaam.
 Balozi
 wa India hapa nchini, Sandeep Arya akiwaonesha waandishi wa habari 
(hawapo pichani)  nembo ya Yonga, leo jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya watu waliofika kufanya mazowezi ya Yoga, leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii)
MAZOEZI
 ya viungo vya mwili yenye asili ya Indi nchiniIndia yanatarajia 
kufanyika Juni 19 mwaka huu katika viwanja vya ufukwe wa Cocobeach 
jijini Dar es Salaa ikiwa ni kuadhimisha siku ya Utamaduni wao na 
kimataifa kwa ujumla.
Akizungumza
 na wanahabari jijini Dar es Salaam, Balozi wa India hapa nchini, 
Sandeep Arya amesema kuwa Yogo ni mazoezi ya kiroho na kimwili yenye 
asili katika falsafa ya uhindi kwa mda wa miaka mingi.
Alimnukuu
 Waziri Mkuu wa India, Shri Narendra wakati akihutubia mkutano wake wa 
69 wa Baraza Kuu la Umojawa Mataifa Septemba 27, 2014 alipendekeza 
jumuiya yakimataifa kupitisha siku ya Kimataifa ya Yoga.
Aidha
 ameeleza kuwa siku ya Yoga sio tu kufanya mazoezi bali mbinu ya 
kujitambua na kutambua mahusiano ya mtu na dunia na mazingira yake.
Balozi
 huyo amewaomba watanzania kujitokeza kwawingi kufanya mazoezi siku ya 
Juni 19 mwaka huu kwenye ufukwe wa Cocobeach Dar es Salaam huku 
akisemamazoezi ni uhai wa binadamu hivyo siku hiyo watawezakufundishwa 
mbinu mbalimbali za kufanya mazoezi yaviungo kutoka kwa wataalamu kutoka
 nchini India.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni