Na Mahmoud Ahmad Arusha
Taifa
 letu linahitajia kuangalia kwa mapana takwimu za wahitimu wahandisi ni 
wengi kuliko wahitimu mafundi sanifu kutokana na hali hiyo huduma za 
kihandisi na za ufundi hazitakidhi matakwa ya maendeleo yanayotarajiwa 
na itakuwa vigumu kufikia malengo makuu ya dira ya maendeleo ya Tanzania
 2025 na pia ya MKUKUTA awamu ya pili.
Kauli
 hiyo imetolewa na Katibu mkuu wa wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi 
Maimuna Tarishi kwa niaba ya waziri wa wizara hiyo Prof Joyce Ndalichako
 wakati wa uzinduzi wa maabara ya skimu ya umwagiliaji (Hydraulics 
Engineering) iliyojengwa na shirika la misaada la Japan(JAICA)kwenye 
chuo cha ufundi Arusha jijini Arusha.
Alitanabaisha
 kuwa Mashirika ya kimataifa yamekuwa kupendekeza kuwa na uwiano kwa 
kila mhandisi mmoja pawepo na mafundi watano na mchundo 25 ilikuweza 
kuleta maendeleo ipasavyoi katika nchi yetu.
Tarishi
 alisema kuwa kasi ya kuendeleza kilimo cha umwagiliaji nchini ni ndogo 
kwa sababu ya uhaba wa maofisa ugani na wataalamu mbali mbali wa 
umwagiliaji wenye uwezo wa kusimamia utekelezaji hasa kwenye ngazi ya 
halmashauri zetu hapa nchini,chuo kama sehemu inatakiwa kubuni mbinu 
mbadala za kuweza kutowa na kuandaa mipango ya masomo yatakayosaidi 
upatikanaji wa ajira kwenye soko la ajira.
"Changamoto
 ya kupata ajira kwa baadhi ya waajiri hawajajumuisha hii kada ya 
uhandisi ujenzi na umwagiliaji katika(Scheme of service) zao hivyo basi 
tunaomba waajiri wote kujumuisha kada hii muhimu katika(Scheme of 
service)zao ili kutatua changamoto hii na kuongeza tija katika kazi zetu
 za kilimo cha umwagiliaji"alisema Tarishi
Aidha
 katibu mkuu huyo alitanabaisha kuwa kutokana na hali hiyo tunaomba kuwa
 program za ufundi sanifu zipewe kipaumbele kwani taifa lenye rasilimali
 nyingi litanufaidika na rasilimali hizo tu iwapo litaziongezea 
thamani(processing and value addition)kabla ya kuuzwa vinginevyo taifa 
hilo litachuuza hizo rasilimali na halitaendelea.kwani mafundi saniu 
mahiri ni mhimili mkuu wa kuongeza thamani ya rasilimali zetu.
Kwa
 upande wake balozi wa japani hapa nchini Masaharu Yoshinda wakati 
akikabidhi mradi huo kwa serikali ya Tanzania alisema kuwa mradi huo wa 
mashine ya umwagiliaji ni mkubwa na mashine ya aina hiyo haipo katika 
ukanda huu wa Afrika mashariki na kati na itasaidia nchi ya Tanzania 
kuwajenga wataalamu wa masuala ya umwagiliaji na kukuza kilimo cha 
umwagiliaji nchini kwenu.
Alisema
 kuwa serikali ya Japan itaendelea kutoa wataalam katika kuhakikisha 
utaalamu huo unawafikia watanzania wote ilikukuza uchumi wa nchi yenu 
kwa kuweza kukuza uzalishaji na hatimaye viwanda.
Kwa
 upande wake Mkuu wa Chuo Cha Ufundi Arusha dkta Richard Masika alisema 
kuwa mradi huo utasaidia chuo na vyuo vyengine kuweza kuinua taaluma 
kwani mashine hiyo itasaidia kukuza na kuweka mezania kwa wahitimi na 
kwenda kufanya vizuri katika kukuza kilimo cha umwagiliaji hapa nchini.
Alisema
 kuwa serikali ya Japan imekuwa mstari wa mbele katika kujengea uwezo 
chuo kupitia ufadhili wa mfuko wa chakula wa pamoja kati ya Tanzania na 
Japan(TJFACF) Kwa wanachuo na chuo wamejengewa uwezo wa kufundisha 
program ya uhandisi ujenzi na umwagiliaji kupitia mradi"kujenga uwezo wa
 wanataaluma katika kutoa mafunzo ya uhandisi Umwagiliaji yaani (ATC 
irrigation human Resoursces Development Programme AIHRDP)Unaofadhiliwa 
na serikali hiyo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni