SERIKALI YATAKIWA KUZALISHA RASILIMALI ITAKAZOSAIDIA KUKUZA NA KUPUNGUZA SOKO LA AJIRA

Image result for arusha technical college
 
 
Na Mahmoud Ahmad Arusha
Taifa letu linahitajia kuangalia kwa mapana takwimu za wahitimu wahandisi ni wengi kuliko wahitimu mafundi sanifu kutokana na hali hiyo huduma za kihandisi na za ufundi hazitakidhi matakwa ya maendeleo yanayotarajiwa na itakuwa vigumu kufikia malengo makuu ya dira ya maendeleo ya Tanzania 2025 na pia ya MKUKUTA awamu ya pili.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu mkuu wa wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi Maimuna Tarishi kwa niaba ya waziri wa wizara hiyo Prof Joyce Ndalichako wakati wa uzinduzi wa maabara ya skimu ya umwagiliaji (Hydraulics Engineering) iliyojengwa na shirika la misaada la Japan(JAICA)kwenye chuo cha ufundi Arusha jijini Arusha.

Alitanabaisha kuwa Mashirika ya kimataifa yamekuwa kupendekeza kuwa na uwiano kwa kila mhandisi mmoja pawepo na mafundi watano na mchundo 25 ilikuweza kuleta maendeleo ipasavyoi katika nchi yetu.

Tarishi alisema kuwa kasi ya kuendeleza kilimo cha umwagiliaji nchini ni ndogo kwa sababu ya uhaba wa maofisa ugani na wataalamu mbali mbali wa umwagiliaji wenye uwezo wa kusimamia utekelezaji hasa kwenye ngazi ya halmashauri zetu hapa nchini,chuo kama sehemu inatakiwa kubuni mbinu mbadala za kuweza kutowa na kuandaa mipango ya masomo yatakayosaidi upatikanaji wa ajira kwenye soko la ajira.

"Changamoto ya kupata ajira kwa baadhi ya waajiri hawajajumuisha hii kada ya uhandisi ujenzi na umwagiliaji katika(Scheme of service) zao hivyo basi tunaomba waajiri wote kujumuisha kada hii muhimu katika(Scheme of service)zao ili kutatua changamoto hii na kuongeza tija katika kazi zetu za kilimo cha umwagiliaji"alisema Tarishi

Aidha katibu mkuu huyo alitanabaisha kuwa kutokana na hali hiyo tunaomba kuwa program za ufundi sanifu zipewe kipaumbele kwani taifa lenye rasilimali nyingi litanufaidika na rasilimali hizo tu iwapo litaziongezea thamani(processing and value addition)kabla ya kuuzwa vinginevyo taifa hilo litachuuza hizo rasilimali na halitaendelea.kwani mafundi saniu mahiri ni mhimili mkuu wa kuongeza thamani ya rasilimali zetu.

Kwa upande wake balozi wa japani hapa nchini Masaharu Yoshinda wakati akikabidhi mradi huo kwa serikali ya Tanzania alisema kuwa mradi huo wa mashine ya umwagiliaji ni mkubwa na mashine ya aina hiyo haipo katika ukanda huu wa Afrika mashariki na kati na itasaidia nchi ya Tanzania kuwajenga wataalamu wa masuala ya umwagiliaji na kukuza kilimo cha umwagiliaji nchini kwenu.

Alisema kuwa serikali ya Japan itaendelea kutoa wataalam katika kuhakikisha utaalamu huo unawafikia watanzania wote ilikukuza uchumi wa nchi yenu kwa kuweza kukuza uzalishaji na hatimaye viwanda.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo Cha Ufundi Arusha dkta Richard Masika alisema kuwa mradi huo utasaidia chuo na vyuo vyengine kuweza kuinua taaluma kwani mashine hiyo itasaidia kukuza na kuweka mezania kwa wahitimi na kwenda kufanya vizuri katika kukuza kilimo cha umwagiliaji hapa nchini.

Alisema kuwa serikali ya Japan imekuwa mstari wa mbele katika kujengea uwezo chuo kupitia ufadhili wa mfuko wa chakula wa pamoja kati ya Tanzania na Japan(TJFACF) Kwa wanachuo na chuo wamejengewa uwezo wa kufundisha program ya uhandisi ujenzi na umwagiliaji kupitia mradi"kujenga uwezo wa wanataaluma katika kutoa mafunzo ya uhandisi Umwagiliaji yaani (ATC irrigation human Resoursces Development Programme AIHRDP)Unaofadhiliwa na serikali hiyo.
 
Mwisho

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni