Mkuu
 wa mkoa wa Arusha Daudi Felix Ntibenda ameyataka mashirika yanahusika 
na kutathimini viwango vya ubora nchini kuhakikisha wanafika katika 
viwanda na  kwa wazalishaji wadogo wadogo ili kuweza kupata twakimu za 
ubora kwa usahii zaidi na kuboresha  hali za bidhaa hapa nchini
Wito
 huo ameutoa hivi karibuni kwenye mkutano wa  mashrikia ya viwango 
Barani Afrika ambapo shirika la viwango Tanzania  TBS pamoja na shirika 
la viwango Afrika ARSO wamezikutanisha nchi zipatazo 15 pamoja na wadau 
wengine kutoka mataifa ya Ulaya.
"Ni
 jukumu la viwango, unajua mara nyingi tumekuwa na matatizo mengi kwenye
 uzalishaji wa bidhaa zetu,kwenda kuwa chini ya viwango,lakini kwa 
utaratibhuu ambao (TBS)wameuandaa wao wenyewe,ninauhakika sasa tutakuwa 
na vitu vinavyokwenda na viwango,ama kiwango ambacho kipo kwenye 
soko,labda niombe (TBS)wawe na wasimamzi ambao wanaweza kuenea Nchi 
nzima ili kuhaikisha tupata bidhaa ambazo zipo kwenye viwango,alisema 
N'tibenda."
Mkurugenzi
 mkuu wa TBS  Tanzania Joseph Masikitiko amesema kuwa  mkutano huo ambao
  wanaanza kukaa kamati kuu ya viwango Afrika na baadae kufuatiwa na 
mkutano mkuu wa wanachama wa shirika la Viwango TBS sambamba na kuwepo 
na siku ya viwango Afrika.
Aidha
 ameongezea kusema kuwa katika mkutano huu Mashirika hayo yanatarajiwa 
kukaa na kutoka na maazimio ya pamoja na kupata njia maafaka za kupata  
bidhaa zinazolingana  kwa viwango ili kuweza kupata bidhaa zinazotoka 
afika zenye viwango sawa.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni