Mkuu wa mkoa wa Arusha Filex Ntibenda amelitaka shirika la 
viwango(TBS) kushughulikia vipasavyo bidhaa  zinazozalishwa hapa nchini 
zisizo kidhi viwango vinavyotakiwa ili kuondoa bidhaa  zisizo na ubora.
Ameyasema hayo Jana wakati akifungua Mkutano wa 22 wa 
maonesho ya viwango barani Afrika yaliyoanza jijini Arusha na 
kushirikisha nchi zaidi ya 15.
Ntibenda alisema kuwa kumekuwepo na tatizo la nchini katika
 suala la uzalishaji wa bidhaa  hivyo ili kuhakikisha   bidhaa  hafifu 
hazitengenezwi kwa mashirika hayo kuongeza juhudi katika usimamizi.
"Ili kuandokana na bidhaa  zisizokidhi viwango hapa nchini 
mnatakiwa  kuwajibika ipasavyo katika kuhakikisha bidhaa  hizo 
hazizalishwa" Alisema Ntibenda.
Kwa upande wake mkurugenzi mkuu wa shirika la viwango 
Tanzania Joseph Masikitiko alieleza kuwa pasipo viwango huwezi kufanya 
biashara yoyote iyostahili kwa kuwa itakuwa  haijathibitishwa  .
Alisema lengo la Mkutano huo ni kuboresha viwango kuwa katika hali ya ubora zaidi na   kwa kiwango kimoja Afrika.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni