Maabara yenye mtambo wa kisasa wa utafiti yazinduliwa




Katibu mkuu wa wizara ya elimu sayansi na teknolojia Maimuna Tarishi amezindua maaabara ya kisasa yenye mtambo wa utafiti wa mwendo kasi wa maji kabla ya kufanya shughuli za kilimo katika chuo cha ufundi jijini Arusha

Akizundua mtambo huo uliogarimu dolla za kimarekani kiasi cha shilingi laki nne, Maimuna amewataka wanafunzi wa kozi ya kilimo na umwagiliaji kujifunza kilimo cha kisasa kinacho endana na teknolojia ya sasa  

Mkuu wa chuo hicho cha ufundi cha Arusha Technical Collage Dokta Richard Masika amesema kukamilika kwa mradi huo umepunguza garama kubwa ya kuwapeleka wanafunzi na wakufunzi kupata masomo nje ya chuo hicho

Amesema kwa saa wanafunzi wa kozi ya umwagiliaji na kilimo watapata fursa ya kufanya vizuri katika masomo yao mara baada ya kukamilika kwa maabara ya kisasa yenye mtambo wa kupima na kufanya utafiti kabla kilimo

Balozi wa japani nchini Tanzania Masaharu Yoshida amesema  nchi ya japani bado itaendelea kutoa misaada katika chuo hicho hususani katika kukuza kilimo cha kisasa kama alivyo ambiwa na Rais wa Jamuhuri wa Mungano wa Tanzania dokta john Pombe Magufuli kuwa nchi ya Tanzania inataji kupiga hatua katika kilimo cha kisasa

Makamu mkuu wa idara ya uwandisi ujenzi katika chuo icho bwana Faraji Mgania ameiyomba wizara ya elimu kutatuwa changamoto kadhaa zinazo ikabili maabara hiyo ikiwemo vifaa vya mwendo kazi vya kubana maji katika mtambo huo

Mtambo huo ulio faziliwa na serikali ya japani ni wa kipee barani afrika na utasaidia wananfunzi wa chuo icho pamoja na nje ya taasisi hiyo kupata mafunzo ya utafiti mwendo.kasi wa maji bila ya kilimo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni