Mkurugenzi
 Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa akizungumza leo 
jijini Dar es Salaam katika hafla ya kukabidhiana magari tisa yenye 
thamani ya Shillingi Millioni mia nane na kumi kutoka Shirika la ICAP 
Tanzania kwa ajili ya Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania
 utakaofanyika nchi nzima kuanzia mwezi Septemba, 2016. Kushoto kwake ni
 Claud Kumalija mwakilishi wa katibu Mkuu wa Wizara Afya, Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.
 Mwenyekiti
 wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS), Dkt. Fatuma Mrisho akizungumza 
leo jijini Dar es Salaam katika hafla ya kukabidhiana magari tisa yenye 
thamani ya Shillingi Millioni mia nane na kumi kati ya Ofisi ya Taifa ya
 Takwimu na Shirika la ICAP Tanzania kwa ajili ya Utafiti wa Viashiria 
na Matokeo ya UKIMWI Tanzania utakaofanyika nchi nzima kuanzia mwezi 
Septemba, 2016. Kushoto kwake ni Claud Kumalija mwakilishi wa katibu 
Mkuu wa Wizara Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na 
kulia kwake ni Dkt. Michelle Roland Mkurugenzi Mkaazi wa Taasisi ya 
Marekani ya Kudhibiti Magonjwa – (Centre for Disease Control and 
Prevention - CDC).
 Mkurugenzi
 Mkaazi wa Shirika wa Taasisi ya Marekani ya Kudhibiti Magonjwa – 
(Centre for Disease Control and Prevention - CDC) Dkt. Michelle Roland 
akikata utepe kuashiria kukabidhi rasmi magari tisa yenye thamani ya 
Shillingi Millioni mia nane na kumi kwa Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa 
ajili ya Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania 
utakaofanyika nchi nzima kuanzia mwezi Septemba, 2016.
 Mkurugenzi
 Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa pamoja na 
mwakilishi wa katibu Mkuu wa Wizara Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, 
Wazee na Watoto Claud Kumalija wakionyesha ufunguo wa gari mbele ya 
waandishi wa habari na wageni waalikwa kuashiria kupokea magari tisa 
yaliyotolewa na Shirika la ICAP Tanzania kwa ajili ya Utafiti wa 
Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania utakaofanyika nchi nzima kuanzia
 mwezi Septemba, 2016.
 Mkurugenzi
 Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa akiwasha gari kama 
ishara ya kupokea magari tisa yenye thamani ya Shillingi Millioni mia 
nane na kumi kutoka Shirika la ICAP Tanzania kwa ajili ya Utafiti wa 
Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania utakaofanyika nchi nzima kuanzia
 mwezi Septemba, 2016. Hafla ya makabidhiano ya magari hayo imefanyika 
leo jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi
 Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa (wa kwanza kulia) 
pamoja na wageni waliohudhuria katika hafla ya kukabidhiana magari 
wakiangalia baadhi ya magari yaliyotolewa na Shirika la ICAP Tanzania 
kwa ajili ya Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania 
utakaofanyika nchi nzima kuanzia mwezi Septemba, 2016. Hafla ya 
makabidhiano ya magari hayo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.
(PICHA ZOTE NA EMMANUEL GHULA)
Na: Veronica Kazimoto.
OFISI
 ya Taifa ya Takwimu imekabidhiwa magari tisa aina ya Land cruiser yenye
 thamani ya Dola za kimarekani laki nne na elfu tano ($ 405,000) sawa na
 Shillingi za kitanzania Milioni mia nane na kumi (810,000,000/=) kutoka
 Shirika lisilo la kiserikali la ICAP linaloendeshwa na Chuo Kikuu cha 
Columbia nchini Marekani kwa ajili ya Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya
 UKIMWI Tanzania utakaofanyika mwezi Septemba, 2016.
Akizungumza
 katika hafla ya kukabidhiana magari hayo iliyofanyika leo jijini Dar es
 Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dkt. Albina Chuwa
 amelishukuru Shirika la ICAP kwa msaada huo ambao utasaidia kupunguza 
gharama za kukodi magari kwa ajili ya kufanyia utafiti.
“Napenda
 kuchukua fursa hii kulishukuru Shirika la ICAP kwa kutupatia msaada huu
 wa magari tisa yenye thamani ya Shillingi milioni mia nane na kumi. Huu
 sio msaada mdogo kwani fedha ambazo zingetumika kukodisha magari ya 
utafiti, sasa zitatumika katika shughuli nyingine za kimaendeleo,” 
amesema Dkt. Chuwa.
Amesema
 katika kutekeleza Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), takwimu rasmi 
zinahitajika ili kupima utekelezaji wake na hivyo utafiti huu 
utakapokamilika utasaidia kutoa takwimu zitakazotumika kupima 
utekelezaji wa malengo hayo.
Kwa
 upande wake Mkurugenzi Mkaazi wa Shirika la ICAP Tanzania, Dkt. 
Fernando Morales amesema utafiti huu unalenga kupima Viashiria na 
Matokeo ya UKIMWI nchini ili kujua ni kwa kiwango gani Tanzania imepiga 
hatua katika kupambana na ugonjwa huo.
Dkt.
 Morales amesema msaada huu wa magari utasaidia kurahisisha usafiri wa 
kutoka eneo moja la utafiti hadi lingine na kuweza kusaidia katika 
upatikanaji wa taarifa muhimu za utafiti huu.
Nae
 Mkurugenzi Mkaazi wa Taasisi ya Marekani ya Kudhibiti Magonjwa – 
(Centre for Disease Control and Prevention - CDC) Dkt. Michelle Roland 
amesema kutokana na utafiti huu kufanyika kwa kutumia teknolojia ya 
kisasa ya ukusanyaji wa takwimu, kutasaidia kupunguza gharama ambazo 
zingetumika kama utafiti huu ungefanyika kwa njia ya kutumia madodoso ya
 karatasi.
Ameongeza
 kuwa utafiti huu utafanyika kwa kutumia sampuli wakilishi ya kaya 
zipatazo 15,800 Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar, na kuwafikia 
walengwa wapatao elfu arobaini (40,000) wakiwemo watoto wasiopungua elfu
 nane (8,000).
Matokeo
 yanayotarajiwa kupatikana katika utafiti huo ni pamoja na taarifa 
sahihi kuhusu hali ya maambukizi mapya ya VVU, upatikanaji wa huduma za 
tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na VVU hapa nchini na kutambua ni kwa
 kiwango gani huduma hizi zimesaidia katika kuudhibiti ugonjwa wa 
UKIMWI.
Utafiti
 huu wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania utafanywa kwa pamoja na 
Shirika la ICAP Tanzania, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, 
Wazee na Watoto kwa Tanzania Bara, Wizara ya Afya kwa Tanzania Zanzibar,
 Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali, 
Zanzibar (OCGS), Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) na Tume ya 
UKIMWI Zanzibar (ZAC).






Hakuna maoni:
Chapisha Maoni