MVUA ZINAZONYESHA ZALETA MAFURIKO JIJINI LONDON NA KUTATIZA ZOEZI LA KURA ZA KUTAKA KUJIONDOA UMOJA WA ULAYA

Mvua za msimu zinazonyesha zikiambatana na radi zimesababisha usumbufu leo asubuhi wakati wa zoezi la kura ya maoni ya kujiondoa Umoja wa Ulaya likifanyika huku mafuriko yakitokea katika sehemu ya Jiji la London na Kusini Mashariki mwa Uingereza.

Baadhi ya barabara za Jiji la London zimeelezewa kuwa zimegeuka kuwa kama mabwawa ya kuogelea kutokana na mafuriko hayo, huku usafiri wa reli ya aridhini ukitatizwa na hali hiyo mbaya ya hewa.
   Mtu akiwa ametoka kwenye gari lake kunusuru maisha yake baada ya kuingia kwenye maji 
Watu wakiokolewa kwa kutumia boti ya kujaza upepo kutoka maeneo yaliyozingirwa na maji 
Abiria wa usafiri wa treni ya aridhini wakiwa wamekwama kutokana na mvua iliyosababisha mafuriko

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni