Mgeni
 rasmi Meja Jenerali James Mwakibolwa akipata maelezo mara baada ya 
kuwasili kwenye  maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Walinda Amani wa 
Umoja wa Mataifa yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Mashujaa wa Mnazi Mmoja 
jijini Dar es Salaam 31 Mei, 2016.
Kutoka
 kushoto ni Mgeni rasmi Meja Jenerali James Mwakibolwa, Mwakilishi 
Msaidizi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Amon 
Manyama pamoja na Mkuu wa Jeshi la Akiba wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi 
wa Tanzania (JWTZ), Meja Jenerali, Elias Athanas wakitoa heshima kwa 
wimbo wa taifa wakati wa maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Walinda 
Amani wa Umoja wa Mataifa yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Mashujaa wa 
Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam 31 Mei, 2016.
Mgeni
 rasmi Meja Jenerali James Mwakibolwa akizungumza kwenye maadhimisho ya 
Siku ya Kimataifa ya Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa yaliyofanyika 
kwenye Uwanja wa Mashujaa wa Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam 31 Mei, 
2016.
Mwakilishi
 Msaidizi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Amon
 Manyama akisoma hotuba pamoja na ujumbe maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja 
wa Mataifa, Ban Ki-Moon kwenye sherehe za maadhimisho ya siku ya 
Kimataifa ya Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa yaliyofanyika kwenye 
Uwanja wa Mashujaa wa Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam 31 Mei, 2016.
Mgeni
 rasmi Meja Jenerali James Mwakibolwa akiweka shada la maua kwenye mnara
 wa mashujaa kuwakumbuka Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa walipoteza 
maisha wakiwa kazini kulinda amani ya mataifa mengine yenye machafuko 
wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Walinda Amani wa Umoja wa 
Mataifa yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Mashujaa wa Mnazi Mmoja jijini 
Dar es Salaam 31 Mei, 2016.
Mkuu
 wa Jeshi la Akiba wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), 
Meja Jenerali, Elias Athanas akiweka shada la maua kwenye mnara wa 
mashujaa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Walinda Amani wa 
Umoja wa Mataifa yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Mashujaa wa Mnazi Mmoja 
jijini Dar es Salaam 31 Mei, 2016.
Mwakilishi
 Msaidizi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Amon
 Manyama akiweka shada la maua kwenye mnara wa mashujaa kuwakumbuka 
Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa waliopoteza maisha katika oparesheni 
ya kulinda amani katika nchi zenye machafuko wakati wa maadhimisho ya 
Siku ya Kimataifa ya Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa yaliyofanyika 
kwenye Uwanja wa Mashujaa wa Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam 31 Mei, 
2016.Uwanja wa Mashujaa wa Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam 31 Mei, 2016.
Mkuu
 wa Jeshi la Akiba wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), 
Meja Jenerali, Elias Athanas akisalimiana na Mwakilishi Msaidizi Mkazi 
wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Amon Manyama mara 
baada ya kuwasili katika maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Walinda 
Amani wa Umoja wa Mataifa yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Mashujaa wa 
Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam 31 Mei, 2016. Katikati ni Afisa Habari 
wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama.
Picha
 juu na chini ni Brass Band ikiongoza gwaride maalum la askari walinda 
Amani kuingia viwanja wakati wa maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya 
Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa katika Uwanja wa Mashujaa wa Mnazi 
Mmoja jijini Dar es Salaam 31 Mei, 2016.Manyama.
Pichani
 juu na chini ni Baadhi ya viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama, 
Balozi wa nchi mbalimbali pamoja na viongozi wa Dini waliohudhuria 
sherehe za maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Walinda Amani wa Umoja wa
 Mataifa yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Mashujaa wa Mnazi Mmoja jijini 
Dar es Salaam 31 Mei, 2016.

 
Katika
 kutambua kujitolea kwa Tanzania kutoa askari wake kwenda kulinda amani 
katika nchi zingine, Umoja wa Mataifa (UN) umesema unatambua huduma 
inayotolewa na Tanzania ikiwa kama mwanachama wa UN na unafurahishwa na 
hatua iliyopo ya kuendelea kusaidia kulinda amani katika operesheni 
zinazofuatia. 
Hayo yamesemwa na Mwakilishi Msaidizi Mkazi wa 
Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Amon Manyama katika 
maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa 
ambapo kwa nchini siku hiyo iliadhimishwa Dar es Salaam katika Uwanja wa
 Mashujaa wa Mnazi Mmoja 
Manyama alisema Tanzania imekuwa 
ikijitolea kusaidia ulinzi wa amani katika mataifa mengine licha ya 
kupoteza baadhi ya wanajeshi wake lakini bado wamekuwa wakiendelea 
kujitolea kusaidia kuimarisha ulinzi wa mataifa mengine ambayo hali ya 
usalama inakuwa siyo ya uhakika. 
“Tumefurahishwa na historia ya 
Tanzania ya kuzisaidia nchi jirani kulinda amani na kutatua migogoro ya 
hapo zamani na kuziwezesha kujipatia uhuru,” alisema Manyama.
Aidha
 Manyama alisema Umoja wa Mataifa umekuwa ukijitahidi kuendelea 
kushirikiana na wanachama wake ili kwezesha upatikanaji wa amani kwa 
mataifa yote na itaendelea kutoa heshima yake kwa wanawake na wanaume 
ambao walipoteza maisha wakiwa kazini kulinda amani ya mataifa mengine. 
“Mwaka
 jana idadi ya waliokufa ilikuwa 129, walinda amani hawa walitoka katika
 nchi 50, wakiwa ni pamoja na wanajeshi, polisi, watumishi kutoka 
mataifa mbalimbali, wafanyakazi wa kujitolea wa Umoja wa Mataifa na 
watumishi wa ndani, 
“Tunapenda kutoa heshima kwa mashujaa wetu 
zaidi wanaume na wanawake milioni moja waliotumikia chini ya bendera ya 
Umoja wa Mataifa kwa majivuno, weledi tangu kuanza kwa kazi hiyo 1948,” 
alisema Manyama.
Nae mgeni rasmi katika siku hiyo, Meja Jenerali 
James Mwakibolwa aliupongeza Umoja wa Mataifa kwa jinsi wanavyofanya 
kazi na kusaidia kuokoa maisha ya watu wengi na kuahidi Tanzania 
itaendelea kutoa wanajeshi wake ili waendelee kulinda amani. 
“Tumeshatoa
 walinda amani 2,328 katika operesheni mbalimbali zilizopita na 
tutandelea kufanya kazi pamoja ili kuimarisha amani na utulivu katika 
maeneo mengine,” alisema Meja Jenerali Mwakibolwa 
 
 
 
 
  
 
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni