Afisa
 Usajili kutoka Rita Makao makuu Jijini Dar es salaam, Augustin Thomas 
Mbuya ,ambaye ndiye mtaribu wa zowezi la Kampeni ya kitoa huduma 
Rita,Akizungumza na wananchi Jijini Arusha ambapo kampeni hiyo 
imezinguliwa rasmi.
Mkuu
 wa  Wilaya ya Arusha Fadhili Nkulu,ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika 
uzinduzi wa Kampeni ya Rita , ambapo imeanza rasmi katika Wilaya ya 
Arusha Mjini na itaendelea kwa siku nne.
Muwakilishi wa Rita Mkoa wa Arusha  Janeth Mandawa.
Afisa
 Usajili kutoka Rita makao makuu Jijini Dar es salaam Joseph Mwakatobe 
akizungumza na wananchi ,akitoa maelekezo namna ya kuandika wosia na 
umuhimu wa kuhifadhi wosia.
Afisa Usajili kutoka Rita Makao Makuu  Grace Shao.
Wananchi kutoka katika Wilaya ya Arusha Mjini wakfuatilia mafunzo 
Na Mahmoud Ahmad Arusha
 wananchi wametakiwa  kuepuka dhana potofu kuwa kuandika wosia ni 
Uchuro,jambo ambalo siyo kweli bali kuandika wosia ni kuepusha usumbufu 
na migogoro kwa ndugu watakaokuwa wamebaki aidha watoto au mjane pindi mlegwa anapokuwa amekufa .
Hayo
 yamesemwa na Afisa Usajili kutoka Rita  Joseph Mwakatobe katika 
ufunguzi wa zowezi la kampeni ya kutoa huduma za Rita kwa wananchi 
,kuwapa elimu juu ya umuhimu wa kuandika wosia, namna ya kuhifadhi 
wosia.
Joseph
 amesema kuwa mara nyingi wosia ni muhimu sana kuandikwa kwasababu 
inawarahisishia wale wanaobaki kuepusha kunyimwa haki zao ,kudhulumiwa 
,Rita inawashauri wananchi kuandika wosia,kwani watu wengi hawana elimu 
ya kutosha juu ya wosia.
Kwa upande wake mkuu wa Wilaya ya Arusha Fadhili Nkulu amewahasa Rita wawaelimishe 
wananchi sheria ya mirathi pamoja mwongozo,pia wawasaidie wananchi 
kufahamu na kuelewa maeneo sahihi ya kuhifadhi wosia
Nkulu
 amesisitiza  kuwa mtu akiandika wosia ni vizuri zaidi maana ndiye 
anayejua mali zake, na pia anamfahamu mtu sahihi wa kumpatia urithi 
huo,na hii itaepusha migogoro na migongano ambayo ingeliweza kujitokeza.
Naye
 Mratibu wa zowezi la kampeni hiyo Augustin Mboya amesema kuwa lengo kuu
 la kampeni hiyo ni kutoa elimu kwa wananchi waifahamu umuhimu 
wa.kuandika wosia nakuhifadhi, watambue kuwa ile dhana ya kuwa kuandika 
wosia ni Uchuro na kujitabiria kifo ni potofu na haina mashiko yeyote 
,Pia watambue kuwa mtu anayeandika wosia lazima awe na akili timamu 
,bila kusahau kuwa wosia huandikwa kwa hiari na siyo kulazimishwa
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni