JUKWAA LA MTANDAO UBUNIFU WA KITEKNOLOJIA LA UBER LAZINDUA USAFIRI WA UBER JIJINI DAR ES SALAAM LEO.

 Meneja wa Uber Kusini mwa Sahara, Alon Lits akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa jukwaa la mtandao ubunifu wa kiteknolojia la Uber.
Baadhi ya waanzilishi na wadau usafiri wa Uber wakiwa katika uzinduzi usafiri wa uber  jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya waandishi wakiwa katika uzinduzi wa usafiri wa uber jijini Dar es Salaam leo.

JUKWAA la mtandao ubunifu wa kiteknolojia la Uber lazindua  usafiri wa Uber  jijini Dar es Salaam leo kwa lengo la urahisisha usafiri kwa wakazi wa Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Meneja wa Uber Kusini mwa Sahara, Alon Lits  amesema kuwa jukwaa la ubunifu wa kiteknolojia, Dar es Salaam inaungana na orodha ya vituo maarufu vya usafiri barani Afrika, mafanikio ya Uber katika nchi nyingi imeshazinduliwa na kuwa na mafanikio makubwa.

“Tunajivunia kuzindua Uber nchini Tanzania katika muda ambao uchumi wake unakua. Wakati miundo mbinu ya Dar es Salaam ikiwezeshwa kuwa ya viwanda, hivyo huongezeka kwa mahitaji ya usafiri nafuu, rahisi na wa kuaminika.”Amesema Lits.

Lits amesema kuwa kwa kutumia usafiri huo 
wasafiri watasafiri kwa muda muafaka ukiwa na program ya maombi ya usafiri(Application), kwa kubonyeza tu kitufe ambacho kitatoa taarifa kwa dereva aliyepo karibu pia amesema kuwa Uber husaidia watu kupata usafiri kwa kubonyeza tu kitufe pia hakuna kusubiri barabarani au kutembea maeneo jirani usiyoyajua kwa ajili kutafuta basi. 

    Amesema kuwa hakuna haja kusimamisha gari mtaani au kuwa nje kusubiri usafiri. Kwa usalama zaidi utaweza kutumia App ya Uber mahali ulipo ukisubiri gari ifike. Hii ikimaanisha hakuna haja ya kusimama barabarani kusubiri taksi au kuhangaika kutafuta kituo cha basi kilicho karibu muda wa usiku.   

    Safari hazina kificho mara dereva anapokubali ombia lako, unaona jina lake la kwanza, picha na namba ya gari yake. Pia unaweza kuangalia kama kuna abiria wengine waliofurahia huduma yake. Kwa kuongezea, dereva anaweza kuona jina lako la kwanza na alama ulizompa. Unaweza kuwasiliana na dereva, naye pia akawasiliana nawe-kupitia hii App kama kuna mkanganyiko wowote kuhusu muda wa kukuchukua. 

“Uber ni sehemu ya mageuzi makubwa duniani katika Nyanja ya usafirishaji. Dar es Salaam ipo juu, inazizima, mji unaokuwa ukiwa na vijana mahiri wenye nguvu ya kufanya kazi ambao wapo tayari kutukaribisha na kusapoti huduma yetu. Pamoja, kwa ushirikiano na mipango ya usafiri iliyopo jijini Dar es Salaam tunaweza kubadilisha sura ya usaifiri wa mjini kunufaisha abiria. Tuna furaha isiyo na kifani kwa uzinduzi huu.”amesema.

ZIARA YA KIKUNDI CHA WAFANYA BIASHARA WANAWAKE TANZANIA, NCHINI COMORO TAREHE 14 JUNI 2016

Kikundi cha wajasirimali wanawake kutoka Tanzania (Tanzania Saccos for Women Enterprenuers) kinachoongozwa na Bi. Anna Matinde Mkurugenzi wa Bodi ya Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania waliwasili nchini Comoro kwa ajili ya ziara ya siku mbili. Lengo la ziara hiyo ni kutafuta masoko kwa ajili ya bidhaa za kutoka Tanzania, pamoja na kukutana na wajasiriamali wa Komoro ili kuweza kubadilishana taarifa juu ya fursa mbalimbali za biashara kati ya Tanzania na Komoro.

Wajasirimali hao waliwasili nchini Komoro tarehe 13 Juni 2016 na kupokelewa na  Balozi wa Tanzania nchini Komoro Mhe. Chabaka F. Kilumanga. Wakati wakiwa nchini Komoro, wajumbe walipata fursa ya kukutana na wajumbe kutoka sekta binafsi ya Komoro pamoja na wa Tanzania waishio Komoro (Diaspora). Ujumbe huo ulifurahishwa sana na fursa za biashara zilizopo Komoro ambapo walielezea kuwa wapo tayari kushirikiana na Wakomoro katika kuleta bidhaa mbalimbali katika soko la Komoro.

Aidha, wajumbe walipata fursa ya kukutana na kufanya mazungumzo na Jumuiya ya Watanzania waishio Komoro (TADICO). Katika majadiliano yao, wajumbe waliweza kushaurina juu ya mikakati ya kufanya biashara nchini Komoro, ambapo Bi. Matinde aliwaaelezea wanadiaspora wasisahu pia kuekeza nyumbani kwani nako kuna fursa nyingi hivyo ni muhimu kwa wanadiaspora kuangalia namna gani na wao wanaweza kunufaika na fursa hizo.

Wajumbe pia walipata fursa ya kuonyesha na kutangaza biashara zao kwa wafanyabiashara wa Komoro ambapo walionyeshwa kuvutiwa sana na bidhaa za kutoka Tanzania. Ikumbukwe kwamba Komoro ni nchi ambayo hutegemea kwa kiasi kikubwa bidhaa zake kutoka nje. Biashara kati ya Tanzania na Komoro imekuwa ikikuwa siku hadi siku hata hivyo, bado kuna mahitaji makubwa ya bidhaa za chakula na imeonekana kuwa Tanzania ndio nchi iliyo katika nafasi nzuri kukidhi mahitaji hayo, kutokana na ukaribu wa nchi hizo kijiografia na kimila.

Sambamba na hilo, kikundi cha wajasirimali wanawake kutoka Tanzania wanatarajia kutiliana saini mkataba wa ushirikiano (Memorandum of Understanding) baina yao na vikundi mbalimbali vya wajasiriamali wa Komoro. Katika maelezo yake, Balozi wa Tanzania nchini Komoro, Mhe. Chabaka Kilumanga alieleza kuwa huu ndio wakati muafaka wa vikundi hivyo vikaanza kufanya kazi kwa pamoja na kujuana ili kuweza kuboresha na kukuza wigo wa biashara kati ya Tanzania na Komoro. Alieleza pia kuwa ubalozi utaaendelea kushirikiana na wanadiaspora iwapo watapendelea kufanya kazi kwa pamoja na wajasirimali hao.
Balozi wa Tanzania nchini Comoro, Chabaka Kilumanga akichangia mada katika warsha hiyo.
Bi. Anna Matinde, Mkurugenzi Bodi ya Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania.
Kikundi cha Wajasiriamali wanawake kutoka Tanzania wakiendelea kusikiliza mada.
Mkuu wa Utawala na Fdha Ubalizi wa Tanzania Komoro Bw.Mudrick Soragha alievaa tai nyekundu akikaribisha wageni.
Wadua wakilendelea kuangalia bidhaa kutoka Tanzania, katika ofisi za ubalozi, Moroni.
wafanyakazi wa Ubalozi katia picha ya pamoja na kikundi cha wajasiriamali wanawake kutoka Tanzania.
Wafanyakazi wa Ubalozi katika picha ya pamoja na wana Diaspora wa Komoro.
wajasiriamali wa Komoro wakiangalia bidhaa kutoka Tanzania.
Wajumbe kutoka Sekta Binafisi Komoro wakisikiliza kwa umakini mada.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni