Mbunge
 wa Jimbo la Kikwajuni ambae pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya 
Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza  na wananchi wa Jimbo
 hilo wakati wa mkutano uliofanyika katika Ofisi ya Jimbo ambapo alitoa 
taarifa juu ya watu wazima kuanzia umri wa miaka 70 kupata huduma ya 
matibabu bure. 
Wananchi
 wa Jimbo la Kikwajuni, Zanzibar  wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la 
Kikwajuni ambae pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, 
Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani) wakati  akizungumza  katika  
mkutano uliofanyika katika Ofisi ya Jimbo ambapo alitoa taarifa juu ya 
watu wazima kuanzia umri wa miaka 70 kupata huduma ya matibabu bure.
Meneja
 wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Tawi la Zanzibar, Ismail 
Kangeta, akitoa ufafanuzi juu ya huduma ya matibabu itakayoanza kutolewa
 bure kwa wananchi wa Jimbo la Kikwajuni, wakati wa mkutano uliofanyika 
Ofisi ya Jimbo.Wapili ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambae pia ni Naibu
 Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni.
Mwananchi
 wa Jimbo la Kikwajuni akisoma kipeperushi kilichotolewa na Mfuko wa 
Taifa wa Bima ya Afya ambacho kina majina ya Hospitali ambazo wafaidika 
wa huduma ya matibabu bure wanaweza kwenda kupata huduma hiyo wakati wa 
mkutano uliofanyika Ofisi ya Jimbo hilo Kikwajuni Zanzibar. 
Mbunge
 wa Jimbo la Kikwajuni ambae pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya 
Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(kulia), akimsikiliza mmoja wa 
wananchi wa Jimbo hilo mara baada ya kutoa muda wa kusikiliza kero 
mbalimbali za wananchi  wakati wa mkutano uliofanyika Ofisi ya Jimbo 
hilo, Zanzibar.
Mwakilishi
 wa Jimbo la Kikwajuni, Nassor Salim Jazeera (kulia), akimsikiliza 
mwananchi wa Jimbo hilo mara baada ya kutoa muda wa kusikiliza kero 
mbalimbali za wananchi  wakati wa mkutano uliofanyika Ofisi ya Jimbo 
hilo, Zanzibar.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni