WAGENI KATIKA MICHUANO YA EURO TIMU YA ICELAND YAIDUWAZA URENO KWA KUTOA SARE

Timu ya taifa ya Iceland imepata pointi muhimu katika mchezo wao wa kwanza katika michuano ya Euro 2016 dhidi ya Ureno katika kundi F, baada ya kutoka sare ya 1-1.

Katika mchezo huo Luis Nani aliifungia Ureno goli na kuifanya iongoze lakini Iceland ilipambana kiume na kusawazisha kupitia kwa Birkir Bjarnason.

Awali Cristiano Ronaldo alishuhudia mpira wake aliopiga kwa kichwa ukiokolewa huku nao Iceland wakipoteza goli dakika za mwisho baada mpira uliopigwa na Alfred Finnbogason kuokolewa.
             Birkir Bjarnason akisawazisha goli na kuiacha Ureno ikiwa na mshangao
                    Cristiano Ronaldo akiinamisha kichwa chini baada ya kuisha mchezo huo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni