Hifadhi ya Taifa ya  wanyamapori 
ya Selous iliyopo kusini mwa Tanzania imepoteza asilimia  90 ya Tembo 
waliopo katika hifadhi hiyo kutokana na ujangili uliokithiri.
Ripoti ya mfuko wa hifadhi ya 
wanyapori na mazingira duniani (WWF) imesema kufikia mwaka 2022 kama 
hakutakuwa na hatua zozote kali zitakazochukuliwa kuwalinda tembo 
kutokana na ujangili  basi  watatoweka kabisa.
Ripoti hiyo imeendelea kusema 
kuwa kwa miaka ya nyuma mbuga ya Selous ilikuwa mojawapo ya mbuga kubwa 
kabisa katika bara la afrika yenye tembo wengi ambapo kulikuwa na tembo 
zaidi ya 110000 lakini kutokana na ujangili uliokithiri katika miaka 40 
iliyopita tembo hao wamepungua na kubakia 15000 tu uku mahitaji makubwa 
ya pembe za ndovu katika nchi ya china yakitajwa na ripoti hiyo kuwa 
kichocheo kikubwa cha ujangili na mauaji ya idadi kubwa ya tembo hao.
Aidha ripoti hiyo inaonyesha 
hathari kubwa  kiuchumi itakayotokea  kutokana na kwamba Tanzania 
kupitia Mbuga ya Selous inaingiza dola milioni 6 kwa mwaka 
ikilinganishwa na Sekta ya Viwanda inayochangia dola bilioni 5 katika 
pato la Taifa.
Pamoja na Hayo Serikali ya awamu 
ya tano  kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imeweka mikakati 
madhubuti ikiwemo kuunda kitengo chake cha intelijensia na kuunda kanda 
nane za doria za ushirikiano katika mifumo ya ikolojia ya mbuga ya 
Selous ambayo imeanza kuwa na mafanikio  ikiwa ni pamoja na kushirikiana
 na wadau wa uhifadhi kuwezesha upatikanaji wa vitendea kazi na zana kwa
 ajili ya doria.
Mwaka 2014 Shirika la Kimataifa 
la Sayansi,Elimu na Utamaduni la umoja wa mataifa(UNESCO) liliiweka 
Mbuga ya Selous katika Urithi wa asili ulio hatarini Duniani.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni