
Siku
 moja baada ya kifo cha dada wa bilionea Erasto Msuya, Aneth imebainika 
kuwa msaidizi wa ndani aliondoka saa sita mchana kwa kuacha funguo 
nyumba ya jirani.
Akizungumza nyumbani.
dada
 wa marehemu, Mbezi Juu, mama mdogo wa marehemu Lilian Benjamin alisema 
msaidizi huyo alimpigia simu bosi wake mchana na kumwambia anaondoka na 
hataendelea na kazi.
Alisema
 marehemu alilazimika kuomba ruhusa mapema kazini ili arudi nyumbani 
kwake Kibada lakini ilimlazimu kukaa nje ya nyumba kwa saa mbili baada 
ya kufika saa tisa alasiri na kukuta mlango umefungwa.
Mama
 huyo alisema baada ya kusubiri kwa muda aliwauliza majirani wakamweleza
 kuwa walipelekewa funguo na mwanafunzi wasiyemfahamu akadai kuwa 
alipewa na dada mmoja aliyemuelekeza aipeleke nyumba hiyo.
Haifahamiki mpaka sasa mahali alipo mfanyakazi huyo anayedaiwa kuwa mwenyeji wa Arusha.
Dada mkubwa wa marehemu, Happy Msuya alisema marehemu aliwaeleza mambo hayo baada ya kupigiwa simu na msichana huyo wa kazi.
Dada
 mwingine wa marehemu ambaye ni wa nne kuzaliwa kati ya watoto saba wa 
Elisaria Msuya, Ester, alisema wauaji hao hawakuwa na nia ya kuiba, bali
 ni kuua kwa sababu hawakuchukua kitu chochote zaidi ya televisheni 
ambayo nayo waliitupa mbali na nyumbani.
Ester
 alisema mara ya mwisho kuonana na marehemu ilikuwa Mei saba 
walipokutana benki na mazungumzo yao yalihusu hali ngumu ya maisha. 
Alisema hakuwahi kumwambia kama ana ugomvi na mtu kwa sababu alikuwa 
mpole na msiri.
Akielezea
 tukio hilo alisema inaonekana kulikuwa na purukushani kubwa chumbani 
kwa sababu besela la kitanda lilikuwa limevunjika na neti ilikuwa 
imetoka, huku nyaraka zikiwa zimepekuliwa na kusambazwa karibu kila kona
 ya chumba.
“Walikuja
 kuua, kuna kitu walikuwa wanatafuta katika nyaraka pia, ooh... Aneth 
umekufa kinyama, umechinjwa kama mnyama,” Ester alishindwa kuendelea na 
kuanza kulia na baadaye kidogo alisema wauaji walimkata marehemu koromeo
 lakini hawakutenganisha kichwa na kiwiliwili.
Simulizi ya mtoto 
Mtoto
 wa marehemu mwenye umri wa miaka minne ambaye alikuwa akiishi na mama 
yake alisema: “Walikuja watu watano weusi usoni, wakanifanya na kitu 
shii usoni, nikalala kwenye kiti mbu wameniuma hadi niliposikia gari la 
shule likiita pipii, nikaamka na nikamuamsha mama anivalishe nguo za 
shule lakini akakataa kuamka, ”alisema mtoto huyo na kuongeza.
“Nikavaa
 mwenyewe nguo za shule na nikamwambia mama nitaendaje shule huku 
sijafanya “Home work” lakini mama hakujibu, mbu walining’ata pale kwenye
 kochi nilipolala, nikatoka nje nikakuta gari limeshaondoka, nikaenda 
kwa mama Salum,” alisema.
Alisema alienda huko akale kwa sababu njaa ilikuwa inamuuma hakula jana yake baada ya ‘wageni’ hao kuja na yeye kulala.
Alieleza
 kuwa alipowaambia mama yake hamjibu amelala tu alirudi na dada ambaye 
amemsahau jina kutoka hapo kwa mama Salum ambaye alipofika nyumbani kwao
 na alipomuona mama yake alianza kupiga kelele.
Ester alisema mwili wa marehemu utasafirishwa Jumatatu ijayo kuelekea kijijini kwao Kairo, Simanjiro mkoani Manyara.
Mtu
 wa karibu na familia ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema mbali ya
 kaka yao Erasto kuuawa kwa risasi, dada yao Ester akiwa na mumewe 
katika Baa ya Hongera, Dar es Salaam alipigwa risasi na kunusurika kufa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni