Mke 
wa Rais Mama Janeth Magufuli akikabidhi sehemu ya vyakula hivyo kwa 
Mwenyekiti wa Kituo cha Charambe Islamic Center Dkt. Haruni Kondo 
aliyepokea kwa niaba ya vikundi vigine vinne. Mke wa Rais amekabidhi 
mchele kilo 500, sukari kilo 500 na tende kilo 28, tukio hilo 
limefanyika katika ofisi ya Mke wa Rais Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Khalifa
 wa Zawiyatul lqadiria, Abas Hamdan watatu kutoka kulia akiongoza dua ya
 kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na viongozi 
wengine wakuu wa serikali mara baada ya tukio la kukabidhi vyakula 
hivyo. Wengine katika picha ni Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli, Mke wa 
Waziri mkuu Mama Marry Majaliwa pamoja na viongozi mbalimbali vya 
vikundi vya kulea watoto yatima na watu waishio kwenye mazingira magumu.
 Mke 
wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwa na  mke wa Waziri Mkuu Mama Marry 
Majaliwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa vikundi vya 
kulea watoto yatima na watu waishio kwenye mazingira magumu. Tukio hilo 
limefanyika katika Ofisi za Mke wa Rais Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Mke 
wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana na Mama Mlezi wa Kituo cha 
Charambe Islamic Center Asile Zahali mara baada ya kukamilika zoezi la 
utoaji wa vyakula mbalimbali kwa vituo vinne vya kulea watoto na watu 
waishio kwenye mazingira magumu. 
Mke wa
 Rais Mama Janeth Magufuli akiwa na mke wa Waziri Mkuu Mama Marry 
Majaliwa akizungumza na viongozi mbalimbali wa vituo hivyo kabla ya 
kuwakabidhi vyakula hivyo katika Ofisi yake Ikulu jijini Dar es Salaam. 
PICHA NA IKULU
MKE wa
 Rais Mama Janeth Magufuli amekabidhi chakula kwa ajili ya futari wakati
 huu wa mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwa vituo vinne vya kulea 
watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu Jijini Dar es 
salaam.
Vyakula
 hivyo vimekabidhiwa leo tarehe 18 Juni, 2016 katika ofisi ya Mke wa 
Rais Ikulu Jijini Dar es salaam vimejumuisha Mchele kilogramu 500, 
Sukari kilogram 500 na Tende kilogramu 28.
Akizungumza
 mara baada ya kukabidhi vyakula hivyo, Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli
 aliyeongozana na Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa amewatakia heri 
Waislamu wote katika mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani na kuwasihi 
waendelee kuliombea Taifa amani na utulivu.
 (“Tunawatakia
 mfungo mwema wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, katika kipindi hiki 
tunawaomba mzidi kuiombea nchi yetu amani, viongozi wetu wa nchi na 
watanzania wote kwa ujumla, nchi ikiwa na amani ndio mambo mengi mazuri 
yanaweza kufanyika”)
Kwa 
niaba ya vituo vilivyopatiwa vyakula hivyo, Mwenyekiti wa Kituo cha 
Charambe Islamic Center Dkt. Haruni Kondo amemshukuru Mke wa Rais kwa 
kutoa vyakula hivyo na ameeleza kuwa kitendo hicho kinaonesha mshikamano
 na ushirikiano walionao watanzania wote bila kujali tofauti ya dini, 
kabila wala maeneo wanayotoka.
 (“Kwa
 hiyo ndugu zangu mna imani ya kikristo lakini mnatambua waislamu ni 
ndugu zenu, wote tunajenga nyumba moja, mshikamano ndio tunu 
tuliyoachiwa na Baba yetu wa Taifa, leo mmeguswa kuona wenzenu tunafanya
 ibada na nyinyi mmeingia kwenye ibada, sasa ibada ya kutoa ni ibada 
kubwa sana, sio nchi nyingi katika Afrika zinafanya kitendo hiki, watu 
hawaelewi, ni nchi chache sana ambazo imani moja inaunga mkono imani 
nyingine, lakini sisi waislamu tunalitambua hili hata toka kipindi 
ambacho mtume wetu SWA anapigana kusimika dini hii kwa waumini alipata 
nusura kwa wakristo”)  
Vituo vilivyokabidhiwa vyakula hivyo ni Charambe Islamic Center, Tasofe Lqadiria, Nur Twarigatu Lqadiria na Zawiyatul Lqadiria.





Hakuna maoni:
Chapisha Maoni