Mkuu
 wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadicky akizungumza wakati wa 
kukabidhi Madawati 50 yaliyotolewa na benki ya Azania tawi la Moshi kwa 
shule ya msingi Mnazi katika manispaa ya Moshi ikiwa ni kuunga mkono 
agizo la rais John Magufuli la kupunguza tatizo la Madawati kwa shule za
 msingi.
Meneja
 wa benki ya Azania tawi la Moshi,Hajira Mmambe akizungungumza juu ya 
hatua ya benki hiyo kuunga mkono agizo la rais John Magufuli la kutatua 
tatizo la Madawati kwa shule za msingi nchini. 
Mkuu
 wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga akizungumza katika hafla hiyo ya 
kukabidhi Madawati 50 yaliyotolewa na benki ya Azania tawi la Moshi kwa 
shule ya msingi Mnazi.
Baadhi ya wafanyakazi wa benki ya Azania tawi la Moshi wakifuatilia hafla hiyo.
Kaimu
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi,Deodatus Nyoni 
akizungumzia juu ya upungufu wa Madawati 701 ulipo sasa kwa shule za 
msingi na Sekondari.
Meneja
 wa benki ya Azania tawi la Moshi, Hajira Mmambe akimkabidhi mkuu wa 
mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadicky Madawati yaliyotolewa na benki 
hiyo. Wengine ni wanafunzi wa shule ya msingi Mnazi.
Mkuu
 wa mkoa wa Kilimanjaro, Said Mecky Sadicky (katikati) akiwa ameketi 
kwenye moja ya Madawati yaliyotolewa na benki ya Azania tawi la Moshi 
kwa shule ya msingi Mnazi, kulia ni mkuu wa wilaya ya Moshi, Novatus 
Makunga na kushoto ni meneja wa Azania benki tawi la Moshi, Hajira 
Mmambe. 
Wanafunzi katika shule ya msingi Mnazi wakiwa wamekaa katika Madawati yaliyotolewa na benki ya Azania tawi la Moshi. 
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadicky, akisalimiana na wanafunzi katika shule hiyo.
Mstahiki
 Meya wa manispaa ya Moshi, Raymond Mboya akitoa neno la shukrani mara 
baada ya kupata msaada wa Madawati kutoka Benki ya Azania tawi la 
Moshi. 
Mstahiki
 Meya wa manispaa ya Moshi, Raymond Mboya akiteta jambo na Meneja wa 
benki ya Azania tawi la Moshi, Hajira Mmambe wakati wa hafla ya 
kukabidhi wa Madawati kwa shule ya msingi Mnazi. 
Mkuu
 wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Mecky Sadicky akisalimiana na wafanyakazi 
wa benki ya Azania tawi la Moshi pamoja na watumishi wa halmashauri ya 
Manispaa ya Moshi.

















Hakuna maoni:
Chapisha Maoni