Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Charles Mwijage.
Waziri
 wa Viwanda  Biashara na uwekezaji Charles Mwijage amelitaka shirika la 
viwango Tanzania TBS pamoja na shirika la ushindani wa haki kuhakisha 
ifikapo July moja  wanamaliza bidhaa zote bandia na  zilizo chini ya  
viwango na wasipo fanya hivyo ajira zao zitafutwa mara na bidhaa hizo 
kuteketezwa.
Tamko
 hilo amelitoa waziri Charles Mwijage lwakati alipokuwa anatembelea 
kujionea bidhaa zinazozalishwa hapa nchini na kusibitishwa ubora wake 
katika siku ya viwango afrika ambapo kwa upande wa kampuni ya cement ya 
Dangote ,Afisa mkuu masoko Joel Laizer amemhakishi a waziri ubora wa 
cement zinazozalishwa na kampuni hiyo.
Wakati
 huo huo kampuni ya Azania pamoja na Azam kwa kupitia kwa maofisa wao 
akiwemo Maofisa masoko  afisa mkuu wa masoko wa AZANIA  Naifa Abubakari 
pamoja Ibrahimu Masome wa AZAM  wamemuhakikishia waziri wa viwanda 
biashara na uwekezaji kuwa wao wamejipanga vizuri kuhakisha wanatoa 
bidhaa zinazokidhi viwango  bora na zenye ushindani na masoko kote 
duniani
Aidha
 kwa upande wao kampuni ya kuzalisha Bodi za magari ya kitalii pamoja na
 vyuma vya kujengea Maghala ya viwanda afisa biashara Mohan Krishan 
amemwambia waziri kuwa wao kama kampuni ya HANSPAUL  wataakikisha 
wanatengeneza bidhaa bora zenye bei nafuu.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni