RAIS MAGUFULI AOMBWA KUWACHUKULIA HATUA KALI MAWAZIRI WOTE WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI AMBAO HAWAJAHUDHURIA VIKAO VYA BUNGE LA BAJETI LA JUMUIYA HIYO

                                                  Na Mahmoud Ahmad,Arusha

BUNGE la Jumuiye ya Afrika Mashariki limemwagiza Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Magufuli kuwachukulia hatua kali mawaziri wote wanaohusika katika wizara zihususuzo Jumuiya hiyo kwa kutokuhudhuria vikao vya Bunge hilo.

Pamoja na hilo pia imebainika kuwa kutokuhudhuria kwao kwenye vikao hivyo ndio chanzo cha wananchi wa Jumuiya hiyo kutojua mambo mengi yahusuyo Jumuiya ya Afrika Mashariki.
 

Hayo yamesemwa kwa masikitiko makubwa na mwenyekiti wa kamati ya sheria katika Bunge la Afrika Mashariki ambaye pia ni mbunge kutoka nchini Kenya,Peter Mathuki alipokuwa akielezea masikitiko yake kuhusiana na mawaziri hao kushindwa kutikmiza wajibu wao.

Mathuki ameeleza kuwa tatizo lililopo kwa wananchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki la kutokuijua vema Jumuiya hiyo ni kutofahamishwa mambo mengi yahusuyo Jumuiya na watu wenye wajibu huo ni mawaziri husika.

Ameongeza kuwa kwa kipindi kirefu sasa mawaziri hao hawajatokea wala kushiriki vikao vya Bunge hilo japo wanatakiwa kufanya hivyo ili kuweza kufikisha ujumbe kwa wananchi ambao ndio walengwa wakubwa katika kujua mambo mbalimbali ya nchi zao.

Mathuki amedhamiria kuletamuswada katika Bunge hilo utakaoazimia kuwakataa na kuwafukuza Bungeni hapo mawaziri wote hao ambao kwa mujibu wake anadai wameonyesha utovu wa nidhamu kwenye Bunge hilo.

Katika suala jingine, Mathuki amezungumzia umuhimu wa kutumia lugha ya kiswahili katika vikao mbalimbali vya Bunge hilo ambapo pia imeonekana ni sababu tosha kwa wananchi wengi kutojua mambo mengi ndani ya Jumuiya kutokana na ugumu wa lugha ya kiingereza inayotumika na kongeza kuwa inatakiwa kutumika sasa.

Amezitaka nchi zote kwa kutambua na kukienzi kiswahili wanatakiwa kuhakikisha kinakuwa ni lugha ya kila Taifa na itumike katika kufundishia mashuleni na hata katika matumizi ya kila siku ya lugha hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni