Na Mahmoud Ahmad,Arusha 
BUNGE
 la Jumuiye ya Afrika Mashariki limemwagiza Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo 
ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Magufuli 
kuwachukulia hatua kali mawaziri wote wanaohusika katika wizara 
zihususuzo Jumuiya hiyo kwa kutokuhudhuria vikao vya Bunge hilo. 
Pamoja
 na hilo pia imebainika kuwa kutokuhudhuria kwao kwenye vikao hivyo ndio
 chanzo cha wananchi wa Jumuiya hiyo kutojua mambo mengi yahusuyo 
Jumuiya ya Afrika Mashariki. 
 
Hayo
 yamesemwa kwa masikitiko makubwa na mwenyekiti wa kamati ya sheria 
katika Bunge la Afrika Mashariki ambaye pia ni mbunge kutoka nchini 
Kenya,Peter Mathuki alipokuwa akielezea masikitiko yake kuhusiana na 
mawaziri hao kushindwa kutikmiza wajibu wao. 
Mathuki
 ameeleza kuwa tatizo lililopo kwa wananchi wa Jumuiya ya Afrika 
Mashariki la kutokuijua vema Jumuiya hiyo ni kutofahamishwa mambo mengi 
yahusuyo Jumuiya na watu wenye wajibu huo ni mawaziri husika. 
Ameongeza
 kuwa kwa kipindi kirefu sasa mawaziri hao hawajatokea wala kushiriki 
vikao vya Bunge hilo japo wanatakiwa kufanya hivyo ili kuweza kufikisha 
ujumbe kwa wananchi ambao ndio walengwa wakubwa katika kujua mambo 
mbalimbali ya nchi zao. 
Mathuki
 amedhamiria kuletamuswada katika Bunge hilo utakaoazimia kuwakataa na 
kuwafukuza Bungeni hapo mawaziri wote hao ambao kwa mujibu wake anadai 
wameonyesha utovu wa nidhamu kwenye Bunge hilo. 
Katika
 suala jingine, Mathuki amezungumzia umuhimu wa kutumia lugha ya 
kiswahili katika vikao mbalimbali vya Bunge hilo ambapo pia imeonekana 
ni sababu tosha kwa wananchi wengi kutojua mambo mengi ndani ya Jumuiya 
kutokana na ugumu wa lugha ya kiingereza inayotumika na kongeza kuwa 
inatakiwa kutumika sasa. 
Amezitaka
 nchi zote kwa kutambua na kukienzi kiswahili wanatakiwa kuhakikisha 
kinakuwa ni lugha ya kila Taifa na itumike katika kufundishia mashuleni 
na hata katika matumizi ya kila siku ya lugha hiyo.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni