RAIS DKT MAGUFULI AWAAPISHA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI WAPYA IKULU DAR ES SALAAM LEO

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Bi. Angela Kairuki kuwa Waziri wa Madini Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Hamisi Kigwangwalla  kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii  Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha  Mhe. Suleiman Saidi Jafo  kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa) Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Mhe. Kangi Lugola kuwa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira)  Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt Mary Machuche Mwanjelwa kuwa Naibu Waziri wa Kilimo Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Mhe. Stella Alex Ikupa kuwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye ulemavu)  Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Mhe. Juliana Shonza  kuwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017.
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Mhe. Stephen Kagaigai kuwa Katibu wa Bunge Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassima Majaliwa, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma, Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai Ikulu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi katika picha ya kumbukumbu na Mawaziri na Naibu Mawaziri baada ya hafla ya kuapishwa  jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na aliyekuwa  Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashilila huku Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma na Katibu wa Bunge Mpya Mhe. Stephen Magaigai wakianfalia Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiendesha kikao cha Baraza la Mawaziri mara tu baada ya kuwaapisha Mawaziri na Naibu Mawaziri wapya  Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba baada ya Mawaziri na Naibu Mawaziri wapya  kuapishwa Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi) Mhe. George Mkuchika huku Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassima Majaliwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wakiangalia baada ya hafla ya kuapishwa  Mawaziri na Naibu Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Naibu  Waziri wa Nchi Ofisi Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe.Kangi Lugola huku  Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassima Majaliwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wakiangalia baada ya hafla ya kuapishwa  Mawaziri na Naibu Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Naibu Waziri wizara ya Nishati Mhe. Subira Hamisi Mgalu huku Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassima Majaliwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wakiangalia baada ya hafla ya kuapishwa  Mawaziri na Naibu Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Naibu Waziri wa Kilimo Dklt. Mary Mwanjelwa huku Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassima Majaliwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wakiangalia baada ya hafla ya kuapishwa  Mawaziri na Naibu Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Naibu Waziri  Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega  huku Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassima Majaliwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wakiangalia baada ya hafla ya kuapishwa  Mawaziri na Naibu Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe. Jumaa Hamidu Aweso huku Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassima Majaliwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wakiangalia baada ya hafla ya kuapishwa  Mawaziri na Naibu Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na  Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye ulemavu) Mhe. Stella Alex Ikupa huku Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassima Majaliwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wakiangalia baada ya hafla ya kuapishwa  Mawaziri na Naibu Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na  Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo Mhe. Juliana Shonza huku Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassima Majaliwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wakiangalia baada ya hafla ya kuapishwa  Mawaziri na Naibu Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na  Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde   huku Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassima Majaliwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wakiangalia baada ya hafla ya kuapishwa  Mawaziri na Naibu Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 9, 2017. Picha na IKULU

WAZIRI MBARAWA AWATAKA WAFANYAKAZI KUFANYA KAZI KWA UADILIFI

 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Atashasta Nditiye (Wa pili kulia) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Eng. Joseph Nyamhanga (Kushoto) wakati alipokaribishwa katika ofisi za Wizara leo Jijini Dar es Salaam, Kushoto ni Katibu Mkuu Sekta ya Uchukuzi Dkt. Leonard Chamuriho na Wa pili kushoto Katibu Mkuu Dkt. Maria Sasabo (Sekta ya Mawasiliano).
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawailiano, Prof. Makame Mbarawa (Kushoto), akisalimiana na Naibu Waziri Eng. Atashasta Nditiye (Kulia), wakati alipomtembelea Waziri Mbarawa ofisini kwake leo Jijini Dar es Salaam. Wa pili kulia ni Katibu Mkuu Sekta ya Uchukuzi Dkt Leonard Chamuriho 
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawailiano, Profesa Makame Mbarawa (Kulia) akisalimiana na Naibu Waziri hiyo Mhe. Elias Kwandikwa wakati alipomtembelea Waziri Mbarawa ofisini kwake leo Jijini Dar es Salaam. 
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawailiano, Prof. Makame Mbarawa (Katikati) akizungumza na Manaibu Waziri wa Wizara hiyo Eng. Atashasta Nditiye (Wa pili kulia) na Mhe. Elias Kwandikwa (Wa tatu kulia), wakati walipomtembelea ofisini kwake leo Jijini Dar es Salaam.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Atashasta Nditiye (aliyesimama) akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa (Wa kwanza kulia), mara baada ya kuapishwa Jijini Dar es Salaam leo. 
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Atashasta Nditiye (aliyesimama) akieleza jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawailiano, Prof. Makame Mbarawa (Wa kwanza kulia), leo Jijini Dar es Salaam kabla ya kikao kazi na Makatibu Wakuu wa wizara na baadhi ya Watendaji waliopo jiji Dar es Salaam leo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawailiano, Profesa Makame Mbarawa (Kulia) akiwakabidhi manaibu Waziri wa Wizara hiyo Eng. Atashasta Nditiye (Kulia) na Mhe. Elias Kwandikwa wakati (Katikati) vitabu vya bajeti ya mwaka wa fedha 2017/18 ya Wizara hiyo kama mwongozo wa utendaji kazi mara baada ya kuapishwa jijini Dar es Salaam leo.


Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Prof. Makame Mbarawa amewataka wafanyakazi wote katika sekta ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kufanya kazi kwa uadilifu na ushirikiano katika kuwahudumia Watanzania ili kufikia malengo ya Wizara.

Prof. Mbarawa ameyasema hayo jana katika mapokezi ya Manaibu Mawaziri wapya wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ofisini Jijini Dar Es Salaam baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt John Pombe Magufuli Ikulu Dar es Salaam.

“Mimi nafurahi sana kufanya kazi katika Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa sababu mimi na wafanyakazi tuko katika timu moja; tunafanya kazi kwa pamoja na kwa ushirikiano. Katika kipindi cha miaka miwili tumefanikiwa kufikia malengo mbali mbali ya serikali mfano ujenzi wa reli ya kisasa na barabara “ Mhe. Mbarawa amesema.

 Akiwakaribisha Manaibu Mawaziri hao katika Wizara hiyo Prof. Mbarawa amesema yeye pamoja na wafanyakazi wote wa wizara wamefurahi kupata mawaziri wapya ambao watafanya nao kazi kwa pamoja katika wizara hiyo.
 “Sisi kama viongozi tunapaswa kuwa mfano katika utendaji wetu wa kazi ili kujenga imani na umoja na wafanyakazi wetu. Tunapaswa kufanya kazi kwa uadilifu, ushirikiano na umoja kwani haya ndio masuala ya msingi katika utendaji kazi,” Prof. Mbarawa amesema .

Waziri amesema Wizara hiyo imefanya kazi nzuri na hili limewezekana kwa sababu sisi kama wizara tumezingatia maadili ya msingi katika utendaji wa kazi zetu, kuna timu nzuri ya watalaam ambao ni wachapa kazi, wana moyo wa kujituma na kazi zote walizozifanya zina matokeo mazuri. 

Kazi nzuri imefanyika, nawaomba  waheshimiwa manaibu mawaziri tufanye kazi kama timu moja na watalaam wetu ili tuweze kufikia malengo ambayo tumejiwekea katika wizara yetu, amesisitiza Waziri Mbarawa.Kwa upande wake Naibu Waziri anayeshughulikia Eng. Atashasta Nditiye anayeshughulikia Sekta ya Uchukuzi na Mawasiliano amesema kuwa amejipanga kufanya kazi na kulete matokea chanya na kwa maendeleo ya nchi.

“Nipo tayari kufanya kazi itakayoleta mabadiliko, tutaboresha miundombinu ili kuchochea kasi ya ukuaji wa viwanda na kila nitakachofanya ni utekelezaji wa yale amabayo Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli anayatarajia,” amesema mhandisi Nditiye.



Hii ni mara ya kwanza kwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli kufanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri tangu serikali yake iingie madarakani Novemba 2015.

DK.MABODI ATOA NASAHA NZITO KWA MAKADA WA CCM

Na Is-haka Omar, Zanzibar.
CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar viongozi watakaochaguliwa kupitia Uchaguzi wa ngazi ya Wilaya ya Kaskazini “B” kichama Unguja kuwa mstari wa mbele kukemea vikali tabia ya makundi na safu za uongozi zenye nia ya kuhatarisha uhai wa CCM katika Wilaya hiyo.
Wito huo umetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdalla Juma Mabodi wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Wilaya hiyo wa kuwachagua viongozi wa nafasi mbali za ngazi hiyo huko Mahonda katika ukumbi wa Ofisi ya CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Alisema matarajio ya CCM ni kuona viongozi wanaochaguliwa katika uchaguzi huo wanachukia kwa vitendo uwepo wa baadhi ya makada wanaoendekeza makundi, Safu na rushwa ndani ya chama hicho.
Dk.Mabodi alieleza kwamba msimamo wa CCM ni kuhakikisha Katiba, kanuni na miongozo inasimamiwa na kufuatwa ipasavyo ili kupata viongozi na makada wenye uwezo wa kuendeleza mafanikio ndani ya chama hicho kwa miaka mitano ijayo.
Aidha aliwambia viongozi watakaopata nafasi ya kuchaguliwa kupitia uchaguzi huo wahakikishe wanajenga ngome imara ya kisiasa katika wilaya hiyo sambamba na kuwashawishi wapinzani waliomo katika Wilaya hiyo kujiunga na CCM kwani ndio chama pekee kinachojali maslahi ya wananchi wote.
“Baada ya kukamilika uchaguzi huu wa ndani ya chama chetu tuna jukumu jingine la kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa Dola wa mwaka 2020 pamoja na kusimamia Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015/2020 kama tulivyoahidi kwa wananchi.”, alisisitiza Dk. Mabodi.
Aliwasihi makada watakaochaguliwa kuwa viongozi kushirikiana vizuri na makada wenzao ambao hawakupata fursa ya kuchaguliwa kwa lengo la kuendeleza misingi imara ya ukomavu wa kisiasa na Demokrasia iliyotukuka.
Hata hivyo aliwapongeza wanachama hasa makada waliogombea nafasi mbali mbali kwa kutofanya kampeni za fujo, vurugu na kuchafuana hali aliyosema kuwa inaonyesha ishara njema ya kukamilika kwa uchaguzi huo bila kujitokeza mapungufu.
Aidha alisema chama hicho baada ya uchaguzi huo kinakusudia kutoa mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi wa ngazi mbali mbali za chama hicho ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.
Naibu Katibu Mkuu huyo Dk. Mabodi aliwataka wanachi hasa wanachama wa chama hicho kupuuza kauli zinazotolewa na Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif za kuwa ataapishwa kuwa Rais wa Zanzibar jambo ambalo haliwezi kutokea kwani Rais halali wa Zanzibar ni Dk. Ali Mohamed Shein mpaka mwaka 2020.
Katika uchaguzi huo nafasi zinazowaniwa ni Mwenyekiti wa Wilaya , Katibu wa Siasa na Uenezi, nafasi ya mkutano Mkuu wa Mkoa , nafasi ya Mkutano Mkuu wa taifa pamoja na nafasi ya Halmashauri kuu ya CCM Wilaya.
-Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk. Abdalla Juma Mabodi akifungua Mkutano Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini "B" huko Mahonda katika ukumbi wa CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja uliofanyika leo.
Baadhi ya Wajumbe wa mkutano Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini "B" wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa CCM Dk. Mabodi huko Mahonda.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Mjumbe wa Mkutano huo Balozi Seif Ali Idd akipiga kura katika uchaguzi wa CCM ngazi ya Wilaya ya Kaskazini "B" uliofanyika leo huko Mahonda katika ukumbi wa CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja uliofanyika leo.

MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI WAWAJENGEA UWEMO MADAKTARI KANDA YA ZIWA

Na Binagi Media Group

Mfuko wa fidia kwa wafanyakazi WCF umetoa semina kwa Waganga na Madkatari Kanda ya Ziwa ili kuwajengea uwezo wa kufanya tathimini sahihi kwa wafanyakazi wanaoumia kazini kwa ajili ya kulipwa fidia.

Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Masha Mshomba amesema ujio wa mfuko huo ni faraja kwa waajiri na waajiwa kwani umelenga kuondoa kero walizokuwa wakizipata wafanyakazi baada ya kuumia kazini hivyo semina hiyo itasaidia madaktari hao kufanya tathmini za malipo kwa haraka zaidi.
 

Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa semina hiyo, amewasihi waajiri wote kujiunga na mfuko huo na kwamba ni kosa kisheria kwa waajiri wanaokwepa kujiunga na kutoa michango kwa ajili ya waajiriwa wao.

Dkt.Furaha Munema kutoka hospitali ya Rufaa mkoani Mwanza Sekou Toure ambaye ni mmoja wa madaktari walionufaika na semina hiyo ya siku tano kuanzia leo, amebainisha kwamba itawasaidia kutenda haki wakati wa tathmini kwa mfanyakazi atakayekuwa ameumia kazini.

Naye mmoja wa wawezeshaji wa semina hiyo Dkt.Robert Mhina ambaye ni daktari bingwa upasuaji mifupa kutoka hospitali ya taifa Muhimbili kitengo cha mifupa MOI, amesema mfuko wa fidia WCF umesaidia kuondoa usumbufu uliokuwepo hapo awali baada ya wafanyakazi kuumia kazini.

Mfuko wa fidia kwa wafanyakazi WCF unatoa huduma ya matibabu, malipo ya ulemavu wa muda, ulemavu wa kudumu, malipo kwa anayemhudumia mgonjwa, msaada wa mazishi, malipo kwa wategemezi ikiwa mfanyakazi atafariki dunia, ukarabati pamoja na ushauri nasaha.

Mgeni rasmi, Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella (katikati), akiwa pamoja na viongozi wa WCF.

Baadhi ya Waganga na Madaktari wanaoshgiriki semina hiyo katika ukumbi wa Kenki Kuu BOT Jijini Mwanza.

Picha zaidi bonyeza Binagi Media Group

WAFANYAKAZI WA BIMA YA BRITAM WATOA MSAADA KATIKA KITUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA CHA CHAKUWAMA.

Mkuu wa operesheni wa Bima ya Britam, Farai Dogo akikabidhi msaada wa vitu mbalimbali katika kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWAMA kilichopo Sinza jijinini Dar es Salaam ikiwa ni kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka wiki ya kwanza Oktoba duniani Kote.
Wafanyakazi wa bima ya Britam wakiwa katika picha ya pamoja wakati wakikabidhi vitu mbalimbali kwa kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWAMA kilichopo sinza jijini Dar es Salaam.
Katibu mtendaji wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha CHAKUWA, Hasan Khamis akizungumza na wafanyakazi wa bima ya Britam na kuwaelezea historia ya kituo hicho pamoja na changamaoto pamoja na mafanikio waliyoyapata. Pia amewashukuru wafanyakazi wa bima ya Britam kwa kuwapa msaada huo.
Baadhi ya wafanyakazi wa bima ya Britam wakimsikili katibu Mtendaji w

KAIMU MKURUGENZI RAHCO AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA USIKU KATIKA MRADI WA RELI YA KISASA




Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO), Masanja Kadogosa (wa pili kulia) akiongozwa na Meneja Mradi wa reli ya Kisasa ya Standard gauge kutoka RAHCO, Maizo Mgedzi (kushoto) pamoja na Meneja mradi huo kutoka kampuni inayotekeleza mradi huo ya YAPI Merkezi kutoka Uturuki, Abdullah Milk mara baada ya kufika eneo la Soga – Kibaha jumamosi usiku kuona endapo wakandarasi wa mradi huo wanafanya kazi usiku na mchana kama walivyosema katika mkataba wao na serikali.
Meneja Mradi wa reli ya Kisasa ya Standard gauge kutoka RAHCO, Maizo Mgedzi akitoa ufafanuzi juu ya mradi.
Watanzania waliopata nafasi ya kufanyakazi katika mradi wa reli ya Kisasa ya Standard gauge wametakiwa kufanya kazi kwa uweledi na kuacha ubabaishaji.

Ujumbe huo aliutoa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO), Masanja Kadogosa wakati alipofanya ziara ya kushtukiza usiku wa jumamosi katika kambi mbalimbali za mradi huo zilizopo Pugu mpaka eneo la Soga Kibaha ili kuona endapo wakandarasi wa mradi huo wanafanya kazi usiku na mchana kama walivyosema katika mkataba wao na serikali.

Kadogosa alisema mradi huo unatakiwa kwenda kwa kasi na kukamilika haraka hata kabla ya muda husika hivyo kila mtu atakayefanya kazi katika mradi huo anakikishe anafanya kazi na sio ubabaishaji utakaopelekea mradi huo kuchelewa.

Aidha Kadogosa alisema wamefikia makubaliano ya kufanya kazi usiku na mchana ili kuharakisha mradii huo na wakandarasi wanafanya haraka na kwa ukubwa wa mradi huu ni lazima tufanye kazi usiku na mchana.

“Kama mnakumbuka wakati Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Makame Mbarawa alipokuja hapa alisema ni lazima twende kasi na wakandarasi wetu wameamua kwenda na kasi na sasa mnaona tuta linaendelea vizuri ni lazima mradi huu ufanywe usiku na mchana kutokana na ukubwa wake,”alisema.