Naibu
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Atashasta Nditiye (Wa 
pili kulia) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Eng. Joseph 
Nyamhanga (Kushoto) wakati alipokaribishwa katika ofisi za Wizara leo 
Jijini Dar es Salaam, Kushoto ni Katibu Mkuu Sekta ya Uchukuzi Dkt. 
Leonard Chamuriho na Wa pili kushoto Katibu Mkuu Dkt. Maria Sasabo 
(Sekta ya Mawasiliano).
 Waziri
 wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawailiano, Prof. Makame Mbarawa (Kushoto), 
akisalimiana na Naibu Waziri Eng. Atashasta Nditiye (Kulia), wakati 
alipomtembelea Waziri Mbarawa ofisini kwake leo Jijini Dar es Salaam. Wa
 pili kulia ni Katibu Mkuu Sekta ya Uchukuzi Dkt Leonard Chamuriho 
 Waziri
 wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawailiano, Profesa Makame Mbarawa (Kulia) 
akisalimiana na Naibu Waziri hiyo Mhe. Elias Kwandikwa wakati 
alipomtembelea Waziri Mbarawa ofisini kwake leo Jijini Dar es Salaam. 
 Waziri
 wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawailiano, Prof. Makame Mbarawa (Katikati) 
akizungumza na Manaibu Waziri wa Wizara hiyo Eng. Atashasta Nditiye (Wa 
pili kulia) na Mhe. Elias Kwandikwa (Wa tatu kulia), wakati 
walipomtembelea ofisini kwake leo Jijini Dar es Salaam.
 Naibu
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Atashasta Nditiye 
(aliyesimama) akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa (Wa kwanza kulia), mara baada ya 
kuapishwa Jijini Dar es Salaam leo. 
 Naibu
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Atashasta Nditiye 
(aliyesimama) akieleza jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawailiano, Prof. Makame Mbarawa (Wa kwanza kulia), leo Jijini Dar es 
Salaam kabla ya kikao kazi na Makatibu Wakuu wa wizara na baadhi ya 
Watendaji waliopo jiji Dar es Salaam leo.
Waziri
 wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawailiano, Profesa Makame Mbarawa (Kulia) 
akiwakabidhi manaibu Waziri wa Wizara hiyo Eng. Atashasta Nditiye 
(Kulia) na Mhe. Elias Kwandikwa wakati (Katikati) vitabu vya bajeti ya 
mwaka wa fedha 2017/18 ya Wizara hiyo kama mwongozo wa utendaji kazi 
mara baada ya kuapishwa jijini Dar es Salaam leo.
Waziri
 wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Prof. Makame Mbarawa amewataka 
wafanyakazi wote katika sekta ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kufanya
 kazi kwa uadilifu na ushirikiano katika kuwahudumia Watanzania ili 
kufikia malengo ya Wizara.
Prof.
 Mbarawa ameyasema hayo jana katika mapokezi ya Manaibu Mawaziri wapya 
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ofisini Jijini Dar Es Salaam baada ya
 kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt John Pombe
 Magufuli Ikulu Dar es Salaam.
“Mimi
 nafurahi sana kufanya kazi katika Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano kwa sababu mimi na wafanyakazi tuko katika timu moja; 
tunafanya kazi kwa pamoja na kwa ushirikiano. Katika kipindi cha miaka 
miwili tumefanikiwa kufikia malengo mbali mbali ya serikali mfano ujenzi
 wa reli ya kisasa na barabara “ Mhe. Mbarawa amesema.
 Akiwakaribisha
 Manaibu Mawaziri hao katika Wizara hiyo Prof. Mbarawa amesema yeye 
pamoja na wafanyakazi wote wa wizara wamefurahi kupata mawaziri wapya 
ambao watafanya nao kazi kwa pamoja katika wizara hiyo.
 “Sisi
 kama viongozi tunapaswa kuwa mfano katika utendaji wetu wa kazi ili 
kujenga imani na umoja na wafanyakazi wetu. Tunapaswa kufanya kazi kwa 
uadilifu, ushirikiano na umoja kwani haya ndio masuala ya msingi katika 
utendaji kazi,” Prof. Mbarawa amesema .
Waziri
 amesema Wizara hiyo imefanya kazi nzuri na hili limewezekana kwa sababu
 sisi kama wizara tumezingatia maadili ya msingi katika utendaji wa kazi
 zetu, kuna timu nzuri ya watalaam ambao ni wachapa kazi, wana moyo wa 
kujituma na kazi zote walizozifanya zina matokeo mazuri. 
Kazi
 nzuri imefanyika, nawaomba  waheshimiwa manaibu mawaziri tufanye kazi 
kama timu moja na watalaam wetu ili tuweze kufikia malengo ambayo 
tumejiwekea katika wizara yetu, amesisitiza Waziri Mbarawa.Kwa
 upande wake Naibu Waziri anayeshughulikia Eng. Atashasta Nditiye 
anayeshughulikia Sekta ya Uchukuzi na Mawasiliano amesema kuwa 
amejipanga kufanya kazi na kulete matokea chanya na kwa maendeleo ya 
nchi.
“Nipo
 tayari kufanya kazi itakayoleta mabadiliko, tutaboresha miundombinu ili
 kuchochea kasi ya ukuaji wa viwanda na kila nitakachofanya ni 
utekelezaji wa yale amabayo Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli 
anayatarajia,” amesema mhandisi Nditiye.
Hii
 ni mara ya kwanza kwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt
 John Pombe Magufuli kufanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri tangu 
serikali yake iingie madarakani Novemba 2015.


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni