MOHAMED SALAH AIPELEKA MISRI KOMBE LA DUNIA BAADA YA MIAKA 28 KUPITA

Nyota wa Liverpool Mohamed Salah ameipelekea nchi yake ya Misri katika fainali za kombe la dunia Urusi, ikiwa ni mara ya kwanza tangu mwaka 1990 baada ya kufunga goli la penati katika dakika ya 95.

Zikiwa zimebakia dakika za lala salama Salah alijitokeza kuipiga penati muhimu dhidi ya Congo, na kuibua shamrashamra za nguvu katika dimba la Borg El Arab huko Alexandria baada ya kufunga.

Sherehe za kutinga fainali za kombe la dunia zilitapakaa mitaani, huku Jijini cairo helkopta za jeshi zikidondosha bendera kwa maelfu ya mashabiki waliokusanyika katika eneo la Tahrir square.
   Mohamed Salah akishangilia baada ya kufunga goli la penati katika dakika za mwisho
   Mashabiki wa Misri wakiwa mitaani kushangilia kutinga fainali za kombe la dunia
Nifuraha tupu jana usiku Misri baada ya kufuzu michuano ya kombe la dunia itakayofanyika Urusi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni