………………………………………
BENKI ya uwekezaji nchini TIB, imekubali kutoa shilingi bilioni 31 kugharimia ujenzi wa hospital ya rufaa ya mkoa wa Arusha, ambayo itajengwa kwenye eneo la hospital ya mkoa ya Mount Meru mapema mwaka huu.
BENKI ya uwekezaji nchini TIB, imekubali kutoa shilingi bilioni 31 kugharimia ujenzi wa hospital ya rufaa ya mkoa wa Arusha, ambayo itajengwa kwenye eneo la hospital ya mkoa ya Mount Meru mapema mwaka huu.
Mkuu wa mkoa wa Arusha, Felix 
Ntibenda, amesema kuwa tayari taratibu za kupatikana kwa fedha hizo 
ambazo ni mkopo zimekamilika na hivi karibuni kutasainiwa mkataba kati 
ya benki hiyo na ofisi ya katibu tawala mkoa ili ujenzi huo uweze kuanza
 mara moja.
Ntibenda, amesema mkoa unaendelea 
wa kuboresha,majengo na huduma ya afya kwenye hospital hiyo ya mkoa 
wakati wakisubiri hospital ya rufaa ijengwe.
Amesema,ukarabati wa hospital hiyo unaofanywa kwa kushirikiana na wadau umewezesha kuirejesha hadhi ya hospital hiyo.
Amesema kuwa mkoa umewezesha 
kuanzishwa kwa bohari la dawa la MSD,ambalo tayari maandalizi yamefikia 
95% na itafunguliwa wakati wowote na kuanza kutoa huduma za dawa kwa bei
 nafuu zaidi kuliko zinavyouzwa kwenye maduka binafsi.
Kwa upande wake,Katibu tawala mkoa
 wa Arusha, Adoh Mapunda, amesema kuwa wiki ijayo mkoa utasaini 
makubaliano ya kupatiwa mkopo na benki hiyo na kufuatiwa na hatua ya 
kutangaza zabuni ili kumpata mkandarasi atakae jenga hospital hiyo yenye
 majengo ya ghorofa tano ya hospital hiyo ya rufaa.
Amewapongeza wadau ambao 
wamejitokeza kuchangia ukarabati wa hospital hiyo ya mkoa unaoendelea na
 tayari jengo la wadi ya Grade one ,ambalo lilikuwa likihudumia kulaza 
wagonjwa katika hospital hiyo ya mkoa limefungwa likisubiri kubomolewa 
kutokana na uchakavu.
Akiwasilisha mpango kazi na mchoro
 wa jengo hilo, Mhandisi wa mkoa, Edward Amboka ,amesema kuwa hospital 
hiyo iliyojengwa mwaka 1915 majengo yake yamechakaa sana na hayafai 
kuendelea kutumika kama hospital .
Hospital hiyo ilijengwa ikiwa ni 
kambi ya kutibia majeruhi wa vita ya kwanza ya dunia hivyo mpango uliopo
 ni kujenga majengo mapya ya ghorofa na kubomoa ya zamani ambayo 
yamechakaa.
Amesema ujenzi huo utahusisha 
maeneo manane zikiwemo nyumba za watumishi ,mafunzo, mapumziko na 
maegesho ya magari.na mipango mingine ya uendelezaji wa hospitali hiyo
Amesema lengo la kujenga majengo hayo ni kupunguza mzigo wa 
wagonjwa mkoani Arusha ikiwemo vizazi na vifo vinavyotokana wakati wa 
kujifungua hivyo wanajenga jengo moja la ghorofa tano ambalo 
litatosheleza mahitaji badala ya kuwa na utitiri wa majengo
Kwa upande wake mganga mfawidhi wa
 hospital hiyo, Dakta Jacklin Urio, amesema hospital hiyo ina vitanda 
500 na ina hudumia watu milioni 1.6 kwa mwaka lakini kutokana na ukuaji 
wa mji na ongezeko la watu hospital hiyo kwa sasa haitoshelezi mahitaji 
kutokana na wingi wa watu.
Amesema kuwa ujenzi wa hospital 
mpya ya rufaa utaiwezesha hospital ya rufaa kuwa na vitanda 600 
,kutakuwa ni vitanda 50 kwa ajili ya wagonjwa mahututi, ICU, na kati 
yake vitatu ni kwa ajili ya watu maalumu (VIP) wakiwemo viongozi wa 
kitaifa na kimataifa .
Jengo la Grade A,lilikuwa na 
vitanda 6,lakini kwa sasa halikidhi mahitaji na jengo jipya litakuwa na 
maabara ,wataalam, vitanda 50 vya wagonjwa wa Mahututi,(ICU) na huduma 
zingine .
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni