BONDIA DAVID HAYE AREJEA KWA KISHINDO ULIONGONI

Bondia David Haye amerejea kwa kishindo uliongoni baada ya kupumzika kwa muda wa miaka mitatu na nusu, kwa kumdunda kwa KO, Mark de Mori katika pambano lililofanyika Jijini London.

Bondia Muastralia De Mori alionekana kuchanganyikiwa mapena na ngumi ya kwanza aliyoirusha Haye na baada ya hapo aliishia kuonekana kuwa ameelemewa.

David Haye, 35, alimaliza pambano hilo kwa ngumi nzito ya mkono wa kulia ambayo ilimfanya De Mori kupoteza fahamu na kuanguka chini ikiwa zimebakia dakika 49 katika raundi ya kwanza ya mpambano huo.
                     Bondia David Haye akimtandika ngumi ya kichwani Mark de Mori 
     Ngumi nzito ya Haye iliyomuingia barabara de Mori na kupata kizunguzungu
                       David Haye akimalizi kazi kwa ngumi iliyompeleka chini de Mori
          Haye aliyepandwa na mzuka akizuiwa na refa asije akauwa mtu ulingoni

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni