ZIARA YA MAJALIWA RUANGWA


rugwe-3
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na vikongwe wa kijiji cha Nandandala wilayani Ruangwa baada ya kuhutubia mkutano wa hadhara kijijini hapo akiwa katika ziara ya jimbo lake la uchaguzi la Ruangwa , Desemba 28, 2016.
rugwe-4
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi wa kijiji cha Namilema wilayani Ruangwa akiwa katika ziara ya jimbo lake la uchaguzi, Desemba28, 2016.
rugwe-2
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wananchi wa kijiji cha Nandandala wilayani Ruangwa akiwa katika ziara ya jimbo lake la uchaguzi la Ruangwa Desemba 28, 2016.
rugwe-5Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Namilema wialyani Ruangwa wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao akiwa katika ziara ya jimbo lake la uchaguzi la Ruangwa Desemba 28, 2016. rugwe-1
rugwe
   Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Namkunjera wilayani Ruangwa wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kijijini hapo akiwa katika ziara ya jimbo lake la Ruangwa Desemba 28, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

RAIS DKT. MAGUFULI ASHIRIKI MSIBA WA MZEE MAARUFU WA CHATO ADMIRABILIS MBABE MANYAMA (82) CHATO MKOANI GEITA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpa pole Bi Mugwe Mbabe ambaye ni Mke mkubwa wa Marehemu Mzee Maarufu Admirabilis Mbabe Manyama(82) mara baada ya kuwasili nyumbani kwa marehemu Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpa pole Bi. Regina Mbabe mke mdogo wa Marehemu Mzee Maarufu Admirabilis Mbabe (82) Manyama mara baada ya kuwasili nyumbani kwa marehemu Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Deodatus Manyama wakwanza (kushoto) ambaye ni mdogo wa marehemu Marehemu Mzee Admirabilis Mbabe Manyama(82) mara baada ya kuwasili nyumbani kwa Marehemu Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Bi. Mugwe Mbabe mke mkubwa wa Marehemu Mzee Admirabilis Mbabe Manyama mara baada ya kuwasili nyumbani kwa marehemu Chato mkoani Geita
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaini daftari la maombolezo mara baada ya kuwasili nyumbani kwa marehemu Mzee Admirabilis Mbabe Manyama (82) Chato mkoani Geita
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na kutoa pole katika msiba huo wa Marehemu Mzee Admirabilis Mbabe Manyama mara baada ya kuwasili nyumbani kwake Chato mkoani Geita

JESHI LA POLISI ARUSHA:WATAKAOCHOMA MATAIRI,FAINI MILIONI NNE,MADEREVA WALEVI KUKAMATWA NA KUNYANG'ANYWA LESENI,WAZAZ I/WALEZI WATAKAOWAACHA WATOTO WAKAZURURA OVYO KUSHTAKIWA,WENYE VIBALI VYA KUFYATUA FATAKI KUTUMIA DAKIKA TATU TU

Image result for kamanda wa polisi
charles mkumbo 
Na.Mahmoud Ahmad,Arusha.


Jeshi la polisi mkoani Arusha limesema kuwa katika kusheherekea mwaka mpya ,kumekuwa na kasumba kwa baadhi ya watu kufanya matukio ya kuhatarisha usalama kwa kuchoma matairi,kupanga mawe barabarani,na hata kuwarushia mawe askari pindi wanapothibiti matukio hayo,haswa maeneo ya majengo,kwa mrombo,kwa mrefu huku wengine wakitumia mwanya huo kufanya uhalifu.


Kwa wale watakaochoma na watakaokamatwa wamechoma matairi barabarani,wakumbuke kwamba watashtakiwa kwa sheria za Tanroad, ambapo watatakiwa kulipa faini isiyopungua milioni nne


Lakini pia baadhi ya madereva huwa wanatumia vilevi kupita kiasi katika majumba ya starehe inapofika saa 00:00 usiku unapoanza mwaka mpya huwa wanashangilia kwa kuendesha vyombo vyao kwa mwendo kasi na kupiga honi mitaani huku wakiwa wamepakia watu kwa kuwaning’iniza milangoni kama njia ya kuonyesha furaha zao.


Uzowefu unaonyesha kwamba maeneo ya sakina mpaka kwa iddi baadhi ya madereva wanatuamia magari aina ya altezana Subaru huwa wanafanya maonyesho kwa kuendesha mwendo kasi vyombo hivyo huku vikitoa sauti kama risasi.


Kwa upande wa wamiliki wa bar wazingatie masharti ya leseni zao ambazo zinaonyesha muda halisi wa kufunga na wasiwe na tama ya kuendelea kupata pesa baada ya kuona wateja wengi katika biashara ,hali kadhalika wamiliki wa kumbi na maeneo mengine ya starehe wanatakiwa kuzingatia usalama katika maeneo yao hasa kwa kuweka wasimamizi na kutojaza watu kupita kiasi.


Aidha wazazi na walezi tunawakumbusha pamoja na kusheherekea mwaka mpya wa 2017 wasisahau majukumu yao ya kuwa makini na watoto kwa kutowaacha peke yao na hata kutoacha mtu yeyote katika majumba ili kuondokana na matukio yanayoweza kuepukika sambamba na kuangalia watoto wao katika maeneo ya round about hasa kijenge mnara wa mwenge,wasizagae barabarani


Jeshi la polisi linatoa onyo kwa baadhi ya watu watakaofanya makosa yaliyoorodheswa hapo juu ,tutawakamata na kuwachukulia hatua za kisheria wawe wahalifu ,wamiliki wa bar na kumbi nyingine za starehe pamoja na wazazi au walezi na madereva walevi ambao pia watapima na ikithibitika wamevuka viwango tutawafungia leseni.


Kwa upande wa waaliomba vibali vya kufyatua fataki ,watatakiwa watumie dakika tatu na wote kwa pamoja watatakiwa kufyatua saa 00:00 na pia hawataruhusiwa kufyatua katika makazi ya watu.


Tutahakikisha nyumba zote za ibada ,kumbi za starehe na maeneo mengine kutakuwa na ulinzi wa kutosha ambapo askari watakuwa katika doroa za miguu na doria za magari kila kona ya jiji la Arusha na wilaya zote za mkoa huu ,hivyo waumini wa dini mbalimbali wasiwe na hofu pindi watakapokuwa wanaendelea na ibada.


Kama ilivyo kwa nyakati zote tunawaomba wananchi waendelee kushirikiana nasi katika kuwabaini na kuwafichua wahalifu na uhalifu ili kuimarisha amani na utulivu uliopo.


Mwisho tunatoa shukrani za dhati kwa vyombo vya habari radio,magazeti,blogs,televisheni,kwa  ushirikiano mkubwa mnaotoa kwa jeshi la polisi mkoa wa Arusha kwa kuwa mbele katika kufichua, kuelimisha,na kuhabarisha umma juu ya uhalifu.


Jeshi la polisi mkoa wa Arusha tunawatakia heri ya mwaka mpya wa 2017 wakazi wote wa Arusha .


       IMETOLEWA NA KAMANDA WA POLISI MKOA WA ARUSHA

                         NAIBU KAMISHANA WA POLISI

                          (DCP)CHARLES MKUMBO

                                  TAREHE 29/12/2016

MAAMUZI YA RUFAA YA KESI YA LEMA KUJULIKANA 4 JANUARI 2017




Na.Mahmoud Ahmad Arusha.

Mahakama kuu kanda ya Arusha imesikiliza maombi ya rufaa yayaliyowasilishwa na upande wa jamhuri na ule wa mshtakiwa Godbless Lema ambapo pande zote mbili wamekubaliana kusikilizwa rufaa ya upande wa jamhuri ambapo upande wa serikali wameiomba mahakama kuwasilisha kwa hati ya maandishi hapo kesho tarehe 30 disemba 2016

Aidha rufaa hizo ni pamoja na ile ya upande wa Jamhuri kutoridhika na maauzi ya Jaji Dkt. Modesta Opiyo la kuwapa siku kumi (10) upande wa mshtakiwa Lema kufaili notisi ya rufaa ,na upande wa wamshtakiwa ni ile ya kupinga uamuzi wa mahakama ya chini kushindwa kumpa lema masharti ya dhamana

Jaji aliyekuwa anasikiliza kesi ya rufaa hizo Salma Magimbi amesema kuwa mara baada ya upande wa jamhuri kuleta rufaa kwa njia ya maandishi upande wa mshtakiwa Lema wataijibu tarehe 30 disemba 2016 ambapo tarehe 2 januari watakutana pande zote kwaajili ya kufanya majumuisho na maamuzi ya rufaa hiyo yatatolewa tarehe 4 januari 2017

Hata hivyo baada ya kusikiliza rufaa hizo mahakama imeibua hoja yenyewe na kuwapa kazi mawakili wa pande zote mbili kuangalia kuwa notisi iliyowasilishwa na mahakama ya chini imekidhi matakwa ya kisheria?

Kwa upande wa wakili wa mshtakiwa Peter Kibatala amesema kuwa kwa upande wao wameiomba mahakama kusubirisha rufaa yao ili wasikilize kwanza rufaa ya upande wa jamhuri kwani rufaa zote zimegongana na zinaelekea sehemu moja  

"Unajua leo rufaa mbili zimegongana ile ya upande wa jamhuri na ile ya kwetu sisi,hivyo basi sisis tumeiomba mahakama kusitisha rufaa yetui isikilizwe ile ya serikali kwanza,kwani rufaa zote zinaelekea upandemmoja ,wandege apande ndege na wa basi apande basi "alisema Kibatala.

Hata hivyo mbunge huyo wa Arusha mjini Godbless lema amerudishwa rumande hadi hapo maamuzi yatakapotolewa na mahakama.

WENGI WAJITOKEZA KWENYE MSIBA WA MPOKI BUKUKU TABATA

Mhariri Mtendaji wa gazeti la Mtanzania, Absalom Kibanda akimfariji mjane wa marehemu Mpoki Bukuku, Lilian nyumbani kwa marehemu, Tabata Bwawani, Dar es Salaam. Bukuku alifariki juzi baada ya kugongwa na gari Barabara ya Bagamoyo karibu na Kituo cha ITV, Mwenge. PICHA NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
                               Kibanda akimfariji mama mzazi wa marehemu Mpoki Bukuku
Kiongozi wa Chama cha ACT, Zitto Kabwe (kulia) akizungumza jambo na Shemeji wa marehemu Mpoki Bukuku, Edwin Mjwahuzi alipokwenda kuwafariji wafiwa nyumbani kwa marehemu, Tabata Bwawani.
Zitto Kabwe (kulia) akizungumza na kaka wa Marehemu Mpoki, Gwamaka Bukuku wakati wa msiba huo
Waandishi wa habari wakiwa kwenye msiba wa marehemu Mpoki Bukuku ambaye alikuwa Mpigapicha mwandamizi wa magazeti ya Kampuni ya The Guardian
                                      Wanahabari wakijadiliana mambo wakati wa msiba huo
Mmiliki wa Blogu hii, Kamanda Richard Mwaikenda, ambaye pia ni Mpigapicha Mkuu wa gazeti la Jambo Leo, Kamanda Richard Mwaikenda (kulia) akiwa na wanahabari wenzie kwenye msiba huo.Kutoka kushoto ni Mpigapicha wa Waziri Mkuu, Hilary Bujiku, Mmiliki wa Blog ya K-VIS, Khalfan Said, Mmiliki wa Blog ya Michuzi, ambaye pia ni Mpiga Picha na Mwandishi wa Habari Msaidizi wa Rais, Muhidini Issa Michuzi, Mpigapicha Mkuu wa Gazeti la Mwananchi, ambaye ni shemeji wa marehemu Mpoki, Edwin Mjwahuzi na Francis Chirwa ambaye ni mmoja wa viongozi wa Bodi ya Wahariri wa Gazeti la Raia Mwema. 
                                                                            Waombolezaji wakiwa kwenye msiba
Jirani rafiki wa karibu wa marehemu, Mpoki, maarufu kwa jina la Mijisu akilia wakati wa msiba

RAIS DKT. MAGUFULI PAMOJA NA MKEWE MAMA JANETH WASHIRIKI IBADA YA KRISMASI KATIKA KANISA KATOLIKI (KANISA KUU LA MOYO MTAKATIFU WA YESU) MKOANI SINGIDA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli wakiwa katika Misa ya Krismasi katika Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida.                                                                                                      Hapa wakiwa katika sala.
                                                                                    
Rais Magufuli na mkewe wakisilkiliza neno
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwasalimia waumini wa Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida mara baada ya kushiriki Misa ya Krismasi katika kanisa hilo mkoani Singida
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia waumini wa Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida mara baada ya kushiriki Misa ya Krismasi katika kanisa hilo mkoani Singida.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Baba Askofu wa Jimbo la Singida Askofu Edward Mapunda mara baada ya Ibada ya Krismasi katika Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Baba Askofu wa Jimbo la Singida Askofu Edward Mapunda mara baada ya Ibada ya Krismasi katika Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida.

Baba Askofu wa Jimbo la Singida Askofu Edward Mapunda akimuombea na kumbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya Ibada ya Krismasi katika Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli wakisalimiana na waumini wa Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida mara baada ya ibada ya Krismasi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli wakipunga mkono wakati wakitoka kwenye Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu mkoani Singida. PICHA NA IKULU

NYOTA WA POP GEORGE MICHAEL AFARIKI DUNIA



Mwanamuziki nyota wa muziki wa Pop George Michael amefariki dunia jana baada ya moyo wake kushindwa kufanya kazi akiwa nyumbani kwake huko Oxfordshire Uingereza.

Mwanamuziki huyo aliyeanza muziki katika miaka 80, na kupata mafanikio zaidi akiimaba peke yake nje ya bendi, amefariki dunia kwa amani jana siku ya Krismasi, kwa mujibu wa msemaji wake.

Mwanamuziki mwenzake wa zamani wa bendi ya Wham! Andrew Ridgeley amesema amevunjika moyo kuwa kumpoteza rafiki yake kipenzi.
           George Michael akiwa na Andrew Ridgeley wakiimba pamoja na bendi ya Wham !
Picha hii inaaminika kuwa ni picha ya mwisho kupiga George Michael hii ilikuwa Septemba mwaka huu akipata mlo wa usiku na rafiki yake

RC GAMBO AZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI ARUSHA

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akizungumza na waandishi wa habari wa Mkoa wa Arushaa ofisini kwake juzi kutoka vyombo mbalimba vya habari kuhusu sakata la kukamatwa kwa mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha ITV Halfani Liundi ambapo amehaidi kulishughulikia huku akiwataka waandishi kufanya kazi zao kwa kuzingatia maadili ya uandishi wa habari
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu mwandishi wa kituo cha ITV Halfani Liundi aliyekamatwa hivi karibuni na jeshi la polisi, ambapo pamoja na mambo mengine alisema kuwa anatambua umuhimu wa vyombo vya habari na hivyo mwandishi ana uhuru wa kwenda popote kupata taarifa yeyote kwa kuzingatia misingi ya uandishi wa habari
Mwandishi wa habari wa kituo cha channel Ten Aristrides Dotto akichangia katika mkutano huo wa waandishi wa habari na mkuu wa Mkoa juzi ofisinii kwake jijini Arusha
                            Baadhi ya waandishi wa habari wakifatilia mkutano huo
Mwandishi wa gazeti la Mwananchi Mosses Mashalla akichangia katika mkutano huo wa mkuu wa Mkoa na waandishi wa habari mkoa wa Arusha. (Picha zote na Mahmoud Ahmad arusha)

VYOMBO VYA HABARI HAVIKUTANGAZA WAGOMBEA WANAWAKE,VIJANA NA MAKUNU -TAFITI YABAINISHADI

Afisa mratibu wa umoja wa mataifa kitengo cha wanawake Rashida Shariff akifungua warsha ya siku mmoja iliyokuwa na lengo la kujadili ripoti ya uchaguzi mkuu kwa wagombea wanawake,vijana na makundi maalumu iliyofanyika kwenye Hotel ya Lush Garden jijini Arusha mwishoni mwa wiki iliyopita picha zote na mahmoud ahmad wa globu ya jamii
Mratibu wa semina hiyo Edson Msofe kutoka TAMWA akiwa na Rashida Sharifu kutoka UN WOMEN wakifuatilia jambo kwenye warsha iliyoandaliwa na chama cha waandishi wa habari wanawake hapa nchini(TAMWA)kwa kushirikiana na UN WOMEN na kuwashirikiasha wagombea wanawake,vijana na walemavu

VIONGOZI KUTOKA VYAMA VYA SIASA WAKIFUATILIA WARSHA HIYO

Mweneykiti wa chama cha walemavu ambaye pia alikuwa mgombea kwenye uchaguzi mkuu akiteta jambo na aliyekuwa mgombea wa kiti cha uraisi kupitia chama cha ACT wazalendo Anna Mghwira wakibadilishana mawili matatu kabla ya kuanza kwa warsha hiyo

sehemu ya washiriki wakifuatilia warsha hiyo

WAHARIRI WA REDIO  ZA JIJINI ARUSHA Baraka Sunga na Joseph Laizer AIDEA FM NA SUNRISE WAKIWA NA MWANDISHI WA  CLOUDS TV Beatrise gerald


Makundi yakichangia maoni yao katika warsha hiyo

Wagombea wanawake waliogombea kwenye uchaguzi mkuu uliopita wilayani Meru wakiteta jambo wakati wa warsha hiyo

Kundi la waandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali walioshiriki warsha hiyo wakijadiliana mada kwenye warsha hiyo ya siku mmoja

WAGOMBEA NA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAKIFUTILIA WARSHA HIYO ILIYOANDALIWA NA TAMWA NA UN WOMEN KWA WAGOMBEA WAANDISHI WA HABARI VIJANA NA MAKUNDI MAALUMU

Washiriki wakifuatilia jambo wakti semina ikiendelea

Mwandishi wa habari wa gazeti la Dail News Hazla quire akiwa na mwandishi wa mwananchi Zulfa Mussa na Mwandishi wa Channel 10 Arstide Dotto wakifuatilia kwa karibu warsha hiyo ambapo imedaiwa kuwa wagombea wanawake waliombwa hadi rushwa ya Ngono ili wapate Airtime kutoka kwa wanahabari picha zote na globu ya jamii Arusha.


                        Na Mahmoud Ahmad Arusha
Wadau wa maendeleo,viongozi wa siasa na vyombo vya habari wanalojukumu la kuhakikisha wanahamasisha wanawake, makundi maalum na vijana kuomba nafasi za uongozi kwa wingi ilikuweza kuwa na usawa wa kijinsia kwenye masuala mbalimbali ya kujiletea Mandeleo,

Hayo yamebainishwa kwenye warsha ya siku moja iliyowashirikisha wagombea wanawake,makundi maalum na vijana,wanahabari, pamoja na viongozi wa vyama vya siasa iliyoandaliwa kwa pamoja na TAMWA na UN WOMEN na kufanyika wilayani Arumeru mkoani hapa.

Akizungumza wakati akitoa mada mratibu wa semina hiyo Rashida Shariff alisema kuwa warsha hiyo ni kushirikiana matokeo ya ripoti ya uchambuzi na kujadili changamoto walizopata wagombea wanawake,makundi maalumu na vijana katika kipindi cha uchaguzi  kwa vyombo vya habari hapa nchini kutoripoti ipasavyo habari zao kutokana na vyombo hivyo kuwa ni vya kibiashara zaidi.

Alisema kuwa malengo ya warsha hiyo ni kujadili changamoto za uchaguzi mkuu na nini kifanyike,ambapo wanatambua vyombo vya habari  ni chanzo mojawapo katika kuwatoa wananchi katika giza na kuwapeleka katika mwanga ili kusaidia na kuibua changamoto ya kuweza kufikisha taifa katika usawa wa kumfanya mwanamke,makundi maalumu na vijana kuwa nao wanauwezo sawa  na wengine ambapo wanasiasa wanawake,makundi maalumu na vijana kama watapewa kipaumbele cha kupata nafasi ya habari zao kuripotiwa na vyombo hivyo kila mara.

“Warsha hii ni kufuatilia jinsi vyombo vya habari vilivyoripoti taarifa za wanawake na vijana katika kugombea kwenye uchaguzi mkuu uliopita na kupata uchambuzi wa dhana ya kijinsia katika vyombo vya habari juu ya usawa wa kijinsia katika huduma za jamii na uongozi”alisema Shariff

Kwa upande wake Katibu wa chama cha wananchi (CUF)mkoani hapa Zuberi Mwinyi alisema kuwa lazima kuwe na mabadiliko kwa wanahabari kupewa semina za mara kwa mara ilikusaidia wanawake,makundi maalumu na vijana kwa sababu tasnia ya habari ndio nyenzo ya kumtoa mtu kutoka eneo moja kwenda jingine.

Alisema kuwa tofauti na hapo watanzania watajiona hakuna kinachoendelea kwa kuwa hakuna tathmini ya mabadiliko katika sekta ya kuwasaidia wanawake,makundi maalum na vijana iliweze kufikia malengo ya kuwa na usawa wa kijinsia katika jamii wanaoishi.

Nae Mjumbe wa halmashauri kuu ya Uvccm mkoani hapa Saitoti Zelothe alisema kuwa ifike mahali wanawake,makundi maalum na vijana wakasaidiwa kukuwa kiuchumi na kuweza kwenda sambamba na wagombea wengine kwani suala la gharama za kifedha katika uchaguzi halikwepiki na limekuwa mwiba kwa wagombea wa kundi hilo kukosa mwamko wa kugombea.
Mwisho…………………………………………………………….