RC GAMBO AZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI ARUSHA

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akizungumza na waandishi wa habari wa Mkoa wa Arushaa ofisini kwake juzi kutoka vyombo mbalimba vya habari kuhusu sakata la kukamatwa kwa mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha ITV Halfani Liundi ambapo amehaidi kulishughulikia huku akiwataka waandishi kufanya kazi zao kwa kuzingatia maadili ya uandishi wa habari
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu mwandishi wa kituo cha ITV Halfani Liundi aliyekamatwa hivi karibuni na jeshi la polisi, ambapo pamoja na mambo mengine alisema kuwa anatambua umuhimu wa vyombo vya habari na hivyo mwandishi ana uhuru wa kwenda popote kupata taarifa yeyote kwa kuzingatia misingi ya uandishi wa habari
Mwandishi wa habari wa kituo cha channel Ten Aristrides Dotto akichangia katika mkutano huo wa waandishi wa habari na mkuu wa Mkoa juzi ofisinii kwake jijini Arusha
                            Baadhi ya waandishi wa habari wakifatilia mkutano huo
Mwandishi wa gazeti la Mwananchi Mosses Mashalla akichangia katika mkutano huo wa mkuu wa Mkoa na waandishi wa habari mkoa wa Arusha. (Picha zote na Mahmoud Ahmad arusha)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni